Uchaguzi 2020 Sababu tatu pekee zitanifanya niipigie kura CCM na wagombea wake

Uchaguzi 2020 Sababu tatu pekee zitanifanya niipigie kura CCM na wagombea wake

MKEHA

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2013
Posts
716
Reaction score
1,143
Pamoja na mengi sana yanayoendelea kwenye kampeni lakini nina sababu tatu tu zitakazonifanya niwapigie kura wagombea wote wa CCM.
Kwanza ni kitendo cha kuufikisha umeme kijijini kwetu kwa mara ya kwanza.

Miaka yote nilikuwa sina wazo la siku moja umeme kuwaka kijijini kwetu kwani hata makao makuu ya wilaya kipindi hicho Kasulu hapakuwa na umeme.

Hata makao makuu ya mkoa Kigoma mjini walikuwa wakipata umeme mara mbili tu kwa wiki. Hivyo umeme kufika kijijini kwetu imesababisha niwapigie kura CCM japo ni wajibu wao kuleta umeme.

Pili, ni kuleta na kusambaza maji ya bomba kijijini kwetu. Tukekuwa tukochota maji mitoni toka udogo wetu japo tumezungukwa na mito mingi lakini ilikuwa ni adha kubwa sana. Leo mama amachotea maji uani kwake lazima niipigie kura CCM na wagombea wake japo ilikuwa wajibu wao kutuletea maji.

La tatu na la mwisho, ni kutuletea huduma za mitandao ya simu. Zamani kuna mlima Kabhuye ukifika tu pale unakaribishwa na meseji ya Vodacom wishes you good journey and stay in Burundi wakati bado upo ndani ya Tanzania.

Kila muda unaongea na wazazi hata kama upo Horohoro Tanga. Ni kwa sababu hizo nitampigia kura Philip Isdory Mpango kuwa mbunge wangu na John Pombe Magufuli kuwa rais wangu.
 
Wewe akili huna.

Mtu aliekunyima chakula miaka zaidi ya 20 kwa maksudi kabisa, akiamua kukupa leo unampongeza?

Umeme kijijini kwenu ulitakiwa uwe umefika miaka 30 iliyopita, lakini kwa udhaifu wa ccm wamekuletea leo unawapongeza?

Kijana wa miaka 20 ukikuta anachezea kinyesi na kufanya mambo kama ya mtoto wa miaka 3 utampongeza kua amekua?
 
Mtaji wa maccm ni kundi la watu wasioelimika, wasioweza kupembua mambo
 
Wewe akili huna.

Mtu aliekunyima chakula miaka zaidi ya 20 kwa maksudi kabisa, akiamua kukupa leo unampongeza?

Umeme kijijini kwenu ulitakiwa uwe umefika miaka 30 iliyopita, lakini kwa udhaifu wa ccm wamekuletea leo unawapongeza?

Kijana wa miaka 20 ukikuta anachezea kinyesi na kufanya mambo kama ya mtoto wa miaka 3 utampongeza kua amekua?
Kila mtu ana uhuru wa kuchagua chochote, uhuru wake yeye kuichagua ccm haimfanyi kutokuwa na akili! The same applying to u, uhuru wako wa kuipinga/kutokuikubali ccm haikufanyi uwe na akili nyingi!

Heshimu mawazo ya mwingine, ni haki yake na utashi wake na sababu zake ambazo ameziona zinafaa kuichagua ccm
 
Serikali dhalimu na Dikteta huwa wanafanya nchi na wao kama serikali na kiongozi kuwa kitu kimoja Eti ukimkosoa dikteta umekosoa nchi Ukipinga sera za serikali, we msaliti wa nchi Kiuhalisia unaweza kupinga serikali, kiongozi na kwa kufanya hivyo ukawa mzalendo
 
CCM wanawaona wakimbizi..kijijini kwetu umeme toka 70s
 
Kwani bila sababu hizo tatu ungepiga tofauti? Acha propaganda, haIsaidii safari hii. CCM maji shingoni. Na hamchomoki. Labda mkubali nchi hii iwe vipande vipande.

Majizi nyie.
 
Back
Top Bottom