Sababu za kisayansi kwanini Sarai mke wa Nabii Ibrahim alikuwa na shida ya Uzazi/ Uzazi mgumu

Sababu za kisayansi kwanini Sarai mke wa Nabii Ibrahim alikuwa na shida ya Uzazi/ Uzazi mgumu

LIKUD

JF-Expert Member
Joined
Dec 26, 2012
Posts
18,037
Reaction score
33,681
Vitabu vitakatifu vya Dini zetu pendwa vinamtaja Sarai ama Sarah kama mwanamke aliye kuwa anakabiliwa na changamoto ya UZAZI.

Vitabu hivi vinatueleza kwamba suala la Sarai kuwa na matatizo katika UZAZI lilikuwa ni suala la kiroho.

Hata hivyo suala la Sarai kuwa Na changamoto ya UZAZI linaweza kuelezewa kisayansi Na Hilo ndio lengo langu kuandika makala HII.

Kabla sija zama into details Nianze Kwa kutoa angalizo kwamba haya nitakayo yaeleza Ni maoni yangu binafsi( my personal opinion). Sina maana kwamba nitakacho kiandika hapa ndio uhalisia.

Back to the point. Sarai alikuwa na tatizo la UZAZI Kwa Sababu ambazo Zina maelezo ya kisayansi.

Sababu kuu kwanini Sarai alikuwa na matatizo katika uzazi ni Kwa Sababu ali olewa Na KAKA YAKE WA DAMU MOJA. Kaka ambae wali share baba mmoja lakini mama tofauti.

Naam Ni Kweli kabisa Sarai Na Nabii Ibrahim walikuwa mtu na kaka yake ambao baba Yao alikuwa mmoja isipokuwa mama zao ndio walikuwa tofauti.

Ushahidi wa kimaandiko? INAENDELEA.

Naomba MTU asikoment mpaka nitakapo malizia Uzi
 
USHAHIDI WA KIMAANDIKO KWAMBA NABII IBRAHIM NA SARAH WALIKUWA KAKA NA DADA WALIO SHARE BABA MMOJA ILA MAMA TOFAUTI.

Ukiishia kusoma kitabu cha Mwanzo sura yote ya 12 Na Na Mwanzo 20:2 utaishia kuamini au kufikiria kwmba Ibrahim alimnena Sarah kuwa nduguye ili kuokoa Maisha yake kwamba aliogopa kusema Sarah ni mkewe Kwa Sababu kama angesema.Sarah Ni mkewe basi huko ugenini alipokuwa angeweza kuuwawa Na watu ambao wangevutiwa Na Sarah mkewe ili wamtwae Sarah.

Lakini ukisoma kitabu cha MWANZO 20 : 12 (SOMA NA GENESIS 20:12 ) Ibrahim anafunguka wazi kwamba SARAH KIUKWELI NI DADA YAKE AMBAE WAME SHARE BABA MMOJA LAKINI MAMA TOFAUTI.
Mfano wake ni kama vile DIAMOND Na QUEEN DARLIN ( ASSUMING MZEE ABDULI NDIO BABA MZAZI WA DIAMOND).

Wananzuoni mbalimbali Wana wataja Sarah Na Ibrahim kama MTU Na dada yake ambao walioana.

Hata katika mtandao wa Wikipedia. Sarah anatajwa kama ABRAHAM'S HALF SISTER AND WIFE.

Sarah Na Ibrahim baba Yao mzazi aliitwa TERAH


Swali la KUjiuliza Ni Je Ina maana Sarah Na Ibrahim kuzaliwa Na baba mmoja ndio Sababu pekee iliyo fanya Sarah awe matatizo ya UZAZI? Mbona WaPo watu wengi Tu katika Historia walizaa wakiwa ndugu Tena WA baba mmoja na mama mmoja Na wengine baba n binti zake WA kuwazaa mwenyewe lakini walizaa watoto wengi? What was wrong with Sarah and Abraham?

JIBU LINA KUJIA BAADA YA MUDA MFUPI.
 

Sarah na Ibrahim huenda walirithi TATIZO La kuwa Na changamoto katika UZAZI kutoka Kwa baba Yao Mzee Terah.

Kwa mujibu Biblia Terah baba wa Ibrahim alikuwa Na wake wawili Na katika wake Hao wawili alifanikiwa kupata watoto wanne ambao ni Ibrahim, Sarah, Nahor Na Haran ambae Ni baba wa Lutu. Huyu Haran alifariki kipindi wakati mzee Terah bado anaishi huko kunako Uru ya Wakaldayo ama Irak au Mesopotamia.
Sasa basi Kwa viwango vya Mesopotamia ya kale, mwanaume mwenye wake wawili na katika.wake.hao wawili akawa Na watoto wanne Tu basi mwanaume alihesabiwa kama.mwanaume mwenye shida ya changamoto katika UZAZI

Narudia Tena Ni shida ya changamoto katika UZAZI au UZAZI MGUMU.sijasema mgumba.

Kama Kuna mganga, mchungaji au Ostaz anasoma Uzi Huu atakuwa Shahidi yangu kwamba watu wanao lala Mika kuwa Na shida ya UZAZI asilimia kubwa hawawagi Na shida ya uzazi ama ugumba Kwa asilimia Mia. Wengi wao ni unakuta mtu ana Mtoto mmoja ambae alimzaa mwaka 2007 Na Leo Ni February mwaka 2022 anatafuta Mtoto WA pili hajampata Na mwingine ana watoto wawili Mtoto WA Kwanza kazaliwa 2005 WA pili 2007 Na leo Ni 2022 anatafuta Mtoto WA tatu hajapata Hawa nao huwa wanajiona kama wagumba vile Na hujiweka katika kundj la watu wenye shida ya uzazi. Baba wa Ibrahim Na Sarah alikuwa katika kundi hili. Je MTU anaweza KURITHI tatizo la changamoto ya uzazi Kwa wazazi wake? Jibu linafuata
 
Tafiti ZA KISAYANSI ZINASEMA MTU hawezi kurithi tatizo la ugumba au changamoto ZA UZAZI kutoka Kwa wazazi wake ila anaweza kurithi MATATIZO ya KIAFYA yenye uwezo WA kurithiwa ambayo huathiri suala zima la UZAZI. Kwa hiyo tunaweza kusema kwamba huenda Terah alikuwa Na matatizo ya kiafya yenye kuweza kurithiwa , matatizo yaliyo incapacitate uwezo wake wa kupata watoto . Sarah Na Ibrahim walirithi matatizo hayo ndio maana matatizo hayo yaka incapacitate uwezo wao wa kupata watoto. Naendelea
 
Kwa kuwa Sarah Na Ibrahim walikuwa wote Kwa pamoja wamerithi tatizo Hilo ilikuwa ngumu Zaidi Kwa wao kupata Mtoto . PENGINE Sarah angeweza kubeba ujauzito Kwa haraka Na mapema Zaidi kama angekuwa ameolewa namtu kutoka damu nyingine ambae probably Hana matatizo ya kiafya ya kurithi yenr kuweza Ku incapacitate uwezo WA kuzaa . The same as IBRAHIM. Lakini Kwa kuwa walikuwa wameoana wote wenye tatizo Moja ndio maana UZAZI ukawa MGUMU Sana kwao.

Inaendelea
 
MAANDIKO YANAYO PROVE NADHARIA YANGU KWAMBA TATIZO LA SARAH NA IBRAHIM LILIKUWA LA KISAYANSI

Huenda Ibrahim alijua kabisa kwamba tatizo lake ni tatizo la kurithi Na kwamba uwezekano WA yeye kumpa ujauzito Sarah ulikuwa Ni MGUMU Sana .

Kumbuka kuwa Ibrahim alikuwa Ni mti mwenye instincts/machale ambayo Yapo very powerful. Ukisoma kitabu cha Mwanzo 12 utagundua kwamba Ibrahim alipata machale kwamba watu wanaweza kumtamani mke wake Sarah Na kutaka kumuua yeye ili wamchukue Sarah halafu Kweli ikatokea kama alivyo waza.

Sasa basi huenda Ibrahim alipatwa Na machale kwamba suala la yeye Na Sarah kupata ugumu katika UZAZI lilikuwa suala la kurithi Kwa baba Yao Na kwamba uwezekano WA Sarah kupata ujauzito wake ulikuwa Ni mdogo Sana.

So huenda Mungu aliyaona mawazo ya Ibrahim Na hivyo akaamua kumtoa Ibrahim wasiwasi. Ndio maana ahadi anayo pewa Ibrahim Ni " UZAO WAKO UTAKUWA MWINGI KAMA MCHANGA WA BAHARI NA NYOTA ZA ANGANI"

Umewahi KUjiuliza Kwa Nini aliahidiwa kupewa uzao mwingi?jibu ni rahisi Sana Kwa Sababu katika familia ya Ibrahim kulikuwa Na shida ya UZAZI . Katika Biblia Mungu alikuwa anatoa ahadi kulingana na changamoto au Jambo linalo wakabili WA ahidiwa husika. Wana Israel utumwani waliahidiwa kupewa nchi ya ahadi, Daud alitamani kujenga hekalu la Mungu , Mungu akamuahidi kuwa hekalu litajengwa lakini Na Mtoto wake .. ahadi zipo nyingi Sana Na watu wali ahidiwa kulingana Na changamoto walizokuwa Nazo.

Inaendelea
 
Andiko la pili linalo prove Nadharia yangu Ni MWANZO 16:2 . Katika andiko hili Sarah anamwambia Ibrahim NENDA kamuingilie mjakazi wangu Hajiri LABDA nitapata mrithi kupitia yeye.

Msisitizo upo kwenye LABDA. Yani hata Sarah Ni kama alishajua ukweli kwamba shida yake Na Ibrahim ilikuwa ni ya kurithi ndio maana akamshauri Ibrahim akamuingilie mwanamke mwingine kutoka damu nyingine huenda akapata ujauzito. Hata Sarah hakuwa Na uhakika kama Ibrahim anaweza kumpa ujauzito mwanamke. Na inawezekana ndio maana alimruhusu Kwa Sababu alijua haiwezekani hata Kwa mwanamke mwingine.


Ongeza pia Na lile andiko ambalo Sarah ananukuliwa akicheka baada ya kumsikia mtu Yule akitoa unabii kwamba Sarah atabeba mimba. Sarah alicheka Kwa dharau Kwa Sababu licha ya kwamba alikuwa ameshapitiliza Muda wake lakini pia alijua kwamba shida yake Ni ya kurithi.

Inaendelea
 
PROVE NAMBA 3. IBRAHIM NA SARAH WALIZAA WATOTO WANGAPI?

JIBU NI MTOTO MMOJA ALIE ITWA ISAKA.

SWALI KWANINI WALIZAA MTOTO MMOJA PEKEE?

JIBU: KWA SABABU WALIKUWA NA SHIDA YA UZAZI AMBAYO WALI IRITHI KUTOKA KWA BABA YAO AITWAE TERAH.
 
Vitabu vitakatifu vya Dini zetu pendwa vinamtaja Sarai ama Sarah kama mwanamke aliye kuwa anakabiliwa na changamoto ya UZAZI.

Vitabu hivi vinatueleza kwamba suala la Sarai kuwa na matatizo katika UZAZI lilikuwa ni suala la kiroho.

Hata hivyo suala la Sarai kuwa Na changamoto ya UZAZI linaweza kuelezewa kisayansi Na Hilo ndio lengo langu kuandika makala HII.

Kabla sija zama into details Nianze Kwa kutoa angalizo kwamba haya nitakayo yaeleza Ni maoni yangu binafsi( my personal opinion). Sina maana kwamba nitakacho kiandika hapa ndio uhalisia.

Back to the point. Sarai alikuwa na tatizo la UZAZI Kwa Sababu ambazo Zina maelezo ya kisayansi.

Sababu kuu kwanini Sarai alikuwa na matatizo katika uzazi ni Kwa Sababu ali olewa Na KAKA YAKE WA DAMU MOJA. Kaka ambae wali share baba mmoja lakini mama tofauti.

Naam Ni Kweli kabisa Sarai Na Nabii Ibrahim walikuwa mtu na kaka yake ambao baba Yao alikuwa mmoja isipokuwa mama zao ndio walikuwa tofauti.

Ushahidi wa kimaandiko? INAENDELEA.

Naomba MTU asikoment mpaka nitakapo malizia Uzi
Acha uongo, zamani watu walikuwa wanaona ndugu, hii ipo mpaka Leo kwa baadhi ya makabila na nchi kama Pajistani
 
Prove NAMBA 5: IDADI YA WATOTO WA ISAKA.


ISAKA alimuoa Rebeka akiwa Na umri WA miaka arobaini.

Kwa Sababu Isaka alikuwa ni investors child or inbreeding child au Mtoto Alie tokana Na ndugu WA damu ambao walikuwa Na shida ya UZAZI basi huenda Na yeye pia alirithi shida hiyo hiyo Kwa wazazi wake.


So ISAKA pia alikuwa Na changamoto ya UZAZI katika ndoa yake.

Alimuoa Rebeka akiwa Na miaka arobaini Na walipata watoto mapacha ISAKA akiwa Na miaka 60 Yani miaka 20 baadae.

Na walipata watoto wawili Tu mapacha YAKOBO NA ESAU.

Kabla hatujaenda Kwa watoto wa YAKOBO NA ESAU tuangalie watoto wa ISHMAELI ambae alizaliwa Kwa mama mwingine , mama ambae hakuwa Na damu Moja Na Ibrahim
 
Prove NAMBA 6: Ishamael alikuwa Na watoto WANGAPI?

Jibu : Ishmael alikuwa Na watoto 13.

Ishmael alizaliwa Na mama ambae si WA damu Moja Na Ibrahim. Huenda ndio Sababu kwanini Ishamael hakuweza kurithi matatizo ya kiafya yenye kuweza Ku incapacitate uwezo WA kuzaa.
 
Acha uongo, zamani watu walikuwa wanaona ndugu, hii ipo mpaka Leo kwa baadhi ya makabila na nchi kama Pajistani
Kwa hiyo unakubaliana Na Mimi kwamba Ibrahim alimuoa Sarah ambae ni dada Ake sio?
 
Back
Top Bottom