Ruvuma: Mtatiro amwakilisha Kanali Labani Elias Thomas, Ibada Takatifu ya Ijumaa Kuu

Ruvuma: Mtatiro amwakilisha Kanali Labani Elias Thomas, Ibada Takatifu ya Ijumaa Kuu

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
IBADA YA KITAIFA YA IJUMAA KUU - MMOMONYOKO WA MAADILI

Jana katika Ibada Kuu ya Kitaifa ya Ijumaa Kuu iliyoadhimishwa hapa KIUMA, kata ya Matemanga - Tunduru, nilipata wasaa wa kutoa salamu za Serikali ya Mkoa wa Ruvuma, nikifanya hivyo kumwakilisha Mhe. RC wa Ruvuma, Kanali Labani Elias Thomas, ambaye alialikwa kuwa Mgeni Rasmi lakini akawa na majukumu mengine ya kitaifa.

Tunaishukuru sana Jumuiya ya Kikristo Tanzania (Christian Council of Tanzania - CCT) kwa kuamua kuleta Ibada hii ya kitaifa Tunduru. Maaskofu wote wa CCT Mkoa wa Ruvuma asanteni sana.

Tunamshukuru Askofu Mbawala Noel Mbawala wa KIUMA na Katibu Mkuu wa KIUMA ndugu Daniel Malukuta kwa ukarimu wao mkuu.

Tunawashukuru sana TBC ambao waliamua kufunga safari kutoka Dar Es Salam hadi Tunduru na kuirusha IBADA hii Mubashara kwenye @TBC1 na TBC FM.

Tunawashukuru sana Redio yetu pendwa Mercy FM inayomilikiwa na Kanisa la Biblia Tunduru kwa kurusha ibada yote Mubashara.

Asantenj nyote na Mungu awabariki.

Karibuni sana Tunduru.

JSM
 
Ila huyu jamaa alicheza karata yake vizuri sana. Anakula maisha tu sasa hivi
 
Back
Top Bottom