Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Mkoa wa Ruvuma. Umepewa jina kutokana na mto Ruvuma ambao ni mpaka wake wa kusini na Msumbiji. Umepakana na Ziwa Nyasa na Mkoa wa Morogoro upande wa magharibi, mikoa ya Iringa na Lindi upande wa kaskazini na Mkoa wa Mtwara upande wa mashariki.
Makao makuu ya mkoa yako Songea mjini. Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 yanaonesha kuwa idadi ya watu
katika Mkoa wa Ruvuma ni 1,848,794; wanaume 902,298 na wanawake 946,496.
Mkoa huu una Halmashauri nane (8) katika mchanguo wa Mamlaka za Miji na Mamlaka za Wilaya
Mkoa wa Ruvuma una majimbo ya uchaguzi tisa (9) ambapo Jimbo la Songea Mjini linaongoza kwa kuwa na watu wengi (286,285) likifuatiwa na Jimbo la Mbinga Vijijini (watu 285,582). Jimbo lenye idadi ndogo ya watu ni Madaba ambalo lina watu 65,215.
Majimbo ya Uchaguzi
Jimbo la Songea Mjini (Watu 286,285 ambapo wanaume ni 134,920 na wanawake 151,365)
Jimbo la Madaba (Watu 65,215, ambapo Wanaume ni 33,085 na Wanawake ni 32,130)
Jimbo la Mbinga Vijijini (Watu 285,582, ambapo Wanaume ni 141,271 na Wanawake ni 144,311)
Jimbo la Mbinga Mjini (Watu 158,896, ambapo Wanaume ni 75,882 na Wanawake ni 83,014)
Jimbo la Nyasa (Watu 191,193 , ambapo Wanaume ni 93,494 na Wanawake ni 97,699)
Jimbo la Namtumbo (Watu 271,368, ambapo Wanaume ni 132,035 na Wanawake ni 139,333)
Jimbo la Tunduru Kaskazini (Watu 225,773, ambapo Wanaume ni 110,614 na Wanawake ni 115,159)
Jimbo la Tunduru Kusini (Watu 186,281, ambapo Wanaume ni 91,054 na Wanawake ni 95,227)
Soma Pia:
- Special Thread: Orodha ya Nyuzi za Mikoa yote Tanzania Bara inayoshiriki katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024
- Orodha ya CV za Wabunge kwa mwaka 2020 - 2025 kutoka kila mkoa Tanzania
Kama ilivyo kwa mikoa mingine, uchaguzi wa Ruvuma unadhihirisha changamoto za uwakilishi wa kisiasa na ushindani wa kidemokrasia. Katika majimbo yote 9 yalichukuliwa na Chama cha Mapinduzi (CCM).
katika jimbo la Tunduru Kusini ambako Daimu Mpakate (CCM) alipata kura 26,982 dhidi ya Abdalah Mtutula (ACT-Wazalendo) aliyepata kura 23,968.
Katika jimbo la Madaba, Joseph Kizito Mhagama alipita bila kupingwa. Katika baadhi ya majimbo kama Peramiho na Nyasa, kulikuwa na tofauti kubwa ya kura kati ya wagombea wa CCM na wa upinzani.
Peramiho -
Jenista Mhagama (CCM) - Kura 27,479
Silvester Mapunda (CHADEMA) - Kura 3,440
Nyasa:
Eng. Stella Manyanya (CCM) - Kura 34,937
Casberth Kiwango(CHADEMA) - Kura 4,055.
Katika majimbo kama Songea Mjini na Tunduru Kusini, upinzani ulionekana kufanya vizuri zaidi ikilinganishwa na majimbo mengine, ingawa hawakufanikiwa kushinda.
Dkt. Damas Ndumbaro(CCM) - Kura 39,783
Aden Mayala(CHADEMA) - Kura 15,146
Daimu Mpakate (CCM) - Kura 26,982
Abdalah Mtutula (ACT Wazalendo) - Kura 23,968.
JANUARI
- Pre GE2025 Wananchi wa Vijiji viwili Jimbo la Namtumbo warudisha t-shirt na fedha za Mbunge wao Vita Kawawa!
- Pre GE2025 Baada ya Wananchi kugomea t-shirt na fedha za Kawawa, ajitokeza na kusema hizo ni fitna za Kisiasa na kuwa wanaichafua CCM
- Pre GE2025 CCM Ruvuma waandamana kuunga mkono uteuzi wa Dkt. Samia, Dkt. Nchimbi na Dkt. Mwinyi
- Pre GE2025 Ruvuma: Wananchi Watakiwa Kupuuza Maneno ya Wanasiasa Wanaodai Kutumwa na Viongozi wa CCM" kuja kugombea
- Pre GE2025 RC Ruvuma: Dkt. Ndumbaro hana deni jimbo la Songea mjini utekelezaji wa miradi ya maendeleo
- Pre GE2025 CCM Ruvuma yahimiza demokrasia kwenye nafasi za wagombea udiwani na ubunge
- Pre GE2025 Mbunge wa Madaba Dkt.Joseph Kizito Mhagama, atembelea kata ya Mkongotema kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo