Mkuu MziziMkavu,tunashukuru sana kwa mchango wako mkubwa unaoutoa kwa wote wenye uhitaji. Umejaliwa elimu ya maarifa tofauti tofauti ambayo mara zote umejitolea kutushirikisha kwa moyo wako wote tena bure kabisa.Wewe ni miongoni mwa wazalendo wa kweli waliopo huko ughaibuni ambao kamwe hawakusahau kwao.Naamini michango yako unayoitoa humu JF ktk majukwaa tofauti tofauti,imesaidia sana kubadiri maisha ya wa TZ wengi. Tunakuombea kwa Mwenyezi Mungu azidi kukubariki katika kazi zako na akujalie afya na nguvu.