Ruto aahidi wanafunzi wa Nairobi mashine inayoweza kutengeneza chapati milioni 1 kwa siku

Wild Flower

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2023
Posts
378
Reaction score
766
Sijui ni vigezo gani tunatumia kuchagua viongozi wetu Afrika. Kwa nchi kama Kenya mabayo imetajwa kuwa mojawapo ya nchi zenye ukame mkubwa barani Africa jambo linalopelekea uhaba wa maji na wana matatizo makubwa kama mfumuko wa bei za vitu na kodi kubwa kwa Wananchi wake imagine Rais anasema yuko tayari kutoa msaada wa kununua mashine ya kutengeneza chapati.

====================================

Rais William Ruto ametoa ahadi kwa Gavana wa Nairobi, Johnson Sakaja kununua mashine yenye uwezo wa kutengeneza chapati milioni moja kwa siku ili kuimarisha mpango wa ulaji 'Dish Na County' katika shule zilizopo jijini Nairobi

Amesema hayo Machi 11, 2025 katika Shule ya Sekondari ya St. Theresa iliyopo Nairobi wakati wa ziara yake maeneo ya Mathare na Ruaraka ambapo wanafunzi wa shule hiyo walimuomba Gavana Johnson kuongeza chapati kwenye menyu ya mpango huo wa ulaji

Aidha, wazo hilo limepingwa na baadhi ya Wananchi wakidai kuwa kuna matatizo makubwa kama vile uboreshwaji wa miundombinu pamoja na upatikanaji wa maji amabyo yanatakiwa kushughulikiwa na kupewa kipaumbele kwanza

=========================For English Audience========================​
President William Ruto has promised to buy Nairobi Governor Johnson Sakaja a chapati-making machine that can produce a million units daily to boost the city’s ‘Dishi Na County’ school feeding program.

Ruto accompanied Sakaja on Tuesday to St Teresa Girls Secondary School in Nairobi’s Mathare area, where students asked the governor to add chapati to the program’s menu.

Chapati-making machines, also called roti makers, are billed as a simple means of making the dish in industrial quantities by feeding them with the ingredients. They cost upwards of Ksh.150,000 and vary by output, with some producing up to 2,000 chapatis per hour.

SOURCE: CITIZEN DIGITAL
 
Chapati milioni moja hapo kama supu inabidi wapate hata pipa moja na nyama nyingi sana,kama na maharage hapo inabidi wapate siyo chini ya gunia tatu.Wakenya nawakubali hapo tu kwenye upande wa kula.
 
Bora hata huo uongo wa kisayansi, huku tshirt na buku tano imetosha
 
Badala ya kusisitiza kuwapa wanafunzi chakula cha asili (viazi/magimbi) yeye anaendekeza kuwalisha ngano.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…