Wanajipeleka wenyewe, yaani katika kundi la wanafunzi zaidi ya mia mbili huyo mhadhiri anaanzaje kukujua bila kujipeleka?
Halafu wengi wao hawajiamini, ni vilaza, hivi mtu course work inasoma 31 huyo mhadhiri anaanzaje kukutishia kukufelisha?
Kama wanapeana wapeane kiroho safi wasisingizie rushwa.
siyo kweli mkuu, wengi wanatongozwa na wahadhiri kwa kulazimishwa.
wavae vizuri kwa namna gani mkuu kabanga, mbona kuna ambao wanajisitiri vyema na mavazi ya heshima kabisa lakini bado wanasumbuliwa kingono na wahadhiri,..
Habari Wana Jamii Forums,..
Kuna hili suala la rushwa ya ngono ambalo limekithiri vyuoni.
Baadhi ya wahadhiri wa vyuo vikuu wanalazimisha mahusiano ya kimapenzi na wanafunzi wao, inapotokea mwanafunzi kumkatalia mhadhiri basi anakuwa matatani kwani wahadhiri hao huwatamkia waziwazi wanafunzi hao kwamba watawafelisha katika mitihani yao.
Ikumbukwe kuna wanafunzi wanafaulu kwa jitihada zao binafsi na kuna wale wanaofaulu kwa kutoa rushwa ya ngono.
Hebu tutafakari basi, ni nini kifanyike maana suala hili lina changamoto kubwa.
Je mwanafunzi akatae kutoa rushwa ya ngono afeli au atoe rushwa ya ngono apate kufaulishwa!!
Pia nini kifanyike kwa baadhi ya wahadhiri wenye tabia hii chafu ya kutaka rushwa ya ngono ambayo inawaathiri wanafunzi katika taaluma!!
Nawasilisha,...
Hiyo ngono wanaitaka wenyewe,mi siwezi kunywa maji kwa kulazimishwa,sasa mtu.mzima above 18 tena mnasema anafelishwa??? Mimi niliwahi kusumbuliwa na lecturer mmoja,nilimrekodi kila aliponipigia simu,end of the day nilienda takukuru na simu vyote alivyoniambia vilibainika,nilipeleka pia kwenye uongozi wa chuo,mpaka leo huyo lecturer alikoma maana hakua na cha kujitetea evidence zilikua zimekamilika,alijikuta anakabiliwa na kesi mbili,uongozi wa chuo pamoja na takukuru,ifike mahali waschana waseme noooo,wawe na msimamo,
Hiyo ngono wanaitaka wenyewe,mi siwezi kunywa maji kwa kulazimishwa,sasa mtu.mzima above 18 tena mnasema anafelishwa??? Mimi niliwahi kusumbuliwa na lecturer mmoja,nilimrekodi kila aliponipigia simu,end of the day nilienda takukuru na simu vyote alivyoniambia vilibainika,nilipeleka pia kwenye uongozi wa chuo,mpaka leo huyo lecturer alikoma maana hakua na cha kujitetea evidence zilikua zimekamilika,alijikuta anakabiliwa na kesi mbili,uongozi wa chuo pamoja na takukuru,ifike mahali waschana waseme noooo,wawe na msimamo,
We naye ulizidi si ungemnyima kimya kimya tu mwenzako ndo kazi ilikuwa inamweka mjini hiyo afu kupendwa na lecturer si kwamba ni kosa wengine wanapenda kwa dhati, ndoa nyingi tu nauzulia za lecturer na dent wake inawezekana ulikosa bahati wewe
kama kweli ulifanya hivyo na ukamaliza chuo salama kwa ufaulu basi mshukuru MUNGU!!