Said Ndemla atua Sweden salama, tayari kwa majaribio

kirerenya

JF-Expert Member
Joined
Aug 27, 2013
Posts
1,696
Reaction score
2,253
Said Ndemla amewasili salama nchini Sweden tayari kuanza majaribio yake katika klabu ya AFC Eskilstima inayoshiriki ligi kuu nchini humo.

 
Hongera sana kijana Said. I hope utaonyesha umahiri wako ingawa hiyo timu imeshuka daraja msimu huu
 
Hongera sana kijana Said. I hope utaonyesha umahiri wako ingawa hiyo timu imeshuka daraja msimu huu
Lakini wanatuambia inashiriki ligi kuu.

Hata tom ulimwengu tuliambiwa kaenda sweden kucheza ligi kuu lakini hatumuoni sijui yupo sweeden ipi.

kuna mwingine tuliambiwa kaenda ligi ya daraja la pili spain lakin sijawahi kumwona hata bench.


Nchi hii kila kitu ni uongo uongo tuu.
 
Nahisi huwa wanaenda kujiunga na timu zinazoshiriki ndondo cup
 
Ndemla angebaki tu hapa Bongo, sidhani kama Ulaya wanahitaji viungo wapiga mashuti siku hizi. Kama wakina Himid Mao wameshindwa huko na ubora wao wakudumu National Team sidhani kama yeye ataweza kabisa.

Labda akubari punguzo lake mshahara wake wa hivi sasa ili atokee benchi kwenye timu inayomtaka kumsajili.


Vinginevyo namtakia utalii mwema kwenye taila hilo la Scaninavia.
 

Hata mashuti yenyewe anayopiga huwa hayalengi lango bongo kuna mawakala wajingawajinga sana.. why ndemla? Miaka zaidi ya 6 kwenye ligi hana uhakika wa namba kwenye timu yake... bora hata kichuya unaweza sema anaweza kwenda kukimbia na kupiga chenga huko
 
Ulitaka aende Mwashuiya,haaaa haaaa kumbe chuki zako sio za kisimba na yanga tu,mpaka kwenye maisha binafsi
 
Namtakia mafankio, maisha Ni mapambano, kama wengine waliweza kwa nini isiwe yeye ?) kama wengine walishindwa si lazima yeye.
 
Mwacheni mtoto wawatu akatafute Maisha yake.
 

Wachezaji wengi wa Kibongo watachelewa sana kuingia Ulaya. Kama Agents wa kibongo ndio wenye macho ya kijinga namna hii, Yaani nilitegemea akina Mzamiru na at least hao akina kichura.....kuwasikia wakienda huko. Ona sasa bench warmer ndio aliyepata chance HAHAHAHA
 
muwe mnafuatilia mambo basi.ULIMWENGU alifanyiwa operesheni Afrika kusini na atakuwa nje ya uwanja kwa miezi sita
 
BIBLIA INASEMA HIVI:
Na itakuwa kama ilivyo hali ya watu, ndivyo itakavyokuwa hali ya kuhani; kama ilivyo hali ya mtumwa, ndivyo itakavyokuwa hali ya bwana wake; kama ilivyo hali ya mjakazi, ndivyo itakavyokuwa hali ya bibi yake; kama ilivyo hali yake anunuaye, ndivyo itakavyokuwa hali yake auzaye; kama ilivyo hali yake akopeshaye, ndivyo itakavyokuwa hali yake akopaye; kama ilivyo hali yake atwaaye faida, ndivyo itakavyokuwa hali yake ampaye faida.

Isaya 24: 2
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…