Red Giant
JF-Expert Member
- Mar 9, 2012
- 15,657
- 20,967
Panic attack ni nini?
Panic attack ni uoga mkubwa unaompata mtu.uko kwenye kundi la magonjwa ya wasiwasi (anxiety disoders). Uoga huu huweza mpata mtu kwa sababu maalum kama vile kuona nyoka. Pia inaweza kutokea bila hata sababu maalum, yaani unaweza ukawa umetulia tu na kushangaa unapata dalili zifuatazo.
Uoga, kutetemeka, moyo kwenda mbio, kutetemeka na kutoka jasho, maumivu ya kifua, kuhisi kushindwa kupumua, kuhisi kukabwa kooni, kuhisi kichefuchefu, tumbo kuchafuka , kuhisi kizunguzungu na kuzimia, kuhisi kuchanganyikiwa na kuhisi kufakufa, kutojitambua (kujihisi kama sio wewe).
Watu wengine hali hii huwapata usiku wakiwa usingizini. Watu hawa hushtuka na kuhisi walikuwa wanakabwa na wachawi au wamepata heart attack lakini ukweli ni kuwa wamepata panic attack. Hali hii kama inatokea mara kwa mara linaweza kumuathiri sana mtu akiwa kazini,shuleni na maisha yake kwa ujumla. hii nikwasababu mtu anaanza kuogopa kujumuika na watu kwa kuogopa hali hii kumkuta.
Watu 30 kati ya 100 hupata panic attack walau mara moja maishani. Pia watu 3 kati ya 100 tatizo hili hujirudia ruudia na tunasema wanapanic disorder. Pia inasemekana kati ya watu 100 wanaoenda kuwaona madaktari wa moyo 60 huwa ni panic attack. Wanawake wanauwezekano mara mbili wa kupata panic attack ukifananisha na wanaume.
Nini husababisha panic attack?
Hali hii husababishwa ubongo kuwa na uwezo mdogo wa kuhimili uoga. Pia kuna hali inaitwa anxiety ambayo mtu anakuwa na wasiwasi sana na maisha yake au afya yake. Hali hii inaweza kusababisha kupatwa na panic attack. Pia maisha ya stress huweza kumsababishia mtu kupata panic attack.
Matibabu
Matababu ya kwanza hulenga kumuondolea mtu wasiwasi (anxiety) na kumuondolea stress maishani.kuondoa wasiwasi hujumuisha mafunzo ya kurelax na kumuexpose mtu kwenye mazingira yanayomletea attack ili ayazoee. Pia kupata elimu kuhusu hali hii ni sehemu ya matibabu. Pia kuna mbinu mbali mbali za kupunguza stress.
pia Kuna dawa za kutibu kama alprazolam ambayo hutumika kwa matibabu ya muda mfupi na dawa kama clomipramine kwa matibabu ya muda mrefu.
Kwa msaada wa kitabu abnormal psychology cha Robin Rosenberg na Stephen Kosslyn.
wenu katika kupani Red Giant.
Panic attack ni uoga mkubwa unaompata mtu.uko kwenye kundi la magonjwa ya wasiwasi (anxiety disoders). Uoga huu huweza mpata mtu kwa sababu maalum kama vile kuona nyoka. Pia inaweza kutokea bila hata sababu maalum, yaani unaweza ukawa umetulia tu na kushangaa unapata dalili zifuatazo.
Uoga, kutetemeka, moyo kwenda mbio, kutetemeka na kutoka jasho, maumivu ya kifua, kuhisi kushindwa kupumua, kuhisi kukabwa kooni, kuhisi kichefuchefu, tumbo kuchafuka , kuhisi kizunguzungu na kuzimia, kuhisi kuchanganyikiwa na kuhisi kufakufa, kutojitambua (kujihisi kama sio wewe).
Watu wengine hali hii huwapata usiku wakiwa usingizini. Watu hawa hushtuka na kuhisi walikuwa wanakabwa na wachawi au wamepata heart attack lakini ukweli ni kuwa wamepata panic attack. Hali hii kama inatokea mara kwa mara linaweza kumuathiri sana mtu akiwa kazini,shuleni na maisha yake kwa ujumla. hii nikwasababu mtu anaanza kuogopa kujumuika na watu kwa kuogopa hali hii kumkuta.
Watu 30 kati ya 100 hupata panic attack walau mara moja maishani. Pia watu 3 kati ya 100 tatizo hili hujirudia ruudia na tunasema wanapanic disorder. Pia inasemekana kati ya watu 100 wanaoenda kuwaona madaktari wa moyo 60 huwa ni panic attack. Wanawake wanauwezekano mara mbili wa kupata panic attack ukifananisha na wanaume.
Nini husababisha panic attack?
Hali hii husababishwa ubongo kuwa na uwezo mdogo wa kuhimili uoga. Pia kuna hali inaitwa anxiety ambayo mtu anakuwa na wasiwasi sana na maisha yake au afya yake. Hali hii inaweza kusababisha kupatwa na panic attack. Pia maisha ya stress huweza kumsababishia mtu kupata panic attack.
Matibabu
Matababu ya kwanza hulenga kumuondolea mtu wasiwasi (anxiety) na kumuondolea stress maishani.kuondoa wasiwasi hujumuisha mafunzo ya kurelax na kumuexpose mtu kwenye mazingira yanayomletea attack ili ayazoee. Pia kupata elimu kuhusu hali hii ni sehemu ya matibabu. Pia kuna mbinu mbali mbali za kupunguza stress.
pia Kuna dawa za kutibu kama alprazolam ambayo hutumika kwa matibabu ya muda mfupi na dawa kama clomipramine kwa matibabu ya muda mrefu.
Kwa msaada wa kitabu abnormal psychology cha Robin Rosenberg na Stephen Kosslyn.
wenu katika kupani Red Giant.