Russia Inazisihi Makampuni ya Nishati ya Magharibi kurejea, Lakini Je, Watarudi?

Russia Inazisihi Makampuni ya Nishati ya Magharibi kurejea, Lakini Je, Watarudi?

Imeloa

JF-Expert Member
Joined
Jan 28, 2013
Posts
14,885
Reaction score
18,083
Maafisa wa Kremlin wanahatarisha matarajio ya uwekezaji wa faida kubwa kwa makampuni ya nishati ya Marekani, inaonekana wanataka kumshawishi Rais Trump kwamba mafanikio makubwa ya kiuchumi yanaweza kuja kutoka kwa Moscow katika kumaliza vita vya Ukraine na kufuta vikwazo vya kiuchumi dhidi ya Russia.

Hakuna shaka kuwa Russia ina hazina kubwa ya mafuta na gesi asilia, lakini juhudi za kuyavutia makampuni ya nishati ya Marekani au mataifa mengine ya Magharibi kutekeleza miradi ya Russia huenda yakakumbana na mashaka, si haba kwa sababu ya historia ya hivi majuzi ya kampuni hizo nchini Russia.

Hata hivyo, Kirill Dmitriev, afisa wa fedha wa Kremlin, alionyesha matumaini wiki iliyopita kuhusu matarajio hayo, akiweka uwezekano wa fursa za uwekezaji na makampuni ya Magharibi, ikiwa ni pamoja na wazalishaji wa mafuta.

Makampuni ya nishati yangehitaji kupima upatikanaji wa mafuta na gesi asilia dhidi ya hatari zinazoweza kutokea, ikiwa ni pamoja na uharibifu wa sifa kutokana na kushiriki katika sekta ambayo imeendeleza kifedha serikali inayopigana vita dhidi ya jirani yake.

 
Chini ya Trump yatarudi nadhani. Unajua Trump hata kwa Kim North Korea yeye anapiga mahesabu kuwekeza huko. Unajua Trump siyo war monger ni mtu wa Amani na kutengeneza hela.
 
Kinachofanyika hapa ni swala la maslahi tu kwani inaonekana akina Trump wanaona baada ya makampuni ya kimarekani peke yake kupoteza zaidi ya dola bilioni 300 kwa kipindi cha miaka mitatu tu ambapo yalilazimika kuondoka nchini Russia, sasa wanaona hawako tayari tena kuendelea kupoteza tena pesa nyingi kiasi hicho hivyo ndio maana wanaona Ukraine lazima atolewe kafara ili kutimiza malengo ya "America First Policy."

Kwa wasio fahamu watafikiri ni kwamba Marekani labda chini ya Trump inaigwaya Russia lakini ukweli ni kwamba wenzetu mbele ya maslahi mapana ya nchi hawana adui wa kudumu wala rafiki wa kudumu.

Kumbe huu uamuzi wa Trump wa kumuweka Putin karibu lengo lake ni kuujenga zaidi uchumi wa Marekani na wala sio kwamba Trump hapendi vita lkn Trump ana ubia na matajiri wakubwa wa Marekani na hapa kuna dili za kufa mtu ambapo serikali ya Russia pamoja na kwamba itafaidi ila pia kuna watu wakubwa ndani ya serikali ya Russia wanatarajia kupiga "Commission" kubwa sana kwenye hizi dili.

Russia tayari imesha mkubalia Marekani haki ya kuja kuchimba madini yenye thamani kubwa kwenye maeneo ya Ukraine inayoyashikilia na ndio maana Marekani ameshaiambia Ulaya kwamba yenyewe haihitaji kuweka wanajeshi wake nchini Ukraine kwani Putin tayari ameshaahidi kuwalinda wamarekani watakaokuwa kwenye migodi nchini Ukraine.

Hatua hii ya Trump/Putin ni pigo la mwaka kwa mataifa kama China na Iran kwani hatua hii itapelekea Russia kuondolewa vikwazo vyote vya kiuchumi ilivyowekewa na kurejeshwa kwenye G8.

Ngoja tuendelee kutizama kwani Trump anatamba kwamba hadi anaondoka 2028 uchumi wa Marekani utakuwa ni tishio kubwa duniani zaidi ya ilivyo sasa.
 
Back
Top Bottom