Kenya 2022 Ruto kugombea urais wa Kenya kwa tiketi ya UDA

Kenya 2022 Ruto kugombea urais wa Kenya kwa tiketi ya UDA

Kenya 2022 General Election

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
1647411341672.png

Wajumbe wa chama cha UDA wamemuidhinisha Naibu Rais William Ruto kuwania kiti cha urais kwenye uchaguzi mkuu nchini Kenya, utakaofanyika tarehe tisa mwezi Agosti mwaka huu.

Ruto sasa atamenyana na kiongozi wa Muungano wa Azimio la Umoja Raila Odinga kwenye uchaguzi mkuu.

Ruto alipokewa na mkewe Rachel pamoja na maafisa wakuu wa chama cha UDA mwendo wa saa tano kasorobo katika uwanja wa kimataifa wa Kasarani, uliokuwa na yamkini wajumbe 5000 waliokuwa na mavazi ya manjano na kijani.

Baadaye aliidhinishwa na wajumbe 4,350 wa UDA bila ya kupingwa kuwania kiti cha urais kwenye uchaguzi mkuu ujao, kwenye hafla iliyofanyika faraghani.

Kiunzi cha pili cha Ruto sasa baada ya kukabidhiwa jukumu la kuipeperusha bendera ya chama hicho, ni kumchagua makamu wake ikizingatiwa kuwa, jamii za mlima Kenya na Magharibi ya Kenya zinakimezea mate kiti hicho. Rigathe Gachagua na Musalia Mudavadi wa ANC wanapigiwa upatu wa kiti hicho.
 
Azimio wamenipanga kuwin kumchukua Kalonzo ilikua tiketi yao muhimu sana, Kwa Ruto kumeanza kupwaya lakini historia inaweza kujirudia rais aliyepo madarakani kwa Kenya akichagua upande ule upande hua haushindi
 

Wajumbe wa chama cha UDA wamemuidhinisha Naibu Rais William Ruto kuwania kiti cha urais kwenye uchaguzi mkuu nchini Kenya, utakaofanyika tarehe tisa mwezi Agosti mwaka huu.

Ruto sasa atamenyana na kiongozi wa Muungano wa Azimio la Umoja Raila Odinga kwenye uchaguzi mkuu.

Ruto alipokewa na mkewe Rachel pamoja na maafisa wakuu wa chama cha UDA mwendo wa saa tano kasorobo katika uwanja wa kimataifa wa Kasarani, uliokuwa na yamkini wajumbe 5000 waliokuwa na mavazi ya manjano na kijani.

Baadaye aliidhinishwa na wajumbe 4,350 wa UDA bila ya kupingwa kuwania kiti cha urais kwenye uchaguzi mkuu ujao, kwenye hafla iliyofanyika faraghani.

Kiunzi cha pili cha Ruto sasa baada ya kukabidhiwa jukumu la kuipeperusha bendera ya chama hicho, ni kumchagua makamu wake ikizingatiwa kuwa, jamii za mlima Kenya na Magharibi ya Kenya zinakimezea mate kiti hicho. Rigathe Gachagua na Musalia Mudavadi wa ANC wanapigiwa upatu wa kiti hicho.
Bila shaka Ruto ni kiongozi bora, na tuna tumai ataibuka mshindi kwenye Uchaguzi huu. Kizungu mkuti ni jinsi ya kuchagua mgombea mwenza. Nilipata fursa ya kuhudhuria mkutano wake Amboseli akiuza sera zake na nilipendezwa naye
 
Back
Top Bottom