Russia reopens flights to Tanzania

Mkuu wapi source yenye paragraphs mbili hizi:



Tusilishane matango pori mkuu au hizi ni mawazo yako tu mkuu kama ya akina magonjwa matambuka tu?
 
Wale wenye roho za "wajumbe" mbona hawakomenti chochote?
Au wameenda kumpokea nuru wao?
 
TRANSLATE /TAFSIRI.


Kufuatia idadi inayopungua ya maambukizo ya virusi vya corona, Urusi imefungua tena ndege kwenda kwa nchi tatu duniani. Sehemu hizi ni Briteni, Uturuki, na Tanzania.

Urusi ni kati ya nchi za juu za utalii kwa Tanzania. Kufuatia uamuzi huu, Injini ya Utafutaji ya Yandex imepata ongezeko la 65% la kutafuta Tanzania ikiwa ni pamoja na fukwe zake na Safaris.

Je! Hii inamaanisha nini kwa Tanzania?

juhudi zinazochukuliwa na viongozi wetu kupambana na janga hili, sasa zimeonekana kwa wale ambao wana macho, na na wale wanaojua ukweli ni nini. Urusi inakuwa balozi wa Tanzania kwa ulimwengu wote kadiri COVID-19 inavyohusika. sasa tutapata ukuaji wa haraka wa Sekta ya Utalii katika siku chache zijazo.
 
Ubashiri wao ushaingia mrama. Eti huyo Mwanadiplomasia wao mbobevu alisema tutatengwa. Hakuna atakayetaka kuja Tanzania
Hivi Huyo mende nao mnawezaje kumuweka ktk idadi ya wanadiplomasia!? Jamani hebu acheni utani, kuingiza wahuni wasiojitambua kwenye fani za watu! Labda kwenye ulanguzi na udalali wa maliasili za Tanzania, hapo unaweza kumuweka na aka'fit in' vizuri!
 
Mkuu wapi source yenye paragraphs mbili hizi:

View attachment 1518383

Tusilishane matango pori mkuu au hizi ni mawazo yako tu mkuu kama ya akina magonjwa matambuka tu?

Kama huwezi hata kusearch kidogo tu huo ni udhaifu wako. Ungeweza ona references nyingi sana hasa kwa Paragraph ya kwanza. Ukiangalia Paragraph ya mwisho haihitaji upewe source, source yake ni aliyeleta uzi.
 
Kama huwezi hata kusearch kidogo tu huo ni udhaifu wako. Ungeweza ona references nyingi sana hasa kwa Paragraph ya kwanza. Ukiangalia Paragraph ya mwisho haihitaji upewe source, source yake ni aliyeleta uzi.


Haha ha ha. Usitake ncheke miye wee!

Ama kweli staajabu ya Mussa.

Source ya hizi paragraphs 2 ni aliyeleta uzi?!



Mtaweweseka sana mwaka huu.

Waliona mbali sana waliosema "penye ukweli uongo hujitenga."

Don Nalimison - popote ulipo, muda wa kuanza kuchua misuli ni huu mkuu. Pana huyu jamaa hapa, eti source ni yeye mwenyewe!

Yaonyesha ana mpango ovu wa kukupokonya maujiko yako yaliyotukuka humu jamvini.
 
mbona unajikanyaga kanyaga mzee hueleweki unasimamia nini...
 
mbona unajikanyaga kanyaga mzee hueleweki unasimamia nini...
Kwa kukusaidia mzee nasimamia ukweli na si ushabiki au chuki, fuatilia hoja yangu chini
Ninasema Urusi(Russia) wameifungulia mipaka Tanzania siyo kwa sababu tumeimaliza COVID-19 bali wamezingatia vigezo vyao vya kufungulia mipaka watu toka nchi yeyote, ambacho kigezo kikuu ni NIPE NIKUPE (Reciprocity, reciprocating the action, give something mutually or in return), wakimaanisha wataruhusu kule waliko ruhusiwa tu.

Lakini kwa vile nilipenda kuweka mizani sawa (balance) bila kuweka ushabiki au upendeleo, tutoe sifa panapostahili ndipo( give credit when it's due) nikasema tumpongeze Mh. Magufuli kwa kuweka msimamo wa kufungua mipaka kwa raia wa nchi yeyote ili mradi wafuate sheria.
Hapo nilimaanisha alistahili pongezi kwa jambo hilo na siyo kwa kuimaliza COVID-19 nchini kwa maana kufungua mipaka kwa nchi yeyote amesababisha Tanzania kufunguliwa mipaka na nchi kubwa kama Russia ambako tunapokea watalii wengi tu toka kwao, pia ameokoa watu wengi sana wasiingie kwenye matatizo makubwa zaidi ya kiuchumi.

NB: Unaposoma makala au mabandiko(posts) yangu weka pembeni akili ya uchama, siasa, ukada, ukabila, and the like, hapo utanielewa kirahisi sana.
 
Taarifa hii hawataipenda wahuni Akina Membe, Zito, TL, Mbowe nk! Pole yenu, makiwani kwenu!
Wewe unawaita wahuni na pia hawatafurahia hivi ni kweli ulichoandika? Watu wa arusha, kilimanjaro, dar, zanzibar wanajua shida ya ajira baada ya kupotea watalii. HATA KAMA NI WAUPINZANI HAWAWEZI KUTOKUFURAHI UTALII KURUDI.WATAKUSHANGAA ULILOANDIKA. SIKU INGINE FIKIRIA CHA KUANDIKA.
 

Umeeleweka mkuu. Yote heri.
 
Twende kazi, tuanze kutest cruise mkonga tayari kwa safari za pori tena. Kaeibuni warusi, tufikishieni shukurani zetu mwamba Putin
 
 

Attachments

  • Screenshot_20200728-135112_Chrome Beta.jpg
    146.5 KB · Views: 1
Siku nyingine jitahidi kutulia na uondoe mihemko, Soma neno kwa neno Kisha utafakaki kabla ya kufwatuka na majibu yasyo na mantiki! Wahuni hawana ukanda Wala kabila! Angalia vizuri msg yangu!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…