Sadney: Yanga ina focus kwenye Social Media na fake branding badala ya kufanya vitu vya maana

Ghazwat

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2015
Posts
23,718
Reaction score
66,267
Mshambuaji Sadney Urikhob ambaye anadaiwa kuikacha timu ya Yanga kwa kuandika barua ya kuvunja mkataba wake kwa kile kinachodaiwa kutolipwa mshahara wake kwa miezi mitatu, amemtolea uvivu mshabiki wa Yanga aliyesema. "Tumefurahi kwa maamuzi yako kwasababu hukufanya kitu"

Baada ya comment hiyo ya mshabiki wa Yanga, mshambuliaji Sadney Urikhob, ambaye kwa sasa inaelezwa yuko kwao nchini Namibia, akamjibu kupitia ukurasa wake wa Instagram.

"Wewe na klabu yako ina focus kwenye social media na fake branding badala ya kufanya vitu vya maana, mimi sio mtumwa na sitakuja kuwa".
 
Me ni mshabiki wa Simba ila niwe mkweli huyo striker hakuna alichokifanya hapo yanga sizani Kama amefikisha hata goal 3 tu japo kacheza michezo mingi hayo maneno alitakiwa aongee ajibu au yule striker mkongo aliyeondoka jina lake nimelisahau ndo wamecheza kwa kiwango kikubwa yanga na wakawa wachezaji muhimu wa yanga hata kuondoka kwao kumeacha pengo kubwa yanga na si huyo mnamibia.
 
Kwahiyo hapaswi kulipwa mshahara wake kwavile hajaonesha kiwango?
 
tatizo la washabiki wa yanga badala ya kuwabana viongozi wao wawalipe mishahara wachezaji wao wanalumbana na wachezaji wanaodai haki zao hivi wanategemea viongozi wao watajirekebisha au wachezaji wataendelea kuwa na moyo au mpaka wachezaji waitishe mgomo kabla ya mechi na simba halafu mkifungwa goli nyingi mdai kuwa Simba walinunua mechi maana hizo ndio zenu
 
Tulipe mishahara kwanza alafu tunaze kulaumu wachezaji, Mimi ni shabiki wa Yanga lkn ukweli tuambizane mpira wa wa dunia ya leo bila hela tuta onana wabaya tu mtu hawezi toka kwao huko aje acheze bila hela una tegemea anatunza vp familia yake
 
Vipi kuhusu dante na lamine moro
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…