Rushwa ya ngono ni nini?

Rushwa ya ngono ni nini?

Shadida Salum

Journalist at JamiiForums
Joined
Sep 11, 2020
Posts
69
Reaction score
105
Kwa mujibu wa kifungu cha 25 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa ya mwaka 2007(PCCB Act, 2007); Rushwa ya ngono ni pale ambapo mtu aliye katika mamlaka na katika kutekeleza mamlaka yake akitaka au akiweka upendeleo wa ngono kama kigezo cha kutoa ajira, cheo, haki, au huduma ya upendeleo.

Na akifanya hivyo atakuwa amefanya kosa, na ataadhibiwa kwa faini isiyozidi shilingi milioni tano au kifungo cha miaka isiyozidi mitatu au vyote kwa pamoja.

Iwapo utakutana na mkasa wa namna hiyo toa taarifa katika ofisi ya TAKUKURU iliyo karibu nawe au piga simu namba 133.
 
Dada zetu ndiyo wahanga wa tatizo hili haina budi jamii kubadilika na vitendo vya ngono kuwa na jamii iliyo tayali kukataa mambo haya
 
haya mm nipo Bar hapa au club ya mataptap, kuna kimwana anataka nimpe huduma yeye atanilipa kwa ngono
mpo wapi? au namba zenu?
Mapenzi ni maridhiano, Bibie km anajua tafeli Paper asinisogelee acha aDISCO tu Chuo
 
lakini anayetoa mzigo naye si anakua amependa au analazimisha kufika eneo la tukio ???

kwa nini wasiadhibiwe wote anayetoa na anayepokea kama ilivo kwenye kupeana mpunga ???
 
Back
Top Bottom