Lavit
JF-Expert Member
- May 16, 2011
- 14,834
- 32,522
Sasa ni takribani miaka 12 toka atoweke duniani msanii na mtayarishaji maarufu wa muziki wa Bongo Fleva akijulikana kama Complex.
Jina la Complex lilianza kusikika hasa pale aliposhirikishwa na msanii mahiri kwa wakati huo akijulikana kama AY. Ay alimshirikisha Complex katika kibao chake cha Raha Tu Remix, hali iliyopelekea kujenga urafiki mkubwa baina ya hawa wawili.
Urafiki wa Ay na Complex ndiyo uliokuja kuwakutanisha Vivian na Complex, ikumbukwe kwamba hapo kabla tayari Ay na Vivi walikuwa wakifahamiana na ni Ay aliyefanya juhudi za kumkutanisha Vivi na Gadner na kupelekea kuajiriwa pale Clouds Media.
Complex aliweza kushirikishwa katika "hit songs" kama Nawakilisha (Prof J), Safari Njema (Jay Moe) , Njoo nikupe love (Bush Baby), Nimezama Remix (Ray C) , Hii Mic (TID) na Walidhani ya Zahrani.
Complex aliweza kufanya ngoma zake kama Hakuna hatari, Bab kubwa feat Jaydee, Wakati ndio huu feat Ay, Vita, Kufa na kupona pia Nyamaza aliyokuwa na Barish, Squeezer na Dataz. Mpaka leo hii Hakuna Hatari ndiyo ngoma iliyoacha kumbukumbu katika kazi zake mwenyewe.
Complex aliendelea na kazi ya Uproducer katika studio za Aigies na baadaye Backyards Studio. Wakati huo huo mpenzi wake Vivian aliweza kutoa ngoma kama Hip Hop muhimu akimshirkisha Ay, Siwaelewi akiwa na Dully pia kalamu na karatasi aliyoimba na Nuruely.
Tarehe 21 ya August mwaka 2005 ndiyo siku ambayo Complex na Vivi walipata ajari wakitokea Moro kwenye show ya Fiesta ambayo kwa wakati huo ilijulikana kama Moto zaidi, hiyo ndiyo ulikuwa mwisho wa safari ya hawa wawili katika muziki na mapenzi yao pia.
Jina la Complex lilianza kusikika hasa pale aliposhirikishwa na msanii mahiri kwa wakati huo akijulikana kama AY. Ay alimshirikisha Complex katika kibao chake cha Raha Tu Remix, hali iliyopelekea kujenga urafiki mkubwa baina ya hawa wawili.
Urafiki wa Ay na Complex ndiyo uliokuja kuwakutanisha Vivian na Complex, ikumbukwe kwamba hapo kabla tayari Ay na Vivi walikuwa wakifahamiana na ni Ay aliyefanya juhudi za kumkutanisha Vivi na Gadner na kupelekea kuajiriwa pale Clouds Media.
Complex aliweza kushirikishwa katika "hit songs" kama Nawakilisha (Prof J), Safari Njema (Jay Moe) , Njoo nikupe love (Bush Baby), Nimezama Remix (Ray C) , Hii Mic (TID) na Walidhani ya Zahrani.
Complex aliweza kufanya ngoma zake kama Hakuna hatari, Bab kubwa feat Jaydee, Wakati ndio huu feat Ay, Vita, Kufa na kupona pia Nyamaza aliyokuwa na Barish, Squeezer na Dataz. Mpaka leo hii Hakuna Hatari ndiyo ngoma iliyoacha kumbukumbu katika kazi zake mwenyewe.
Complex aliendelea na kazi ya Uproducer katika studio za Aigies na baadaye Backyards Studio. Wakati huo huo mpenzi wake Vivian aliweza kutoa ngoma kama Hip Hop muhimu akimshirkisha Ay, Siwaelewi akiwa na Dully pia kalamu na karatasi aliyoimba na Nuruely.
Tarehe 21 ya August mwaka 2005 ndiyo siku ambayo Complex na Vivi walipata ajari wakitokea Moro kwenye show ya Fiesta ambayo kwa wakati huo ilijulikana kama Moto zaidi, hiyo ndiyo ulikuwa mwisho wa safari ya hawa wawili katika muziki na mapenzi yao pia.