Sababu kwanini hatuokoti hela kama zamani

sangujoseph

Senior Member
Joined
Nov 30, 2015
Posts
164
Reaction score
183
By Sangu Joseph

Nimejaribu kufanya kautafiti uchwara juu ya kuokota hela na nikauliza watu mara ya mwisho umeokota hela lini na Kwanini sasa ni ngumu kuokota hela.

Kila mtu alijibu lake Ila baadhi ya majibu ambayo watu waliyatuma nimeona yanamake sense Kidogo nikaona niyamwage hadharani.

Mtu wa kwanza aliniambia si kweli Kwamba watu hawaokoti hela watu wanaokota hasa watoto, wewe (Sangu ) itakua una Mawazo ndiyo maana huokoti hela. Sasa sijui wenye watoto kipindi hichi cha Corona watoto ndiyo wanalisha familia.[emoji3]

Wapili aliniambia watu hawaokoti hela kwa sababu ya ujio wa mfumo kieletroniki, yaani Money Mobile Transaction ambayo wenye hela wengi wanaitumia kwa usalama wao. (Nikafikiria nikahisi kama ni kweli) sijui kwako.

Mwingine akaniambia broh kiukweli siku hizi no kuokota hela sababu kubwa Maisha yamekua magumu, ( Nikamwambia bro wimbo wa Maisha magumu nausikia tangu zamani wakati naokota hela Hadi sasa lakini now no kuokota hela, akasema ndiyo ukweli life gumu)

Mwingine akanieleza broh kuokota hela kuna umri kuna wakati ukifika hela zinakukimbia [emoji3][emoji3] zikikuona tena zinakuchamba Braza Nenda kafanye kazi hakuna cha bure (Hapa nilicheka Sana)

Naendelea kufanya tafiti kwanini kwa sasa ni ngumu kusikia mtu kaokota hela kama miaka ya zamani.

Insta : FB : Twit : Sangu Joseph

#KijanaMzalendo #IloveTz

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Inategemea na Bahati ya mtu. Mara ya mwisho nilibahatika kuokota $200. Ilikua December last year.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…