Safari ya Mo kuimiliki Simba S.C; Before and After.

sembo

JF-Expert Member
Joined
May 25, 2011
Posts
4,350
Reaction score
3,451
1. Safari yake ilianzia katika kipindi cha TV kilichokua kinafatiliwa na wengi, Mkasi.. Huku akitumia zaidi ya dk. 15 [mda wa kipindi ni dk. 30] kuelezea mapenzi yake "ya dhati" kwa Simba, nini ameshaifanyia Simba na kwanini apewe "auziwe" timu.

2. Kesho yake Magazeti yote, Blog zote za michezo, Mitandao ya kijamii vyote "Mo aitaka Simba".

3. Haikuchukua round, Mara T Shirt za kumpigia kampeni apewe timu zikawa mtaani, Mara vikundi katika mitandao ya kijamii vikaanzishwa ili kumsapoti apewe timu pia "wachambuzi" wa soka wakaanza kuandika kwanini Mo ni mtu sahihi na pekee wa kupewa timu.

3. Baada ya hapo kukawa kimya.. Ilipobaki kama wiki moja ili kufanyika Mkutano Mkuu.. Wanachama "wachache" wakaanza kujazana Msimbazi.. Kushinikiza Mo apewe timu.. Magazeti nayo hayakua nyuma.. "Wanachama lukuki [lundo] waandamana Mo apewe timu"

4. Siku 1 kabla ya Mkutano Mkuu.. Mo anaita vyombo vyote vya habari nchini na kumwaga ahadi lukuki endapo atapewa timu.. Huku akijua usajili unasua sua kwa sababu ya ukata, akanena "nipeni timu niwasaidie katika usajili".

5. Siku ya Mkutano.. Magazeti yote yanaelezea kwa nini Mo apewe timu [na si kwanini asipewe]. Mda wa Mkutano kila Mwanachama ni Mo.. Mo.. Mo..

6. Siku 2 baada ya mkutano, Mo anakabidhi Milioni 100 kama msaada wake katika usajili.

7. Mwezi mmoja baada ya Mkutano, Mo akabidhi Milioni ... kwa ajili ya ...

8. Miezi mitatu baada ya Mkutano, Mkuu, hatimae mchakato wa Simba S.C kua Kampuni wakamilika huku Mo akikabidhiwa umiliki hisa asilimia ... za Simba S.C. [... kwa sababu tunapoeleka tunaweza mpatia zaidi ya 51℅]

Hongera "Mfanyabiashara" Mo katika hili.. Nadhani huu msemo wa wahenga "Before you enter into a game, you should learn how to play it rightly" ulikua mwongozo wako.
 
Kweli Mkuu.. Naimani hizo mbinu hazitaishia hapa.. Atazitumia pia katika kuiendeleza Timu.
Timing yake nzuri sana
1.Amevizia kipindi ambacho wanachama/mashabiki/wapenzi wemechoka kuwa wasindikizaji kwenye ligi-Wanachama/mashabiki/viongozi wamechoka kuitwa wa mchangani wakakubali idea yake
2.Akajua kuwa uongozi wa Aveva na wenzake kwa sasa hawana fedha za kusajili wachezaji akasema atawapa hela ya usajili-Aveva na wenzake wakawa hawana ujanja
 
Tangu swala hili lianze nimekusoma huungi mkono mo kupewa timu naomba sababu Tatu mhimu...
 
Huyu jamaa ni "Mfanyabiashara" Kweli na anajua anachokifanya.. Nimemvulia kofia.
Tangu swala hili lianze nimekusoma huungi mkono mo kupewa timu naomba sababu Tatu mhimu...
Mkuu jambo la muhimu ni kumpa sapoti Mo.. Hata nikieleza kwanini nilikua simuungi Mkono haitasaidia.

Sauti ya wengi ishaongea.. Ambayo wahenga wanasema ni "Sauti ya Mungu".. Hivyo siwezi pingana nao.

Tena tufanye haraka haraka kumpatia timu kama anavyotaka mwenyewe.
 
Mkuu naomba unifafanulie haya mambo ya hisa,faida na hasara na mengine mengi tupate kujua mo anachokikimbilia
 

Thamani ya Simba Sports Club ni huo msaada wa 100m???? Mbona ni mbigu na ardhi?
 
Mkuu naomba unifafanulie haya mambo ya hisa,faida na hasara na mengine mengi tupate kujua mo anachokikimbilia
Mkuu kuhusu darasa la Hisa ni nini.. Na mambo mengine lukuki kuhusu Hisa yameelezewa vyema katika Uzi huu [emoji116]

Hisa ni nini?
 
Thamani ya Simba Sports Club ni huo msaada wa 100m???? Mbona ni mbigu na ardhi?
Kama nilimuelewa vyema Mo;

1. Anadai atatoa Bilioni 20 ili apewe umiliki wa 51℅.. Hii ina maana 49℅ zitakazo milikiwa na wanachama, nazo zinaweza kua Bilioni 20.. Hivyo thamani ya timu kwa ujumla ni Bilioni 40.

2. Hiyo milioni 100 ni msaada [ na si sehemu ya Bilioni 20 anazotoa] wake kwa timu katika kipindi hichi cha usajili
 
Kama Manji tu,, isipokuwa kila mmoja anatumia formular tofauti na ya mwenzie,, ila jawabu wote wanalolipata ni lile lile =TUMEWAKUTA WANACHEZA BAO KWA KUTUMIA KETE ZA ALMASI HIVYO NI KUWACHONGEA BAO ZURI NA KETE ZA GOROLI ILI TUCHUKUE HIZI ALMASI ZOTE.
 
Upo sahihi Mkuu.
 
Hizo 100m ni za kumrahisishia process za kupata 51% waswahili wanasema "penye uzia peleka rupia ".Wanachama wangeelewa hii issue vizuri wasingempa hisa 50% kama ana nia kweli wampe 30-35
 
Hizo 100m ni za kumrahisishia process za kupata 51% waswahili wanasema "penye uzia peleka rupia ".Wanachama wangeelewa hii issue vizuri wasingempa hisa 50% kama ana nia kweli wampe 30-35
Kwani ninyi manji ana mipa kiasi gani?
 
Tena tufanye haraka haraka kumpatia timu kama anavyotaka mwenyewe

Hapana sio haraka haraka.....Wanasimba tuko soooo "desperate" kwa sasa...nadhani kwa mwenendo wa timu yetu kwa miaka kama kumi hivi....ndio maana imekuwa hivi

Naunga mkono haya maamuzi ya wanachama...Lakini MO ni business man...hii haraka nadhani anataka kuingiza watu kingi sehemu Fulani

Simba waende taratbu
 
Belo I agree with you...Hata kama ni 50% +1% lakini sio kwa 20 Bn...20 bn ndogo sana....Kninght Frank wapewe kazi wafanye Proffesional Valuation

Halafu pia nani ataitumia hiyo 20 bn pia bado ni kizungumkuti

coz yeye atakuwa na say kwenye simba (Majority shareholder)

kwa hio hata wakiwekeza kwenye TBond bado itakuwa ni simba imewekeza...na simba ni yeye...kwa hiyo pesa atapata yeye........

ina umuhimu wa kuajiri professional law firm ili kuangalia appropriate structure
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…