Sababu za Nikki wa Pili kuamua kuokoka

Sababu za Nikki wa Pili kuamua kuokoka

evonik

JF-Expert Member
Joined
Jun 12, 2015
Posts
3,996
Reaction score
5,156
38f252adfad5cc7c90a24b1211d28a08.jpg

Rappa Nikki wa Pili kutoka kundi la Weusi ameweka wazi na kukiri aliamua kuokoka baada ya kutoka mtaani na kurudi shuleni baada ya matokeo ya awamu ya pili (Second Selection) kutoka na kumrejea shuleni.

Nikki amesema tukio la kuamua kumpokea Yesu (Kuokoka) kulimfanya kuimarisha mahusiano yake na Mungu kutokana na maajabu aliyotendewa kwani hakuwa na pesa za kumuwezesha kwenda kusoma shule binafsi.

"Nilivyokuwaga kidato cha tatu nilisimama mbele ya watu na kuokoka yaani kumpokea Yesu na kumrudia Mungu.......offcoz nilifanya hivyo kwakuwa alinitendea maajabu ya kunitoa kitaa kupitia matokeo mnaita 'second selection' nilikuwa sina issue kitaa wala sikuwa na fedha kwenda private schoool" ameandika Nikki kwenye ukurasa wake wa Instagram.

Rappa Nikki wa Pili kwa sasa anafahamika zaidi kama msanii msomi ambaye kwa sasa anadaiwa kuwa yupo shule kwa ajili ya ngazi ya Uzamifu (PhD)

Nikki kwa sasa ana ngoma mpya inayokwenda kwa jina la Kihasara ambapo anadai Sehemu kubwa ya wimbo huo inazungumzia maisha yake halisi aliyowahi kupitia.

Source : Muungwana Blog
 
Habari za Yesu ni scam tu, kama zilivyo za yule mwingine Muhemedi. Waafrika ndio bado tunaibiwa. Halafu mtu kama huyu anajiita msomi, wakati hayuko conscious!!!
Una maanisha tunaibiwa kwa hii mikataba tunayo saini au vp?
 
Back
Top Bottom