Jamaa aliondoka kinyonge sana ila alikuwa poaNakubaliana na wewe mkuu but Kocha mkuu na kocha wa viungo Kuna kazi ya ziada!,sijajua ni kwanini Gamondi alimkataa yule kocha wa Viungo aliyemkuta,jamaa aliwajenga wachezaji Kwa Ubora wa Hali ya Juu!
Huyu wa Sasa ni kama hakuna anachokifanya,si mbali utasikia Yanga wameachana nae
Boka yupo vizuri , kuna kitu tu anapaswa kuongezewa .Lomalisa alikuwa sio mkabaji mzuri, akikaba lazima atengeneze faulu. Kimbinu Boka ni mzuri zaidiNje ya hapo pia alikuwa mstaraabu sana ila kwenye uchezaji jamaa alikuwa anajua sana ku scan mchezo
Boka sijamuelewa kabisa
Mpaka saivi mimi sijajua wanaomsifia Lomalisa wanamsifia katika nyanja ipi iliyomzidi Boka. Kwenye kukaba Lomalisa vs Boka naona Boka yuko vizuri.Boka yupo vizuri , kuna kitu tu anapaswa kuongezewa .Lomalisa alikuwa sio mkabaji mzuri, akikaba lazima atengeneze faulu. Kimbinu Boka ni mzuri zaidi
Ngoja niendelee kumuangalia ila binafsi receiving zake bado sijazielewaBoka yupo vizuri , kuna kitu tu anapaswa kuongezewa .Lomalisa alikuwa sio mkabaji mzuri, akikaba lazima atengeneze faulu. Kimbinu Boka ni mzuri zaidi
Mipira mingi ya boka akipanda huwa haina faida! Either inaishia kuchukuliwa,au anapiga tu ilimradi kama kibabage! Lomalisa ilikuwa anatoa pasi au kross za uhakika vinginevyo anarudisha nyuma ila mpira haupotei!Mpaka saivi mimi sijajua wanaomsifia Lomalisa wanamsifia katika nyanja ipi iliyomzidi Boka. Kwenye kukaba Lomalisa vs Boka naona Boka yuko vizuri.
Kushambulia Lomalisa vs Boka naona wanafanana tu isipokuwa Boka ana spidi zaidi.
Hakuna Mwanayanga mwenye tabia za kishabiki za aina Yako....!Wewe ni Kolo,hakuna mwanayanga asiyefahamu kwasasa timu inachopitia!
Hua huangalii mpira wewe.Nguvu zipi alizonazo?,akienda mbele kurudi kukaba ni mtihani,mwisho wa siku anampa taabu Baca
Timu inatengeneza nafasi za kutosha tu na haijaruhusu goli mpaka sasa. Tatizo mnataka timu ishinde goli 4,5,6 we unadhani wapinzani wamekata tu wanatizama. Huko uingereza Man City tu na ubabe wake anateseka.Nsikuchoshe na Usinchoshe, Tusichoshane!
Kabla ya yote nikubali ya kwamba Mimi ni shabiki na mkereketwa wa timu ya Yanga!,hivyo nitakachokiandika hapa kinaihusu timu ya Yanga!
Tangu ligi ya NBC imeanza kiukweli binafsi hakuna mechi hata moja kutoka Kwa timu yangu ya Yanga iliyonishawishi na kunivutia!
Timu kwasasa inashinda Kwa mbinde na makosa ya Marefa (Ukweli lazima usemwe),sijaona kabisa timu ikitengeneza nafasi na Kuwa katiri kwenye lango la mpinzani,hii ni tofauti kabisa na msimu wa mwaka Jana!,Sasa bado sijaelewa ni mbinu na kiwango Cha Gamondi kimefika mwisho au tatizo ni wachezaji?
Mbona wachezaji takribani wote wa msimu wa mwaka Jana ndiyo hawahawa?,au shida ni kuchoka?
Wachezaji walioshuka kiwango Kwa Hali ya Juu!
1.Aziz Ki
Huyu jamaa Bado sijajua ni kitu gani kinamsumbua,yaani akiwa nje kabla hajaingia unaona namna anavyowaelekeza wenzie wakiwa dimbani utadhani yeye ndiye kocha!,ila akiingia uwanjani anacheza ovyo mnoo!
2.Khalid Aucho
Huyu yeye kiwango kimeshuka zaidi na Wala halihitaji binocular kuona hilo,kwasasa Babu Kaju ni Bora kuliko Aucho ila sema ndo vile Kwa Gamondi ni kama kalogewa!,jamaa anacheza vibaya na kiwango hakiridhishi hata kidogo,sijajua ni kutumika sana au umri umemtupa mikono!
3.Chadrak Boka
Bado sijajua sababu za kutokumuongezea mkataba Joyce Lomalisa zilikuwa ni zipi,Huyu Boka hamzidi kitu chochote Kibabage,kwasababu kama ni kukimbia wote wanakimbia na hatimaye huwa hawana mbinu mbadala,Joyce Lomalisa alikuwa ni habari nyingine linapokuja suala la utulivu na upigaji wa Krosi!,Kama Hersi aliamua kutomuongezea mkataba Lomalisa na kumletea Boka Kwa nia ya kuongezea hatari Kwa wapinzani,kiukweli hapa tumeingia chakike!,Boka Hana Ubora kama tulivyoaminishwa!
Naelewa timu za ligi kuu msimu huu ziko vizuri,hilo halina Ubishi!
Tatizo la timu yangu ya Yanga ni Kucheza vibaya kila mechi na kushinda Kuwa katiri kwenye lango la mpinzani tofauti na msimu uliopita!
Mechi ya Jkt wiki iliyopita walikuwa wanacheza mpira mzuri pamoja na kipa wao kupewa kadi nyekundu!,Hivi Yanga ya Msimu uliopita ingekuta Jkt kapewa redi kadi vile tena kipindi Cha kwanza,Nina hakika Jkt angekufa si chini ya goli 7!
Tatizo kwasasa pale Yanga ni Nini?, na Je tiba yake ni ipi?
Kila siku timu badala ya kuongeza kiwango ndiyo inashuka kiwango!
Kayoko Na WenzakEIla timu kucheza mechi 7 bila kufungwa inatokana na nini mchambuzi?
Una jicho la mpiraUkweli usemwe Lomalisa ni Bora kuliko Boka kuanzia Skills, mikimbio (sio mbio), kutengeneza nafasi hatari, kumwaga maji (krosi), kuzuia, na pia kupanda kwa wakati sahihi...
Lomalisa labda tu alikua na pancha nyingi by the way namkumbuka sana mwamba huyu Boka yeye ni kupiga tu mikrosi isiyo na kichwa Wala miguu... Anafosi aende mwisho wa uwanja ndo apige krosi wakati Lomalisa alikua anapiga krosi hata mbele kidogo ya msitari wa kati ya uwanja na inaleta balaa kwa wapinzani (rejea game ya usma vs Yanga fainali ya confederation...)
Basi tu mabadiliko yalikua n lazima lakini Lomalisa alikua FUNDI...
Kwa hiyo kuna mechi watu hawakamiani yamekuwA mazoezi?hivi wapinzani wa Yanga wao wanacheza mechi kila baada ya mwezi?kwAni Azam complex yanga ndo anashinda magoli mengi kila mechi?ukiondoa mechi ya pamba ipi ameshinda tatu na kuendelea?Kwa sasa washukuliwe Marefa bila hivyo mtaani kungekuwA na hadithi kwAmba yanga Ashamimimwa mechi kadhaa.Labda nikujibu kitaalamu hoja yako kwa kufata sayansi ya Mpira na sio mihemko ya shabiki asiyejitambua na asiyeuelewa Mpira,
1) Yanga katumia energy kubwa sana kwa misimu 3 mfululizo uku akicheza mechi nyingi zaidi kuliko timu yoyote hapa Tanzania ndani na nje ya nchi ivyo kitaalamu lazima wawe na fatique na lazima uwezo wao upungue kwa kiasi Fulani ili kutengeneza energy mpya waliyopoteza ndio maana wanafanya game management kwenye Kila mechi( kuna mda watakushambulia na Kuna muda watakuachia ucheze wewe Mpira kwenye eneo lako awatumii nguvu kubwa)
2) Hoja ya pili inayofanya yanga aonekane kashuka ni kukamiwa na timu zote anazokutana nazo, ni jambo la kawaida kwa bingwa mara 3 mfululizo kukamiwa kwasababu Kila timu inakuwa inataka kumzuia asichukue Tena ubingwa ama zinakuwa zinataka kumfunga bingwa ili kuvunja mwiko wa kutokufungwa, matokeo yake yanaifanya yanga kupata wakati mgumu kufunga magoli mengi maana timu nyingi kwa sasa zinakaa nyuma ya Mpira azitaki kufunguka wanapocheza na yanga wanaona ni Bora wafungwe na timu nyingine magoli mengi lakini sio yanga!
3) Hoja ya 3 ni ratiba ya mechi na mechi kwa sasa sio rafiki, timu inacheza mechi Kila baada ya siku 3 na muda mwingine inatakiwa usafiri kwenda mikoani, ni changamoto nyingine utaweza kufanya mazoezi saa ngapi na kurudisha mwili kwenye utayali saa ngapi!
4) hoja ya 4 ni aina ya viwanja, yanga anayecheza uwanja wa Azam complex au taifa au kmc complex ni tofauti na yanga atakayecheza sokoine mbeya, Sheikh amri abeid Arusha, au lake Tanganyika kigoma, approach ya mechi kwenye viwanja kama ivyo lazima ibadilike uwezi kuweka Mpira chini ama Mpira kuflow kama viwanja vingine Bora, ivyo unaweza kuona yanga anapata shida ukadhani ameshuka kiwango lakini inakuwa ni namna ya kucheza kimbinu ili kupata point 3 muhimu kwenye ivyo viwanja vigumu na kuepusha majeraha kwa wachezaji wanaokuwa wanacheza kwa tahadhali ya kuumia!
Nafikiri nimekujibu vizuri hoja zako kama utakuwa umenielewa utakuwa umepata vitu vya kiufundi vinavyoifanya yanga ionekane imeshuka kwa sasa lakini aijashuka kama mnavyofikiria!
Sio Yanga imeshuka. Na timu nyingine zmeongezeka ubora.Kama Kuna shabiki wa Yanga ambaye haoni Yanga imeshuka Ubora atakuwa na tatizo la kiakili!
Vile vizee ni shida! Nasikia Dube analamika kila akiingia uwanjan anapata maumivu makali ya kichwa! Wazee wa Yanga wawasaidie hawa wachezaji, kuna uhuni unafanywa nje ya uwanja😀Ila yanga wanakamiwa sana, pamoja na kurogwa na wazee wa simba