Sadaka ya mbwa, yenye laana, iliyobeba uharibifu, HAIPOKELEWI ng'o!!

Sadaka ya mbwa, yenye laana, iliyobeba uharibifu, HAIPOKELEWI ng'o!!

Rabbon

JF-Expert Member
Joined
Apr 16, 2022
Posts
21,625
Reaction score
33,688
Salaam, Shalom!!!

Kuna wajinga wengi wanaodhani kuwa watumishi wa Mungu na Mungu mkuu kuwa Wana njaa na kudhani kuwa wapo Ili kukusanya sadaka Ili kujiongezea ukwasi,

Usilolijua ni kuwa, SADAKA HUKATALIWA, Fuatana nami.

1. Nabii Elisha, anakataa vitofali sitini vya Dhahabu alivyoleta Naamani, Jemedari wa Jeshi la nchi ya Shamu aliyekuwa na ukoma, sadaka aliyobeba ilibeba ukoma na ilitokana na miungu iliyokuwa kinyume na Mungu wa Nabii Elisha, Mungu mkuu akamkataza Nabii Elisha asipokee sadaka hiyo, amponye Bure bila kupokea chochote Toka kwake, Mtumishi wa Elisha aliingiwa na tamaa, akatangulia mbele na kwenda kupokea sadaka hiyo Kwa Hila, matokeo ni kuwa, Ukoma alioponywa Naamani, ulimrudia mtumishi wa Elisha.

2. Yuda anapokea vipande 30 vya Fedha na kumsaliti Yesu, Yesu akakamatwa na kusulubiwa, Yuda anaamua kuzichukua sadaka na kuipeleka Kwa waliomuhonga wanaokataa, anaamua kuipeleka madhabahuni napo inakataliwa, sadaka hiyo inampelekea kwenda kujinyonga. Sadaka hiyo ilibeba LAANA hivyo HAIPOKELEWI.

3. Kaini anatoa sadaka iliyobeba uharibifu na UOVU Toka ndani ya moyo wake, sadaka Mungu anaikataa, Kaini anaamua kwenda kuua baada ya sadaka yake kukataliwa, ndipo ujue sadaka iliyotokana na UOVU, ukipeleka madhabahuni, itakurudia kukumaliza.

4. Hanania na mkewe, Saphira, wanakubaliana kuuza shamba Ili wapate pesa ya Kutoa sadaka Yao, tamaa inawaingia baada ya kupata pesa, wanaamua kupunguza kiasi Kisha wanapeleka sadaka pungufu kinyume na nadhiri Yao. Ingekuwa Leo wachungaji Hawa wasingejua Hila hiyo, lakini Petro Kwa msaada wa Roho MTAKATIFU anajua na kuikataa sadaka hiyo, matokeo ya kukataliwa sadaka hiyo, mume na mke, wanafia madhabahuni na wanapelekwa kuzikwa, matokeo ni kukataliwa sadaka ya uharibifu.

5. Yesu pia alikataa kupokea sadaka ya Zakayo mtoza ushuru, baada ya kukutana na neema ya Kristo, akaazimia Kutoa nusu ya Mali yake Kwa maskini, na hatuoni popote Yesu akipokea chochote Toka Kwa Zakayo maana pesa zake alizopata akiwa TRA ya Israeli wakati huo, ilitokana na RUSHWA na kupiga madeal na dhuluma, pesa hizo zinatakiwa zirudishwe Kwa maskini na wajane na yatima waliodhulumiwa pesa hizo indirectly, na ndiko Zakayo alikozielekeza sadaka hizo Kwa msaada wa Roho mtakatifu, na Si kuzipeleka madhabahuni,Kanisani.

FUNZO.

1. Ewe kahaba, ukilipwa pesa Kutoka KAZI haramu ya kujiuza, hiyo ni "sadaka ya mbwa" HAIPOKELEWI Kanisani, katika madhabahu takatifu, ukiitoa, unaharakisha MAUTI Yako. Anza kwanza kuacha ukahaba, fanya KAZI halali ,malipo halali ndiyo uyatolee sadaka.

2. Wewe muuaji, umeua mtu Kwa kulipwa, unaona upeleke sehemu ya sadaka hiyo ya Damu madhabahuni, Kanisani, ukidhani utamhonga Mungu akusamehe dhambi,jua kuwa haitapokelewa, na sadaka hiyo itageuka kuwa moto kichwani mwako, hutopata utulivu, tubu kwanza, acha uuaji, fanya KAZI halali ndipo peleka sadaka hiyo madhabahuni.

3. Umeiba pesa za Umma, umetapeli mtu, umepokea RUSHWA, Kisha unachukua sehemu ya pesa hiyo ya wizi na kuipeleka madhabahuni Kanisani, wachungaji na maaskofu na mapadri wa Leo, hawataki kusikia huduma ya unabii ndani ya Kanisa sababu, manabii ndani ya Kanisa wangeona na kuwatimua wezi wasilete sadaka ovu ndani ya Kanisa. Kutoruhusu manabii makanisani ndio chanzo Cha wezi kuleta RUSHWA Kanisani Kisha wanapigiwa makofi Badala ya kutimuliwa kama alivyofanya Elisha kumtimua Naamani asikabidhi Dhahabu Ile madhabahu ya Mungu Mkuu.

4. Unauza au unamiliki bar, unauza pombe, Kisha unachukua sehemu ya mapato yatokanayo na pombe unapeleka Kanisani, yaani unamwambia Mungu Asante Kwa kukusaidia kupata walevi wengi wa kununua pombe Ili ulete sadaka Kanisani, unajidanganya, sadaka hiyo HAIPOKELEWI, itazidisha matatizo kwako na Kwa familia Yako. Acha KAZI hiyo, fanya KAZI halali, Kisha toa sadaka na ZAKA, ubarikiwe.

5. Una chuki na ugomvi na ndugu Yako au Jirani Yako, au mke wako, usipende Kutoa sadaka madhabahuni kabla hujasameheana nao au kumaliza magomvi na tofauti hizo, usiposuluhisha, sadaka Yako itageuka kuwa LAANA na kukuharibia maisha Yako. Ni muhimu sana kuzingatia nisemacho, maana wengi wanatoa sadaka na ZAKA na wanarudi nyuma kiuchumi, kimahusiabo, Kijamii nk nk bila kujua sadaka walizotoa bila TOBA ndio chanzo.

HITIMISHO:
Ikiwa hujampa Yesu maisha Yako na ulikuwa ukitoa sadaka iliyotokana na wizi au dhambi madhabahuni na watumishi wasio na macho ya kiroho wanaipokea na kukuombea baraka fake, kumbe unalaanika na kurudi nyumbani na LAANA Badala ya baraka, unajikuta matatizo yanazidi Badala ya kupungua, fuatisha Sala hii:

EE MUNGU KATIKA JINA LA YESU KRISTO, NINAKUKIRI WEWE KUWA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE, NINAOMBA UNISAMEHE, ULIFUTE JINA LANGU KATIKA KITABU CHA HUKUMU, ULIANDIKE JINA LANGU KATIKA KITABU CHA UZIMA, NIPE UWEZO WA KUISHI MAISHA MATAKATIFU, DHAMBI ISINISHINDE, UOVU USINISHINDE, NINAOMBA HAYO KUPITIA JINA LA YESU KRISTO ALIYE BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU. AAMEN.

Mungu awapendaye sana, Awabariki.

Source : 1. (2 Kings, chapter 5:1.....),

(Mwanzo 4:1-12), (Mathayo 27:3....)

Karibuni 🙏
 
Sijui tumeelewana?

Mungu hapokei RUSHWA, tuache kujidanganya.
 
Salaam, Shalom!!!

Kuna wajinga wengi wanaodhani kuwa watumishi wa Mungu na Mungu mkuu kuwa Wana njaa na kudhani kuwa wapo Ili kukusanya sadaka Ili kujiongezea ukwasi,

Usilolijua ni kuwa, SADAKA HUKATALIWA, Fuatana nami.

1. Nabii Elisha, anakataa vitofali sitini vya Dhahabu alivyoleta Naamani, Jemedari wa Jeshi la nchi ya Shamu aliyekuwa na ukoma, sadaka aliyobeba ilibeba ukoma na ilitokana na miungu iliyokuwa kinyume na Mungu wa Nabii Elisha, Mungu mkuu akamkataza Nabii Elisha asipokee sadaka hiyo, amponye Bure bila kupokea chochote Toka kwake, Mtumishi wa Elisha aliingiwa na tamaa, akatangulia mbele na kwenda kupokea sadaka hiyo Kwa Hila, matokeo ni kuwa, Ukoma alioponywa Naamani, ulimrudia mtumishi wa Elisha.

2. Yuda anapokea vipande 30 vya Fedha na kumsaliti Yesu, Yesu akakamatwa na kusulubiwa, Yuda anaamua kuzichukua sadaka na kuipeleka Kwa waliomuhonga wanaokataa, anaamua kuipeleka madhabahuni napo inakataliwa, sadaka hiyo inampelekea kwenda kujinyonga. Sadaka hiyo ilibeba LAANA hivyo HAIPOKELEWI.

3. Kaini anatoa sadaka iliyobeba uharibifu na UOVU Toka ndani ya moyo wake, sadaka Mungu anaikataa, Kaini anaamua kwenda kuua baada ya sadaka yake kukataliwa, ndipo ujue sadaka iliyotokana na UOVU, ukipeleka madhabahuni, itakurudia kukumaliza.

4. Hanania na mkewe, Saphira, wanakubaliana kuuza shamba Ili wapate pesa ya Kutoa sadaka Yao, tamaa inawaingia baada ya kupata pesa, wanaamua kupunguza kiasi Kisha wanapeleka sadaka pungufu kinyume na nadhiri Yao. Ingekuwa Leo wachungaji Hawa wasingejua Hila hiyo, lakini Petro Kwa msaada wa Roho MTAKATIFU anajua na kuikataa sadaka hiyo, matokeo ya kukataliwa sadaka hiyo, mume na mke, wanafia madhabahuni na wanapelekwa kuzikwa, matokeo ni kukataliwa sadaka ya uharibifu.

FUNZO.

1. Ewe kahaba, ukilipwa pesa Kutoka KAZI haramu ya kujiuza, hiyo ni "sadaka ya mbwa" HAIPOKELEWI Kanisani, katika madhabahu takatifu, ukiitoa, unaharakisha MAUTI Yako. Anza kwanza kuacha ukahaba, fanya KAZI halali ,malipo halali ndiyo uyatolee sadaka.

2. Wewe muuzaji, umeua mtu Kwa kulipwa, unaona upeleke sehemu ya sadaka hiyo ya Damu madhabahuni, Kanisani, jua kuwa haitapokelewa, na sadaka hiyo itageuka kuwa moto kichwani mwako, hutopata utulivu, tubu kwanza, acha ujuaji, fanya KAZI halali ndipo peleka sadaka hiyo madhabahuni.

3. Umeiba pesa za Umma, umetapeli mtu, umepokea RUSHWA, Kisha unachukua sehemu ya pesa hiyo ya wizi na kuipeleka madhabahuni Kanisani, wachungaji na maaskofu na mapadri wa Leo, hawataki kusikia huduma ya unabii ndani ya Kanisa sababu, manabii ndani ya Kanisa wangeona na kuwatimua wezi wasilete sadaka ovu ndani ya Kanisa. Kutoruhusu manabii makanisani ndio chanzo Cha wezi kuleta RUSHWA Kanisani Kisha wanapigiwa makofi Badala ya kutimuliwa kama alivyofanya Elisha kumtimua Naamani asikabidhi Dhahabu Ile madhabahu ya Mungu Mkuu.

4. Unauza au unamiliki bar, unauza pombe, Kisha unachukua sehemu ya mapato yatokanayo na pombe unapelekwa Kanisani, yaani unamwambia Mungu Asante Kwa kukusaidia kupata walevi wengi wa kununua pombe Ili ulete sadaka Kanisani, unajidanganya, sadaka hiyo HAIPOKELEWI, itazidisha matatizo kwako na Kwa familia Yako. Acha KAZI hiyo, fanya KAZI halali, Kisha toa sadaka na ZAKA, ubarikiwe.

5. Una chuki na ugomvi na ndugu Yako au Jirani Yako, au mke wako, usipende Kutoa sadaka madhabahuni kabla hujasameheana nao au kuimaliza magomvi na tofauti hizo, usiposuluhisha, sadaka Yako itageuka kuwa LAANA na kukuharibia maisha Yako. Ni muhimu sana kuzingatia nisemacho, maana wengi wanatoa sadaka na ZAKA na wanarudi nyuma kiuchumi, kimahusiabo, Kijamii nk nk bila kujua sadaka walizotoa bila TOBA ndio chanzo.

HITIMISHO:
Ikiwa hujampa Yesu maisha Yako na ulikuwa ukitoa sadaka iliyotokana na wizi au dhambi madhabahuni na watumishi wasio na macho ya kiroho wanaipokea na kumuombea kumbe unalaanika na kurudi nyumbani na LAANA Badala ya baraka, unajikuta matatizo yanazidi Badala ya kupungua, fuatisha Sala hii:

EE MUNGU KATIKA JINA LA YESU KRISTO, NINAKUKIRI WEWE KUWA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE, NINAOMBA UNISAMEHE, ULIFUTE JINA LANGU KATIKA KITABU CHA HUKUMU, ULIANDIKE JINA LANGU KATIKA KITABU CHA UZIMA, NIPE UWEZO WA KUISHI MAISHA MATAKATIFU, DHAMBI ISINISHINDE, UOVU USINISHINDE, NINAOMBA HAYO KUPITIA JINA LA YESU KRISTO ALIYE BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU. AAMEN.

Mungu awapendaye sana, Awabariki.

Source : 1. (2 Kings, chapter 5:1.....),

(Mwanzo 4:1-12), (Mathayo 27:3....)

Karibuni 🙏
Mchungaji;
Upo Kanisa gani ili nipate siku moja nije nipate mawaidha ya Ibada kutoka Knaisani kwako?
 
Mchungaji;
Upo Kanisa gani ili nipate siku moja nije nipate mawaidha ya Ibada kutoka Knaisani kwako?
Mimi Si Mchungaji,

Ni mtumishi mdogo tu katika shamba la Mungu mkuu.

Ni mwalimu wa watoto WADOGO.

Zaidi ya hapo ,ninahubiri JF.

Ubarikiwe🙏
 
Mimi Si Mchungaji,

Ni mtumishi mdogo tu katika shamba la Mungu mkuu.

Ni mwalimu wa watoto WADOGO.

Zaidi ya hapo ,ninahubiri JF.

Ubarikiwe🙏
Ubarikiwe sana pia
Una naoni gani kuhusiana na positive challenge iliyotolewa kwenye uzi huu hapa chini, ambayo mimi nina uhakakika kuwa wanaoifahamu watakuwa ni watumishi wa Mungu wachache sana?

 
Ubarikiwe sana pia
Una naoni gani kuhusiana na positive challenge iliyotolewa kwenye uzi huu hapa chini, ambayo mimi nina uhakakika kuwa wanaoifahamu watakuwa ni watumishi wa Mungu wachache sana?

Ngoja niipitie ndugu.
 
Ubarikiwe sana pia
Una naoni gani kuhusiana na positive challenge iliyotolewa kwenye uzi huu hapa chini, ambayo mimi nina uhakakika kuwa wanaoifahamu watakuwa ni watumishi wa Mungu wachache sana?

Kuna Kweli kidogo ameandika na Kutoa uongo mwingi.

Neno la Mungu linajitosheleza, limeeleza Kila kitu Kwa usahihi.

Roho wa Mungu asipomsaidia mtu kuijua Kweli ndani ya maandiko lazima apotoke.

Muhimu Tusome neno Kwa msaada wa Mungu.
 
Unaweza ukazianisha hasa sehemu zile ambazo amesema uongo?
Je, vipi kuhusu alichosema kuhusiana na Kitabu cha Ayubu?
Vipi pia kuhusu hizi structures hapa ambazo baadhi yake zimejengwa kabla ya kuumbwa kwa Adamu?

Hakuna buildings zilizojengwa kabla ya Kuumbwa Adam, hazipo!!

Vyote vinefanyika baada ya Kuumbwa Kwa Adam.

Tangu kuubwa Adam na Hawa Eden Hadi leo, haizidi miaka elfu Saba. Yaani siku SITA na masaa kadhaa, miaka Elfu SITA na ishirini na nne.
 
Are you sure🤔
Si maneno yangu,

Ni Neno la Mungu limesema, zipo sadaka ambazo hugeuka LAANA ikiwa zitatokewa madhabahuni bila kuwa makini,

Kumbuka AGANO la kale, kuhani aliyechukua sadaka za watu wake kuzipeleka hekaluni, Patakatifu pa Patakatifu,

Alifungwa Kamba mguuni na kengele, Kamba mguuni na kengele ni special Kwa kumvuta nje ikitokea Mungu amemuua huko ndani ikiwa hakujitakasa Sawa sawa.

Ubarikiwe 🙏
 
Hakuna buildings zilizojengwa kabla ya Kuumbwa Adam, hazipo!!

Vyote vinefanyika baada ya Kuumbwa Kwa Adam.

Tangu kuumbwa Kwa Adam Hadi Leo, haizidi miaka elfu Saba.
unathibitishaje kua haizidi miaka efu saba ?
 
unathibitishaje kua haizidi miaka efu saba ?
Codes za kitabu Cha Daniel na Ufunuo na mwanzo zinathibitisha Hilo.

Utapotimia Mwaka wa elfu Saba , Saba ni namba ya utimilifu, hapo ni umilele na milele. Dunia itakuwa imeteketezwa na kutupwa JEHANUM, patakuwa na Nchi mpya Kwa ajili ya WATAKATIFU milele na milele.
 
unathibitishaje kua haizidi miaka efu saba ?
Tulipo sasa ni siku ya SITA Kwa hesabu za Mungu, yaani mwaka 6024....., Ifikapo mwaka elfu Saba, siku ya Saba, Kila kitu kitakuwa kwishney, ni maisha ya milele na milele Kwa WATAKATIFU na moto WA milele Kwa waovu.
 
Kwa kifupi ni kwamba usitoe sadaka tu
Usipotoa sadaka, usishangae wewe ndio ukawa sadaka.

Hili lilimtokea Isaac mwana wa Ibrahim, ilibaki kidogo tu achinjwe Ili kufanyika sadaka.

FUNZO hapo ni kutafuta Kwa JASHO kilicho halali na HAKI Yako.

Ikiwa una pesa zisizo halali, warudishie wahusika, na wahusika hao ni uliowadhulumu, wapewe yatima na wajane na wasiojiweza. Huko ndiko pesa za dhuluma Huwa zinatoka, maskini anakandamizwa, anadhulumiwa Ili tajiri mwovu apate.

Ndipo Ule msemo aliotoa Yesu unatumia kuwa, ni Rahisi ngamia kupita Tundu la sindano kuliko tajiri kuingia ufalme wa Mungu.

Moyo wako wa TOBA na kujutia dhambi, hiyo ni sadaka kubwa mno Mbele za Mungu.

Ubarikiwe 🙏
 
Tulipo sasa ni siku ya SITA Kwa hesabu za Mungu, yaani mwaka 6024....., Ifikapo mwaka elfu Saba, siku ya Saba, Kila kitu kitakuwa kwishney, ni maisha ya milele na milele Kwa WATAKATIFU na moto WA milele Kwa waovu.
hapo umeni changanya zaidi mkuu,

ila navyofahamu ni kua binadamu wamekuwepo duniani kwa miaka mingi sana sio elfu 7 tuu...

kutokana na ushahidi kama mabaki ya binadamu, michoro ya mapamgoni n.k

hata kwenye Biblia (injili) inasema, hakuna ambae anajua siku ya mwisho ni lini.

kwaiyo wewe ukisema tupo mwaka wa 6024 kati ya 7000 inakuaje ?

ikumbukwe kua watu wameshatabiri maranyingi mwisho wa dunia na haikutokea
 
Back
Top Bottom