RUSHWA: Laini za uwakala wa TiGO-PESA na M-PESA zauzwa na wafanyakazi kwa dau refu!

RUSHWA: Laini za uwakala wa TiGO-PESA na M-PESA zauzwa na wafanyakazi kwa dau refu!

Rich Dad

JF-Expert Member
Joined
Dec 15, 2010
Posts
748
Reaction score
135
HII nchi inakokwenda sijui ni wapi? PCCB wamelala usingizi mzito. Hawana msaada wowote kusaidia kukomesha katabia ka baadhi ya wafanyakazi wa hizi kampuni za simu zenye kuuza laini za uwakala kinyume cha taratibu. Unakuta mtu kakamilisha taratibu zote za usajili, lakini kinachotokea hawa jamaa wana ku-delay makusudi ili uwakatie kitu kidogo. Kwa sasa hawa jamaa wanataka TZS 100,000 hadi TZS 300,000 kwa laini moja.
Ukijifanya wewe ni mtu wa kufuata taratibu basi jua itakuchukua zaidi ya miezi sita kupata laini. Kila siku utapigwa kalenda kwamba kuna hiki na hiki kinakosekana. Sasa hivi TiGo wanatumia mgogo wa TCRA kwamba ndio wanaobania watu wasipate laini, lakini ukigawa chenji .....fasta ndani ya siku moja au mbili unakuwa umepata line.
Haya nayasema si kwamba nimehadithiwa, ni kwamba yamenikuta mimi mwenyewe.
Wadau naombeni tu mnipe taratibu za nani nimuone pale TiGO na Voda ili niwasilishe barua yangu ya malalamiko pamoja na vithibitisho kwa jinsi rushwa inavyokwamisha juhudi za watu kujikwamua na umaskini.
 
Hii nchi inakokwenda sijui ni wapi? PCCB wamelala usingizi mzito. Hawana msaada wowote kusaidia kukomesha katabia ka baadhi ya wafanyakazi wa hizi kampuni za simu zenye kuuza laini za uwakala kinyume cha taratibu. Unakuta mtu kakamilisha taratibu zote za usajili, lakini kinachotokea hawa jamaa wana ku-delay makusudi ili uwakatie kitu kidogo. Kwa sasa hawa jamaa wanataka TZS 100,000 hadi TZS 300,000 kwa laini moja.
Ukijifanya wewe ni mtu wa kufuata taratibu basi jua itakuchukua zaidi ya miezi sita kupata laini. Kila siku utapigwa kalenda kwamba kuna hiki na hiki kinakosekana. Sasa hivi TiGo wanatumia mgongo wa TCRA kwamba ndio wanaobania watu wasipate laini, lakini ukigawa chenji .....fasta ndani ya siku moja au mbili unakuwa umepata line.
Haya nayasema si kwamba nimehadithiwa, ni kwamba yamenikuta mimi mwenyewe.
Wadau naombeni tu mnipe taratibu za nani nimuone pale TiGO na Voda ili niwasilishe barua yangu ya malalamiko pamoja na vithibitisho kwa jinsi rushwa inavyokwamisha juhudi za watu kujikwamua na umaskini.
 
mimi ilichukua miezi minne kupata M-PESA nilikwenda tigo wakaniambia huduma imesitishwa hadi August sijui ni kweli hili au ndio wanataka rushwa
 
ok- nimeshawapa taarifa!

hapo ndo umetenda haki, sio kuwashutum. Angalia watakavyofanyia kazi japokuwa usha haribu kazi yao, kwani tayari wahusika watakuwa makini, ikumbukwe nao wanapita jf
 
Wape TiGO laki moja uone kama hupati laini ndani ya siku mbili!

mimi ilichukua miezi minne kupata M-PESA nilikwenda tigo wakaniambia huduma imesitishwa hadi August sijui ni kweli hili au ndio wanataka rushwa
 
Jamani mbona mnanikatisha tamaa maana jana ndio nimekamilisha Leseni ya Biashara na nimemwomba kijana wangu achukuwe formu zakuomba hizo line sasa kama itanichukuwa miezi sita nitafanyaje jamani?
Kuna mtu alijitokeza kwamba anasadiai kupata MPESA hapa hapa Jamii forums lakini naona kama haeleweki ?
JAMANI LINE YENYEWE NI GHALI SANA KAMA MTANDAO WA TIGO NASIKIA NI MILLION NA VODA NI LAKI 4 SASA UTAPATA WAPI TENA ZA KUWAPA JAMANI WATANZANIA TUWE NA HURUMA KIDOGO
MAISHA NI MAGUMU
 
We wape uendelee na mambo yako...!!!
System imeshaharibika, kama wezi wakubwa hawashikwi we unataka wadogo wafanyeje>....>??
Kila mtu anatikwa atengeneza system ya kula alipo, kwani si hata pccb wana sehemu zao za kula??
INGAWA KOSA NI KOSA TU...,Ila system ya kimaisha imeshahalibika,so kuombwa kutoa iyo pesa kwaajili ya Line za PESA so issue,kila sehemu kumehalibika.....!!
 
Ningependa sana mtu kutoka vodacom aje ajibu hii mambo hapa mana mimi nilikaa miezi 4 bila kupewa till namba ilihali nilishamaliza taratibu zao. waweke wazi kwamba unatakiwa utoe kitu kidogo na kiwe oficially mambo ya nani anamjua nani ndio upate huduma hayana nafasi kwenye biashara ya ushindani. na biashara haitambui kujuana...
 
Nadhani umechelewa sana kutoa lalamiko hadi lime expire. Kwa miezi kadhaa sasa vodacom na tigo hawatoi uwakala direct bali kupitia aggregators au wakala wakuu. Hiyo hakuna popote mtu anaye taka uwakala anaingiliana directly na wafanya kazi wa kampuni hizo.
 
Nadhani umechelewa sana kutoa lalamiko hadi lime expire. Kwa miezi kadhaa sasa vodacom na tigo hawatoi uwakala direct bali kupitia aggregators au wakala wakuu. Hiyo hakuna popote mtu anaye taka uwakala anaingiliana directly na wafanya kazi wa kampuni hizo.

Na tigo wamesitisha kusajili mawakala?
 
Muwe mnawahisha malalamiko ili 'tukiwalaani' wahusika laana 'ziwashike'
 
Tigo wamesitisha kutengeneza till mpya. Wanataka kwanza wawapokonye wale ambao till zao hazifanyi kazi vizuri waziswap wawape wengine. Baadaye wataendelea kutengeneza till.
 
Hii nchi inakokwenda sijui ni wapi? PCCB wamelala usingizi mzito. Hawana msaada wowote kusaidia kukomesha katabia ka baadhi ya wafanyakazi wa hizi kampuni za simu zenye kuuza laini za uwakala kinyume cha taratibu. Unakuta mtu kakamilisha taratibu zote za usajili, lakini kinachotokea hawa jamaa wana ku-delay makusudi ili uwakatie kitu kidogo. Kwa sasa hawa jamaa wanataka TZS 100,000 hadi TZS 300,000 kwa laini moja.
Ukijifanya wewe ni mtu wa kufuata taratibu basi jua itakuchukua zaidi ya miezi sita kupata laini. Kila siku utapigwa kalenda kwamba kuna hiki na hiki kinakosekana. Sasa hivi TiGo wanatumia mgongo wa TCRA kwamba ndio wanaobania watu wasipate laini, lakini ukigawa chenji .....fasta ndani ya siku moja au mbili unakuwa umepata line.
Haya nayasema si kwamba nimehadithiwa, ni kwamba yamenikuta mimi mwenyewe.
Wadau naombeni tu mnipe taratibu za nani nimuone pale TiGO na Voda ili niwasilishe barua yangu ya malalamiko pamoja na vithibitisho kwa jinsi rushwa inavyokwamisha juhudi za watu kujikwamua na umaskini.

Tafuta wakala mkuu (Aggregator) upate usajili wako mara moja au ukipenda wasiliana nami 0754485762 nikupe procedures na utaidhinishwa kuwa wakala kwa muda mfupi sana na ni BURE kabisa.
 
hii ni kweli kabisa huwa ni kazi sana kuapply hizo line ingawa mimi nlipata zote huu ndo msoto wangu...MPESA nilipitia kwa wakala nikiwa na business licence na mil 1 ikachukua wiki 3 hadi 4 kupata line...sikusumbuka sana.... tigo pesa-nilipitia kwa wakala mkuu kama kawa ila waliniambia imesitishwa had miez mi3 mbele nilingoja nikaapply nikakaa miez mi2 tena hadi kpata hyo line kiukweli tigo wasumbufu sana..zantel na airtel ilichukua 30mins kupata hizo line
 
yaani acha kabisa juzi nmenunua line ya mpesa standalone laki 5
 
HII nchi inakokwenda sijui ni wapi? PCCB wamelala usingizi mzito. Hawana msaada wowote kusaidia kukomesha katabia ka baadhi ya wafanyakazi wa hizi kampuni za simu zenye kuuza laini za uwakala kinyume cha taratibu. Unakuta mtu kakamilisha taratibu zote za usajili, lakini kinachotokea hawa jamaa wana ku-delay makusudi ili uwakatie kitu kidogo. Kwa sasa hawa jamaa wanataka TZS 100,000 hadi TZS 300,000 kwa laini moja.
Ukijifanya wewe ni mtu wa kufuata taratibu basi jua itakuchukua zaidi ya miezi sita kupata laini. Kila siku utapigwa kalenda kwamba kuna hiki na hiki kinakosekana. Sasa hivi TiGo wanatumia mgogo wa TCRA kwamba ndio wanaobania watu wasipate laini, lakini ukigawa chenji .....fasta ndani ya siku moja au mbili unakuwa umepata line.
Haya nayasema si kwamba nimehadithiwa, ni kwamba yamenikuta mimi mwenyewe.
Wadau naombeni tu mnipe taratibu za nani nimuone pale TiGO na Voda ili niwasilishe barua yangu ya malalamiko pamoja na vithibitisho kwa jinsi rushwa inavyokwamisha juhudi za watu kujikwamua na umaskini.

Usihangaike... peleka takukuru na vielelezo vingine weka hapa..
 
Back
Top Bottom