demigod
JF-Expert Member
- Jan 2, 2015
- 8,292
- 15,250
Nakumbuka nilisema juzi humu kuwa kuna pahala Simba SC wanakosea. Huwezi kuifanya klabu iendeshwe kwa weledi na wakati huo huo unaiendesha kwa Uhuni wa kizamani.
Nilikuwepo na Social Media Content Manager pande fulani usiku wa Jana. Jamaa akanimwagia mchele chini ya kwamba sakata la BM kusaini Simba SC litaondoka na mtu, Sikumuelewa.
Mapendekezo ya usajili wa wachezaji wapya yalioachwa na kocha Kishingo alikuwa nayo mtendaji mkuu wa klabu ambaye ni msouth afrika bwana Senzo Mbatha. Kwa utaratibu wa kiuweledi yeye ndiye anayehusika na masuala ya usajili wa aina ya mchezaji kutokana na ripoti ya mwalimu aliyo iacha.
Baada ya BM kusajiliwa Jana, jamaa akashtuka. Maana ulikuwa usajili ambao wala haukuwa kwenye mapendekezo ya mwalimu. Senzo ikabidi amvutie waya Bwana Mo, Boss akamwambia yeye alitaarifiwa na baadhji ya viongozi kuhusu kuhitajika kwa pesa kwa ajili ya mchezaji fulani na yeye akaidhinisha.
Senzo akaamua kuthibitisha kwa Mwalimu mkuu ikiwa kama yeye pia alichangia usajili huo ambao yeye mhusika hakihusishwa hata kwa asilimia 1. Mwalimu akasema ahusiki kwakuwa yeye alikwisha acha repoti ya wachezaji wanao hitajika.
Mtendaji Mkuu huyo akaamua kuachia ngazi klabuni hapo kwa madai ya kuwa anaingiliwa kwenye majukumu yake kwa kulazimishwa kuenenda na tamaduni ya usajili wa klabu hiyo. Pia hofu ya kutiwa doa kwa CV yake na sifa yake kiujumla kumempelekea kuachia ngazi.
Nilikuwepo na Social Media Content Manager pande fulani usiku wa Jana. Jamaa akanimwagia mchele chini ya kwamba sakata la BM kusaini Simba SC litaondoka na mtu, Sikumuelewa.
Mapendekezo ya usajili wa wachezaji wapya yalioachwa na kocha Kishingo alikuwa nayo mtendaji mkuu wa klabu ambaye ni msouth afrika bwana Senzo Mbatha. Kwa utaratibu wa kiuweledi yeye ndiye anayehusika na masuala ya usajili wa aina ya mchezaji kutokana na ripoti ya mwalimu aliyo iacha.
Baada ya BM kusajiliwa Jana, jamaa akashtuka. Maana ulikuwa usajili ambao wala haukuwa kwenye mapendekezo ya mwalimu. Senzo ikabidi amvutie waya Bwana Mo, Boss akamwambia yeye alitaarifiwa na baadhji ya viongozi kuhusu kuhitajika kwa pesa kwa ajili ya mchezaji fulani na yeye akaidhinisha.
Senzo akaamua kuthibitisha kwa Mwalimu mkuu ikiwa kama yeye pia alichangia usajili huo ambao yeye mhusika hakihusishwa hata kwa asilimia 1. Mwalimu akasema ahusiki kwakuwa yeye alikwisha acha repoti ya wachezaji wanao hitajika.
Mtendaji Mkuu huyo akaamua kuachia ngazi klabuni hapo kwa madai ya kuwa anaingiliwa kwenye majukumu yake kwa kulazimishwa kuenenda na tamaduni ya usajili wa klabu hiyo. Pia hofu ya kutiwa doa kwa CV yake na sifa yake kiujumla kumempelekea kuachia ngazi.