Chambusiso
JF-Expert Member
- Jul 11, 2007
- 2,592
- 4,640
Wakati tunakaribia na kujiandaa kwa uchaguzi mkuu ujao ni muda muafaka kuanza kuevaluate viongozi wetu tuliowachagua na kucrosscheck ahadi zao kwa wapiga kura waliozitoa wakati wanaomba kuchaguliwa kipindi kilichopita. Nikiwa kama mkazi wa Tegeta mbunge wangu alituahidi katika baadhi ya ahadi zake kwamba atachukua vijana wetu kwa exchange program kuwapeleka Marekani kwa makubaliano na governor wa jimbo la Birmingham (kama lipo, huenda ni la 51) kwa mafunzo na kuleta vijana wa huko pia kuja kushirikiana nasi kujifunza mambo na kuwezeshana.
Mbunge alisema pia atanunua grader lake binafsi na barabara zote za jimbo la Kawe zitatengenezwa sawasawa kwa kutumia pesa yake (alisema hana shida ya fweza so hatasubiri serikali ndio ifanye) tukasema tumepata mwokozi na maombi yetu yamejibu kwa bashasha kubwa.
Baadaye mbunge akasema pia atapeleka vijana Japan wakajifunze uvuvi wa samaki na baada ya kupata ujuzi sahihi atasimamia wapate boti za kuvua samaki hadi bahari kuu na jimbo letu kwa kweli tukaamini litakua kitovu cha maendeleo na kwa kweli hali ya kiuchumi itabadilika kabisa ndani ya miaka mitano ya malaika huyu wa bwana. Huenda tutatakapompa miaka mingine mitano na mabomba ya maziwa kabisa tutapata.
Kama mpiga kura nauliza wandugu wenzangu haya mambo yalifanyika? Na kwa nature yake inaonekana kabisa yanapimika quantitatively, kwa JF ni jungukuu na halikosi ukoko, naomba wadau wenye namba za matokeo ya hizi ahadi watusaidie kushea hapa tumpime muheshimiwa sana kabla hatujaenda kwenye idea yake ya kuanzisha mradi mkubwa wa kuanzisha benki ya kutunza mbegu za asili.
Vijana wangapi walipata mafunzo? Wapo wapi? Walipewa boti? Ngapi? Wazungu toka Birmingham wangapi walikuja? Wametusaidia kwenye sekta gani? Vijana wangapi wamepata ajira na vipato baada ya hizi program? Barabara ngapi zishatengenezwa? Zenye urefu gani? Kwa kiwango gani? Nk. nk.
Naomba mdau mwenye statistics za performance ya ahadi za huyu jamaa yetu tutathmini utekelezaji wa ilani.
Mbunge alisema pia atanunua grader lake binafsi na barabara zote za jimbo la Kawe zitatengenezwa sawasawa kwa kutumia pesa yake (alisema hana shida ya fweza so hatasubiri serikali ndio ifanye) tukasema tumepata mwokozi na maombi yetu yamejibu kwa bashasha kubwa.
Baadaye mbunge akasema pia atapeleka vijana Japan wakajifunze uvuvi wa samaki na baada ya kupata ujuzi sahihi atasimamia wapate boti za kuvua samaki hadi bahari kuu na jimbo letu kwa kweli tukaamini litakua kitovu cha maendeleo na kwa kweli hali ya kiuchumi itabadilika kabisa ndani ya miaka mitano ya malaika huyu wa bwana. Huenda tutatakapompa miaka mingine mitano na mabomba ya maziwa kabisa tutapata.
Kama mpiga kura nauliza wandugu wenzangu haya mambo yalifanyika? Na kwa nature yake inaonekana kabisa yanapimika quantitatively, kwa JF ni jungukuu na halikosi ukoko, naomba wadau wenye namba za matokeo ya hizi ahadi watusaidie kushea hapa tumpime muheshimiwa sana kabla hatujaenda kwenye idea yake ya kuanzisha mradi mkubwa wa kuanzisha benki ya kutunza mbegu za asili.
Vijana wangapi walipata mafunzo? Wapo wapi? Walipewa boti? Ngapi? Wazungu toka Birmingham wangapi walikuja? Wametusaidia kwenye sekta gani? Vijana wangapi wamepata ajira na vipato baada ya hizi program? Barabara ngapi zishatengenezwa? Zenye urefu gani? Kwa kiwango gani? Nk. nk.
Naomba mdau mwenye statistics za performance ya ahadi za huyu jamaa yetu tutathmini utekelezaji wa ilani.