Yanga itaendelea kufanya vibaya hadi itakapomtimua au kumwambia mmoja wa viongozi wake awaombe radhi wana Dar Es Salaam na hususani Wazaramo. Kiongozi huyo muandamizi wa klabu hii ya Jangwani ambaye inawezekana haelewi vema historia ya uundwaji wa team, amedirika kuwakashfu wana Mzizima waliojichangisha vijisenti vyao na kuijenga team kubwa katika ukanda huu wa Africa Mashariki na Kati.
Laana ya jasho la wazee wa mzizima litaiandama klabu kwa kuwa haikuchukua hatua dhidi ya yule aliyewavua nguo waanzilishi wa klabu.
Hapa kuna uwezekano kwamba mkizidi kuchelewa kuchukua hatua laana za wana mzizima zinaweza kuwashukia na kuwaletea madhara hata ya kupigwa mkono na watani wa jadi.
Laana ya jasho la wazee wa mzizima litaiandama klabu kwa kuwa haikuchukua hatua dhidi ya yule aliyewavua nguo waanzilishi wa klabu.
Hapa kuna uwezekano kwamba mkizidi kuchelewa kuchukua hatua laana za wana mzizima zinaweza kuwashukia na kuwaletea madhara hata ya kupigwa mkono na watani wa jadi.