Kama CCM haiwezi kubuni mfumo bora wa kusimamia mchakato wa Katiba Mpya na badala yake kuturudishia kitu kile kile ambacho tumekikataa miezi michache iliyopita ni jukumu letu kukataa siyo tu kuunga mkono mchakato huu bali pia kushiriki endapo utapitishwa - na uwezekano wa kupita ni mkubwa kwani wao ni wengi, rais wao na vyombo vyote vyao.
Ninachoweza kusema ni kwamba kama CCM na serikali yake watalazimisha kutulisha katiba mpya kama kwa nguvu. Ni wajibu wetu kukataa kushiriki kwenye mijadala yao na kwa hakika kwenye kura ya maoni watakayoitisha. Kama tumeweza kusubiri miaka 20 nina uhakika tunaweza kusubiri miaka mingine mitano kwani tunajua ni kina nani kweli walipigania Katiba Mpya. Wanaotaka Katiba Mpya ya CCM waendelee na mchakato wao, wanaotaka Katiba Mpya kwa ajili ya Watanzania wote wasubiri wakati wao. Kwani miaka minne iliyobakia si mingi.
Facebook: "Mimi Mwanakijiji"
MIMI PIA nafikiri sawa naweSasa, kwa mtu yeyote ambaye amewahi kupita kwenye majengo ya shule anaweza kukiona kitu kimoja kilicho wazi sana - mchakato wa Katiba Mpya unamhitaji Rais ili kufanikiwa na kuwa halali. Lakini siyo kumhitaji Rais tu bali kumfanya Rais kuwa ndiye kiini cha mchakato mzima. Naweza kusema kwa ujasiri wa ukweli mchakato unaopendekezwa ukikubaliwa utamfanya Rais kuwa ndiye mwanzo na mwisho wa mchakato wa kuandika Katiba mpya na siyo wananchi.
Mchakato huu unamfanya rais awe Kingkwete yaani Mfalme Kikwete.
Karibu ndugu yanguSasa, nakubaliana na wewe japo kwa kuchelewa, waswahili wanasema, ' kawia ufike'
""""Ninachoweza kusema ni kwamba kama CCM na serikali yake watalazimisha kutulisha katiba mpya kama kwa nguvu. Ni wajibu wetu kukataa kushiriki kwenye mijadala yao na kwa hakika kwenye kura ya maoni watakayoitisha. Kama tumeweza kusubiri miaka 20 nina uhakika tunaweza kusubiri miaka mingine mitano kwani tunajua ni kina nani kweli walipigania Katiba Mpya. Wanaotaka Katiba Mpya ya CCM waendelee na mchakato wao, wanaotaka Katiba Mpya kwa ajili ya Watanzania wote wasubiri wakati wao. Kwani miaka minne iliyobakia si mingi""""".
subira yavuta heri. kwa ninyi mlio utumwani na mnaoijua tanzania kupitia magazeti(biased tabloids) na blogs!! sio ajabu mkisema hivyo kwani mnachokiona kila cku ni habari za ARUSHA,MWANZA,MBEYA na miji mingine na mwisho mnadhani hiyo ndio hali halisi hadi vijijini. kaka Tanzania ni kubwa kupita kiasi na kama hujapata nafasi ya kuitembea huna haki ya kuongea kuhusu nini chaguo la watu. karibu tz uje utembee na upate hali halisi ya nchi ilivyo kisiasa.
hizo propaganda zenu ili mje mseme watu wamechakachua hazina maana.nashukuru analysis yako juu ya mapungufu yaliyomo katika uwasilishaji wa hoja ya katiba mpya na ninakuunga mkono100% lakini tukisema tususie eti kwa vile 2015 chama chako kitashinda!!!! tutakuwa tunacheza na muda na mustakabali wetu.kama ni kukomaa tunatakiwa tukomae sasa na kama kueleweka kinatakiwa kieleweke sasa,, sasa hivi..........
2015 tuingie tukiwa na kitu kinachotuongoza ili hata porojo za kura kuchakachuliwa zisiwepo.
ama umeshasoma alama kuwa chama chako hakina nafasi 2015 na uwepo wa katiba mpya kutainyima nafasi chama chako kupiga kelele za kuibiwa???????
msicheze na akili za waTZ kwa kujenga mazingira ya future conflicts
ndugu kumbe unaongozwa na chuki... humu tunatanguliza taifa kwanza.. anaefikiria tofauti na wewe huna haja ya kumchukia, jaribu kumshawishi kwa hoja. tupo katika mti mmoja ila matawi tofauti. tujaribu kuutunza mti wetu kwani siku shina la huu mti likianguka hakuna tawi litakalosalimika. BY THAT TIME!!! MWANAKIJIJI NA mamluki wengine hawatakuwepoHivi ww unaona kwa kuandika haya ndo una uchungu na watanzania? Ww ni mpuuzi na ccm yako nyie ndo mnataka kucheza na akili za watanzania tena siwapendi siwapendi