Saigon Club yafanya Khitma kuwarehemu wazee Wa Dar es Salaam waliofanya makubwa kwa Taifa la Tanzania

Saigon Club yafanya Khitma kuwarehemu wazee Wa Dar es Salaam waliofanya makubwa kwa Taifa la Tanzania

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074


Mufti wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubeir katika nasaha zake
amesema historia ya Saigon Club iandikwe kwani kiandikwacho
hudumu.

Mufti akaendelea kusema kuwa Saigon Club ni kielelezo cha
historia ya mji wa Dar es Salaam, Tanzania na wazee wake
waliotangulia mbele ya haki ambao walifanya makubwa kwa
taifa hili.

Saigon Club imeutwisha mzigo huu wa kuiandika historia ya
Saigon kwa Abdallah Tambaza na Mohamed Said.

Naweka hapo chini picha ya Saigon Club ya miaka ya 1970
wakati Saigon bado vijana na wanacheza mpira.

1553445315063.png

Picha kwa hisani ya Aziz wa Azam

1553445488218.png

Kulia ni Hassan (Gilbert Mahinya), Said Ali Abbas, Yakub Mbamba,
Ahmada Digila (Danny Blanchflower) (marehemu) na
Atika Kombo


Picha hii nimeipunguza kuifanya ndogo ili nimuonyeshe rafiki yangu
Ahmada Digila tukimwita Danny Blanchflower jina la mchezaji wa
Uingereza katika miaka ya 1960.

Danny Blanchflower alikuwa mmoja wa wachezaji wazuri sana katika
Ligi ya Uingereza.

Wakati ule kulikuwa hakuna TV lakini tukifuatilia Ligi hii kupitia gazeti la
''Shoot.''

Ahmada tulimpa jina hilo kwa uchezaji wake katika nafasi ya kiungo.

Namkumbuka Ahmada uchezaji wake na jinsi alivyokuwa hodari wa
kuhamasisha timu.

Alikuwapo midfielder mwenzake Khalid Fadhili na yeye ni marehemu
pia.

Khalid tukimwita George Young mchezaji mwingine wa katika Ligi ya
Uingereza.

Saigon kulikuwa na Okasha akicheza kama striker na jina lake
lilikuwa Mazola katika wachezaji ambao Italy haitaweza kumsahau.

Okasha na yeye katangulia mbele ya haki na hawa wote wamekufa
katika umri mdogo sana.

Hassan (GIlbert Mahinya) yeye ni mstaafu akiwa afisa mkubwa Idara
ya IT NPF.

Hassan yeye hakuchukua jina la mchezaji kutoka Ulaya.

Yeye alichukua jina la kiungo hatari sana aliyekuwa Simba kisha akaenda
Yanga, Gilbert Mahinya.

Hadi leo tumekuwa watu wazima Hassan bado tunamwita Hassan Gilbert.

Hivi niandikapo ni kama niko Mnazi Mmoja ambao ndiyo ulikuwa kiwanja chetu
toka tulipokuwa tunajiita Everton hadi tulipokuja kujulikana kama Saigon.

Hii ilikuwa miaka ya katikati 1960 na umri wetu ulikuwa wastani wa miaka 15.
Katika utoto huu wengi wetu tukiwa shule za msingi na wachache sekondari
kama Said Ali Abbas hatukujua kama hii club yetu itakuja kuwa club kubwa
na maarufu sana.

Nilitaka kueleza historia ya Saigon kwa mukhtasari tu kupitia maisha ya wenzetu
wachache waliotangulia.

Mola awasamehe dhambi zao hawa wenzetu wana Saigon Club waitangulia
mbele ya haki na awatie peponi.

Amin
 
Wapumzike kwa amani [emoji120]


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Ni Saigon hii hii kijiwe cha kawaha cha kina Marehemu Ditopile Ukiwaona Mzuzuri Mwinshee Ramadhani ?

Sent using Jamii Forums mobile app
Yamakagashi,
Sijui kwa nini unaiita Saigon Club, ''kijiwe.''

Saigon ni club na tofauti na club kama Gymkhana ni mila na utamaduni
wa wanachama.

Sijapato kuona watu wakinywa kahawa Saigon wakati Gymkhana pale
watu wanakunywa ulevi.

Hata hivyo sijapata kusikiapo watu wakiita Gymkhana kijiwe cha ulevi.
 


Mufti wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubeir katika nasaha zake
amesema historia ya Saigon Club iandikwe kwani kiandikwacho
hudumu.

Mufti akaendelea kusema kuwa Saigon Club ni kielelezo cha
historia ya mji wa Dar es Salaam, Tanzania na wazee wake
waliotangulia mbele ya haki ambao walifanya makubwa kwa
taifa hili.

Saigon Club imeutwisha mzigo huu wa kuiandika historia ya
Saigon kwa Abdallah Tambaza na Mohamed Said.

Naweka hapo chini picha ya Saigon Club ya miaka ya 1970
wakati Saigon bado vijana na wanacheza mpira.

View attachment 1053125
Picha kwa hisani ya Aziz wa Azam

View attachment 1053128
Kulia ni Hassan (Gilbert Mahinya), Said Ali Abbas, Yakub Mbamba,
Ahmada Digila (Danny Blanchflower) (marehemu) na
Atika Kombo


Picha hii nimeipunguza kuifanya ndogo ili nimuonyeshe rafiki yangu
Ahmada Digila tukimwita Danny Blanchflower jina la mchezaji wa
Uingereza katika miaka ya 1960.

Danny Blanchflower alikuwa mmoja wa wachezaji wazuri sana katika
Ligi ya Uingereza.

Wakati ule kulikuwa hakuna TV lakini tukifuatilia Ligi hii kupitia gazeti la
''Shoot.''

Ahmada tulimpa jina hilo kwa uchezaji wake katika nafasi ya kiungo.

Namkumbuka Ahmada uchezaji wake na jinsi alivyokuwa hodari wa
kuhamasisha timu.

Alikuwapo midfielder mwenzake Khalid Fadhili na yeye ni marehemu
pia.

Khalid tukimwita George Young mchezaji mwingine wa katika Ligi ya
Uingereza.

Saigon kulikuwa na Okasha akicheza kama striker na jina lake
lilikuwa Mazola katika wachezaji ambao Italy haitaweza kumasahu.

Okasha na yeye katangulia mbele ya haki na hawa wote wamekufa
katika umri mdogo sana.

Hassan (GIlbert Mahinya) yeye ni mstaafu akiwa afisa mkubwa Idara
ya IT NPF.

Hassan yeye hakuchukua jina la mchezaji kutoka Ulaya.

Yeye alichukua jina la kiungo hatari sana aliyekuwa Simba kisha akaenda
Yanga, Gilbert Mahinya.

Hadi leo tumekuwa watu wazima Hassan bado tunamwita Hassan Gilbert.

Hivi niandikapo ni kama niko Mnazi Mmoja ambao ndiyo ulikuwa kiwanja chetu
toka tulipokuwa tunajiita Everton hadi tulipokuja kujulikana kama Saigon.

Hii ilikuwa miaka ya katikati 1960 na umri wetu ulikuwa wastani wa miaka 15.
Katika utoto huu wengi wetu tukiwa shule za msingi na wachache sekondari
kama Said Ali Abbas hatukujua kama hii club yetu itakuja kuwa club kubwa
na maarufu sana.

Nilitaka kueleza historia ya Saigon kwa mukhtasari tu kupitia maisha ya wenzetu
wachache waliotangulia.

Mola awasamehe dhambi zao hawa wenzetu wana Saigon Club waitangulia
mbele ya haki na awatie peponi.

Amin

Mzee Mohammed Said, Shikamoo, kitambo sana umeandika, na ninapopitia vichwa habari na kuona ni lako hata kabla ya kuona kilichomo ndani huvutwa kuangalia, unayajua mengi. Sasa ulichoandika hapa kinaacha maswali ambayo unajua fika tutajiuliza.

1. Saigon club imeacha historian kubwa sana katika nchi hii. Ni ipi hiyo historian
2. Umejaribu kuipa Saigon club picha ya jambo kuuubwa sana, Mufti kaongea juu yake, kwanini Mufti na sio kiongozi mwingine yeyeto.
3. Huu ufupisho utautanua lini
 
Mzee Mohammed Said, Shikamoo, kitambo sana umeandika, na ninapopitia vichwa habari na kuona ni lako hata kabla ya kuona kilichomo ndani huvutwa kuangalia, unayajua mengi. Sasa ulichoandika hapa kinaacha maswali ambayo unajua fika tutajiuliza.

1. Saigon club imeacha historian kubwa sana katika nchi hii. Ni ipi hiyo historian
2. Umejaribu kuipa Saigon club picha ya jambo kuuubwa sana, Mufti kaongea juu yake, kwanini Mufti na sio kiongozi mwingine yeyeto.
3. Huu ufupisho utautanua lini

Mao,
Mimi nakujibu kwa kuwa ndiye niliyeandika makala hii lakini Saigon Club
ina viongozi wake ambao hili swali ungelielekeza kwao.

Sisi Saigon sote ni wenyeji wa Dar es Salaam ama kwa kuzaliwa au kwa
wazee wetu kuhamia.

Wengi wa wanachama wa Saigon kwa hiyo ni kizazi cha mwishoni 1940
na mwanzoni 1950.

Wazee wetu ndiyo walikuwa wanamji na hawa ndiyo waliotuzaa sisi kwa
hiyo sisi tumerithi yote waliyofanya wazee wetu.

Wazee wetu ndiyo waliounda TAA na kuasisi harakati za kudai uhuru wa
Tanganyika chini ya TANU.

Wazee wetu ndiyo waliowapokea kwa mapenzi wote waliokuja katika mji
huu kutafuta maisha.

Kwa ajili hii basi sisi Saigon tumebeba historia ya Dar es Salaam.

Umeuliza kwa nini Mufti Zubeir kaongea katika khitma ya Saigon.
Naomba nikutengenezee swali lako liwe zuri zaidi.

Kwanza ningependa kukueleza kuwa kwa siku ya jana Mufti Zubeir ndiye
alikuwa mgeni rasmi na hiyo nafasi ya kuzungumza ilikuwa yake na kila
mwaka huwa tunakuwa na viongozi tofauti kama wageni wa heshima.

Ningefurahi sana kama ungeuliza kwa nini tunafanya khitma na kwa nini
katika khitma zote za Saigon tunapoanza kutaja majina ya wazee wetu
huwa tunaanza na masheikh na jina la kwanza linakuwa la Mufti Sheikh
Hassan bin Amei
r?

Nimefupisha maelezo ya kumbukumbu ya wachezaji wa Saigon wengi
wao wametangulia mbele ya haki kwani historia ndefu inayowahusu
watu wengi.

In Shaa Allah iko siku historia hii itakuja kuandikwa kwa manufaa ya
taifa letu.

1553506971519.png

Makamu wa Rais wa Tanzania Dr. Gharib Bilal akiwa Mgeni Rasmi akiingia Saigon Club katika khitma ya mwaka wa 2010.
 
Back
Top Bottom