Sakata la Bundles - Suluhisho

Sakata la Bundles - Suluhisho

Logikos

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2014
Posts
15,460
Reaction score
24,233
Kutokana na Mvutano uliopo kati ya Serikali, Watoa Huduma na Wananchi kuhusu Bundles na Shutuma za Wizi inabidi sisi wananchi tuelewe tunataka nini na Wizi ni nini?

Issue za Wizi:
Kama kuna issue za Wizi na mtu kaibiwa kuna vyombo vya kisheria na TCRA inabidi mwananchi aweze kupeleka issue zake huko ili asaidiwe, na hapa wizi ni kuuziwa tofauti na makubaliano yaani unanunua mb 10 unapewa mbili na sio gharama ya bei

SULUHISHO

A: Serikali ikae Kando

Mbaya katika haya mambo mara zote ni Serikali kuingilia haya mambo na mara nyingine gharama inatokana na Tozo / Au Sheria za Serikali, Wote tunakumbuka SKYPE ilivyokuja nchi kama Tanzania ilikuwa inazuiliwa eti TTCL itakosa mapato..., Juzi Juzi tunakumbuka Serikali iliipa Mitandao Bei elekezi na kilichotokea mitandao yote ikacheza kwenye zile Bei Elekezi!!! (ALAS!! kumbe Bando zilikuwa bei rahisi kuliko Bei Elekezi hivyo Bei zikapanda na Mitandao yote Bei zikawa sawa zote Juu); Kumbe Ushindani ulipelekea kila kampuni kushusha to the minimum sasa kuwekewa bei elekezi wote wakawa na bei sawa...

Kumbuka pia huyu Mtetezi mwisho wa siku anatetea Mapato yake na sio necessarily bei rahisi kwa mtumiaji (Refer Matamko ya Naibu Spika akimwambia Waziri akaangalie ni vipi wanaweza kupata fedha zaidi kutoka kwenye Data)

Au Kuna waziri alishasikika wacheki ni vipi wanaweza kupata pesa kwenye mitandao kama Whats-app

Kuwepo kwa bei elekezi huenda kweli bei ikashuka lakini vipi kuhusu quality ? Sababu kama wote bei zitakuwa sawa na huwezi kuwavuta wateja kwa bei huenda quality ikawa minimum na uwekezaji ukashuka... AFTER ALL UBINAFSHAJI TULIFANYA ILI ULETE USHINDANI sasa tukipangiana Bei kwa Sheria Ushindani utapotea... Kwahio ushauri wangu Hii Mitandao Binafsi iachwe hata ikitaka kuuza Bundle kwa Laki moja ifanye hivyo Tigo wakipandisha watu watahamia Halotel na Voda..., Ingawa kuna uwezekano wa Cartels hii Mitandao kukaa pamoja na kupanga Bei nadhani Suluhisho la kuzuia hilo ni Hapo Chini B:

B: Ili Kuepusha Cartels na Bei kupanda sana Juu Serikali Iwekeze / Maintain Quality ya Mashirika yake TTCL na Airtel (ambapo wana Share nyingi)

Huwezi kumpangia mtu bei wakati hujui uwekezaji wake upo vipi, ni kweli huenda leo napata faida kubwa ila ninawekeza kwenye Research and Development kwa ajili ya Kesho ya Promotion ili kuwafahamisha wadau kwamba bei zangu ni ndogo kuliko za jirani.

Sababu ni ushindani na ushindani ndio determinant na kuepusha upangaji wa bei Serikali na kama Serikali inaona bei fulani ndio halisi kwa mwananchi kuchajiwa basi ihakikishe hizo bei na hizo Quality zinatolewa na mashirika yake ambayo ni TTCL na AIRTEL, yaani hizi Kampuni mbili ndio pace setters, Bei ndogo na Quality ya Juu hivyo basi hizo nyingine zitakuwa hazina jinsi ili kupata wateja ni either kushusha kama TTCL au zaidi ya TTCL

C: Serikali iangalie manufaa yanayotokana na Outcomes za Cheap Bundles na Sio Kutaka kupata Pesa Directly
Juzi tu hapa tumepata mkopo wa TEHAMA na kila siku tunaimba ngonjera za vijana kujitafutia ajira na kuongeza uvumbuzi..., Kwahio kama kweli tunataka kuleta / kuhimiza ukuaji wa TEHAMA tuanzie kwenye kufanya Bundle kuwa as Cheap as Possible..., na hilo linaweza kufanyika kwa Serikali kupunguza kuchota kwenye Data na sio Kuongeza Uchotaji..., Kuliko kuomba misaada ya sijui kuwekeza kwenye majengo ya TEHAMA tunaweza kuwekeza kwenye kutokuchaji TOZO nyingi kwenye DATA hivyo vijana wanaweza wakajifunza wenyewe kwenye mitandao (Karne hii Information zipo Widely available and for Free)

D: Tuache Siasa na Cheap Politics
Badala ya kuwekeza sijui kwenye TUME / SHERIA na Wadau (tunaowalipa kwa gharama) kukaa vikao vya kila mara ili waonekane kwamba wanawatetea wananchi lakini ukweli ni kwamba tunaongeza gharama za kuwalipa watu na hii mitandao tunaiongezea gharama za kuajiri wanasheria na consultancy firms kuona ni vipi wanaweza wakafanya lobbying ili bei ifike ile wanayotaka - Kwahio kwenye hizi Siasa ni kwamba tunawapatia ulaji wachache...

C: Wananchi tuelewe tunataka Kupata nini na Wizi ni Nini
Wananchi inabidi tuelewe tunataka nini ? Kupangiana Bei au Soko Huria ? Na wizi ni nini ? : Sababu wizi ni kufanya / kwenda tofauti na makubaliano, sasa kama inabidi usome vigezo na masharti na ushaambiwa kwamba hili bundle linakwisha masaa 24 basi ukiona hutaki unataka likae mwaka basi ongea na Kampuni wape proposal ya ma-bundle ya mwaka wakiona kuna wateja watafanya hivyo na huenda ukalipwa kwa mawazo yako mazuri...

Sababu ukinganganiza Bundle la Masaa 24 sijui likae wiki huenda Kampuni limeweka hilo bundle wakijua kwamba Jtatu watumiaji ni wachache hivyo tushushe bei ili watumie wengi zaidi ila likikaa wiki alafu jmosi ambapo watumiaji ni wengi huenda capacity ikajaa na hata wale wanaotulipa 1000/= wasipate the required quality

Hivyo wananchi tutumie Power yetu ya Choice Kampuni A ikizingua tuhamie Kampuni B na Kampuni zote zikipanga zituibie tuna Kampuni yetu ya TTCL tuibane Serikali iweze kuifanya hii Kampuni iwe mfano ili wengine waige..., na hizo suggestions zetu tuzipeleke huko TTCL ambapo atleast sisi ni wamiliki na sio Hizo Kampuni Binafsi ambazo hatukuzisaidie kuwekeza leo tuwapangie vya kufanya....
 
Hawa majamaa ni wanyonyaji sana sometimes unaweza ukawa unawahisi vibaya makampuni ya simu ila kauli za Nape zikaku prove wrong kabisa

Kama mtanzania mwenzako anaweza kukufanyia undava kama huu si bora mara 10 utawaliwe na mkoloni anaweza akawa na sababu ya msingi
 
Hawa majamaa ni wanyonyaji sana sometimes unaweza ukawa unawahisi vibaya makampuni ya simu ila kauli za Nape zikaku prove wrong kabisa

Kama mtanzania mwenzako anaweza kukufanyia undava kama huu si bora mara 10 utawaliwe na mkoloni anaweza akawa na sababu ya msingi
Hii Serikali acha tu yaani ndio Hindrance ya mambo mengi...

Kipindi watu tunahangaika na TTCL kupigia ndugu zetu huko mtoni wakati kuna SKYPE huku ilikuwa Inapigwa marufuku (Eti itapunguzia mapato TTCL)..., Yaani leo nina uhakika ukija na innovative ya watu kuongea bure watasema achana nayo hio tutakosa TOZO au wao ndio watapanga Bei. ili wapate TOZO zao....

Sasa kuliko tuwapangie kina VODA na TIGO (ambao hata kama wanapata faida kubwa ila pia kuna Research and Development zinabuma au hizo pesa wanazitumia kuwapa mapesa zaidi wafanyakazi wao au wanawapa panya wazile - "who cares") Kwanini Serikali wasideal na Kampuni yao na hizo Innovative Ideas zote nzuri nzuri wazipeleke huko TTCL na Bei zishuke Huko TTCL ?!!!! Kwa kufanya hivyo sisi walaji watakuwa wametupa the cheapest choice (TTCL) hao wengine itabidi waige...
 
Hii Serikali acha tu yaani ndio Hindrance ya mambo mengi...

Kipindi watu tunahangaika na TTCL kupigia ndugu zetu huko mtoni wakati kuna SKYPE huku ilikuwa Inapigwa marufuku (Eti itapunguzia mapato TTCL)..., Yaani leo nina uhakika ukija na innovative ya watu kuongea bure watasema achana nayo hio tutakosa TOZO au wao ndio watapanga Bei. ili wapate TOZO zao....

Sasa kuliko tuwapangie kina VODA na TIGO (ambao hata kama wanapata faida kubwa ila pia kuna Research and Development zinabuma au hizo pesa wanazitumia kuwapa mapesa zaidi wafanyakazi wao au wanawapa panya wazile - "who cares") Kwanini Serikali wasideal na Kampuni yao na hizo Innovative Ideas zote nzuri nzuri wazipeleke huko ?!!!!

Na sisi walaji Serikali watakuwa wametupa the cheapest choice hao wengine itabidi waige...
Huwa na wish siku moja kwenye hayo makampuni utokee mlipuko mkubwa ambao utaharibu miundombinu na kuwatia hasara kubwa ambayo itawahitaji miaka kadhaa ku fix

Yani wakisema waanze kufanya repair wajirudi upya uwe ni mchakato mgumu sana halafu unaoenda taratibu

Katika hicho kipindi ambacho watakuwa wanateseka pengine wataelewa hizi kelele za mateso tunayo lalamika kila siku afu wao wanatupuuza.

Kiukweli nawaombea mabaya zaidi ya hayo
 
Huwa na wish siku moja kwenye hayo makampuni utokee mlipuko mkubwa ambao utaharibu miundombinu na kuwatia hasara kubwa ambayo itawahitaji miaka kadhaa ku fix

Yani wakisema waanze kufanya repair wajirudi upya uwe ni mchakato mgumu sana halafu unaoenda taratibu

Katika hicho kipindi ambacho watakuwa wanateseka pengine wataelewa hizi kelele za mateso tunayo lalamika kila siku afu wao wanatupuuza.

Kiukweli nawaombea mabaya zaidi ya hayo
Tatizo tunatafuta mchawi ambapo hayupo.... Hizi Kampuni zina makosa gani ?

Kampuni hizi kazi yao sio Service (hio ni aftermath) kazi yao first and farmost ni kutengeneza Pesa kwao na Shareholders wao..., kwahio tukadhani kwenye ushindani wakishindana wenyewe kwa wenyewe basi bei zitashuka.... (free market)

Ila ukiangalia Serikali kuna kipindi ilitoa bei elekezi (makampuni yakafuata bundle zote zikafutwa) na bei kupanda maradufu..., kwahio utaona kwamba hizi Kampuni zikifuata kama Serikali inavyotaka huenda kutakuwa hakuna ahueni...

Ila Serikali kama inataka inashindwa nini kuonyesha mfano kwenye Kampuni yao !, Sababu tukianza kuzipangia hizi kampuni huenda zikaacha kuwekeza kama zinavyofanya sasa...,

Pili usitegemee Serikali (inayotaka Mapato) ikushushie bei, bei itashuka tu kulingana na wananchi kuwa na choices zaidi ya moja na sababu katika hizo choices kampuni mojawapo ni ya kwetu (TTCL) kwanini hii isiwe mfano ? Kwanini tusumbuke na hizi Kampuni Binafsi wakati tunayo ya kwetu ya kuipigia kelele ?

By the way TTCL Customer Care inamiundo mbinu kiasi gani kwanini inashindwa kazi ? Huyu Nape kwanini asiwekeze nguvu zake kule na kutengeneza the best model for business huko (Shamba Darasa)..
 
Hawa majamaa ni wanyonyaji sana sometimes unaweza ukawa unawahisi vibaya makampuni ya simu ila kauli za Nape zikaku prove wrong kabisa

Kama mtanzania mwenzako anaweza kukufanyia undava kama huu si bora mara 10 utawaliwe na mkoloni anaweza akawa na sababu ya msingi
Kama umesoma mfumo wa Oligopoly haitakusumbua kuelewa mitandao ya simu inaoperate vipi. Kifupi serikali ndio inahusika na bei za Bando,

Angalia vifurushi ambavyo sio mainstream kama Tigo postpaid, Vodacom Supakasi etc Voda wanatoa Unlimited 5G, nchi chache sana duniani wana huduma kama hii, wameweza kufanya hivi sababu ni niche product, ambayo mkono wa serikali haujafika, ila ukifika nayo itapotea.

Kuna kipindi nchi hii awamu ya 4 mitandao yote walikuwa na unlimited, Tigo walikuwa na vifurushi vya lite, standard na Max unlimited as cheap as 9000 kwa mwezi, Voda walikuwa na Bomba7 na Bomba30, Zantel walikuwa na unlimited 5000 siku 3 etc. Then kukaja vifurushi vya usiku vya bei rahisi unlimited etc.

Sasa hivi mitandao ya simu ndio Ng'ombe anayekamuliwa maziwa, wamenogewa.
 
Kwa inshu hizi to be serious tatizo hasa ni serikali kutaka kunufaika zaidi kwa kile ambacho haikizalishisuala la ubinafshaji kwa njia nyingine ni huu yaanikikisa ubunifu wa namna ya kupata mapato zaidi nalo pia ni janga

Yaanii suala hapa ni kuvuna usichopanda kwa kisingizio tu cha kuwa eti ni serikali
 
Kama umesoma mfumo wa Oligopoly haitakusumbua kuelewa mitandao ya simu inaoperate vipi. Kifupi serikali ndio inahusika na bei za Bando,

Angalia vifurushi ambavyo sio mainstream kama Tigo postpaid, Vodacom Supakasi etc Voda wanatoa Unlimited 5G, nchi chache sana duniani wana huduma kama hii, wameweza kufanya hivi sababu ni niche product, ambayo mkono wa serikali haujafika, ila ukifika nayo itapotea.

Kuna kipindi nchi hii awamu ya 4 mitandao yote walikuwa na unlimited, Tigo walikuwa na vifurushi vya lite, standard na Max unlimited as cheap as 9000 kwa mwezi, Voda walikuwa na Bomba7 na Bomba30, Zantel walikuwa na unlimited 5000 siku 3 etc. Then kukaja vifurushi vya usiku vya bei rahisi unlimited etc.

Sasa hivi mitandao ya simu ndio Ng'ombe anayekamuliwa maziwa, wamenogewa.
Huu ndio uchungu wenyewe sasa yaani ubunifu hamna na huko wanaona pesa ipo

Unanunua kifurushi toka voda serkl wanakata VAT pia wanakata tozo na kodi kutoka voda kwenye muamala huohuo mmoja....ni huzuni
 
Kama umesoma mfumo wa Oligopoly haitakusumbua kuelewa mitandao ya simu inaoperate vipi. Kifupi serikali ndio inahusika na bei za Bando,

Angalia vifurushi ambavyo sio mainstream kama Tigo postpaid, Vodacom Supakasi etc Voda wanatoa Unlimited 5G, nchi chache sana duniani wana huduma kama hii, wameweza kufanya hivi sababu ni niche product, ambayo mkono wa serikali haujafika, ila ukifika nayo itapotea.

Kuna kipindi nchi hii awamu ya 4 mitandao yote walikuwa na unlimited, Tigo walikuwa na vifurushi vya lite, standard na Max unlimited as cheap as 9000 kwa mwezi, Voda walikuwa na Bomba7 na Bomba30, Zantel walikuwa na unlimited 5000 siku 3 etc. Then kukaja vifurushi vya usiku vya bei rahisi unlimited etc.

Sasa hivi mitandao ya simu ndio Ng'ombe anayekamuliwa maziwa, wamenogewa.
Na Bado alisikika Naibu Spika (Zungu) akimwambia Nape akaangalie jinsi gani serikali inaweza kunufaika na Bundle / Data kwamba huko ndio pesa zilipo..., alafu watu badala ya ku-deal na tatizo wapo wanapambana na watu wenye biashara zao kwamba ndio wachawi (ukizingatia hawa watu first and foremost wapo pale kutengeneza faida and are answerable to their shareholders) wale ambao tunawalipa ili watutetee wamegeuka kuwa kupe wa kutunyonya....
 
Tatizo tunatafuta mchawi ambapo hayupo.... Hizi Kampuni zina makosa gani ?

Kampuni hizi kazi yao sio Service (hio ni aftermath) kazi yao first and farmost ni kutengeneza Pesa kwao na Shareholders wao..., kwahio tukadhani kwenye ushindani wakishindana wenyewe kwa wenyewe basi bei zitashuka.... (free market)

Ila ukiangalia Serikali kuna kipindi ilitoa bei elekezi (makampuni yakafuata bundle zote zikafutwa) na bei kupanda maradufu..., kwahio utaona kwamba hizi Kampuni zikifuata kama Serikali inavyotaka huenda kutakuwa hakuna ahueni...

Ila Serikali kama inataka inashindwa nini kuonyesha mfano kwenye Kampuni yao !, Sababu tukianza kuzipangia hizi kampuni huenda zikaacha kuwekeza kama zinavyofanya sasa...,

Pili usitegemee Serikali (inayotaka Mapato) ikushushie bei, bei itashuka tu kulingana na wananchi kuwa na choices zaidi ya moja na sababu katika hizo choices kampuni mojawapo ni ya kwetu (TTCL) kwanini hii isiwe mfano ? Kwanini tusumbuke na hizi Kampuni Binafsi wakati tunayo ya kwetu ya kuipigia kelele ?

By the way TTCL Customer Care inamiundo mbinu kiasi gani kwanini inashindwa kazi ? Huyu Nape kwanini asiwekeze nguvu zake kule na kutengeneza the best model for business huko (Shamba Darasa)..
Mkuu nafahamu kuwa serikali ndio imesababisha hili tatizo, ila binafsi naona sio kila kinachotamkwa na Serikali basi makampuni lazima yafate

Na hapo ndipo napoona ipo haja ya haya makampuni kupokea hizi lawama.

Assume sera kandamizi zingewalenga direct wao bila kupozea maumivu yao kwa kutukandamiza wateja wao unafikiri wasinge chukua hatua yeyote kuhakikisha kuwa hawaumizwi?

Hapa ni kwasababu tunao umia ni sisi, na kupitia maumivu yetu nao wamekuwa wanufaika na ndio maana huwezi kuwaona wakipigania kuondolewa kwa hizi kero.

Ila ingekuwa ni wao ndio wanaumia nadhani hata mgomo ungewekwa
 
Mkuu nafahamu kuwa serikali ndio imesababisha hili tatizo, ila binafsi naona sio kila kinachotamkwa na Serikali basi makampuni lazima yafate

Na hapo ndipo napoona ipo haja ya haya makampuni kupokea hizi lawama.

Assume sera kandamizi zingewalenga direct wao bila kupozea maumivu yao kwa kutukandamiza wateja wao unafikiri wasinge chukua hatua yeyote kuhakikisha kuwa hawaumizwi?

Hapa ni kwasababu tunao umia ni sisi, na kupitia maumivu yetu nao wamekuwa wanufaika na ndio maana huwezi kuwaona wakipigania kuondolewa kwa hizi kero.

Ila ingekuwa ni wao ndio wanaumia nadhani hata mgomo ungewekwa
Hapa kuna mambo mawili moja lazima tukubaliane hizi Kampuni hazipo hapa kutangaza injili au kufanya kazi ya kanisa (yaani kuleta service) hata kwa bahati mbaya wakifanya mazuri ni kutengeneza brand yao kwamba wanajali (yaani ile good image inawaongezea masoko) na hio sio mbaya sababu wapo pale ku-make as much money as possible hio ndio kazi yao...

Sasa Serikali imekuwa ikiwabana sana hawa watu na hapo hawajafunga virago kama kina (UBER) n.k. sababu they are still making a but-load of money kwahio na haya machungu bado profits ni lukuki....

Na Tigo anashusha bei (sio sababu anatupenda sana) HAPANA; sababu Voda ameshusha na yeye asipofanya hivyo watu wataingia mitini na katika hio faida kuna pesa anaingiza katika research and promotion ili aendelee kukaa na wateja wake au kuvuta wengine;

Kwahio Serikali wakipandisha matozo yao wenyewe wanayaleta kwa mteja na sabanu serikali tuseme impandisha mpaka tshs 500 regardless muda au wakati basi wao hawawezi wakaleta offer za tshs 400/= sababu wanajua hata Tigo au yoyote yule hawezi kushusha beyond hiyo 400/= Ofcourse ingekuwa overheads ni kubwa sana na hawapati faida kubwa wangeweza kukaa pamoja na kupanga bei ya kumkomoa mlaji...

Ndio hapo nikasema kweli hawa watu (serikali) wangekuwa na Mwarobaini kwanini huo mwarobaini wasimwenyeshe TTCL ili bei ziwe chini wote tuhamie nyumbani na hao so called matapeli watashusha bei ili tusiende TTCL...

Sisi ndio walaji tunaowaweka kina Voda Mjini hivyo wakiachiwa kweli ushindani na washindane na mmoja wapo wa washindani ni kampuni yetu (TTCL) ambaye hawawezi wakapanga nae matokeo (bei za bundle) watashusha to the minimum.... (sababu huo sio mkate wakipandisha watakula bundle zao wenyewe)
 
Hapa kuna mambo mawili moja lazima tukubaliane hizi Kampuni hazipo hapa kutangaza injili au kufanya kazi ya kanisa (yaani kuleta service) hata kwa bahati mbaya wakifanya mazuri ni kutengeneza brand yao kwamba wanajali (yaani ile good image inawaongezea masoko) na hio sio mbaya sababu wapo pale ku-make as much money as possible hio ndio kazi yao...

Sasa Serikali imekuwa ikiwabana sana hawa watu na hapo hawajafunga virago kama kina (UBER) n.k. sababu they are still making a but-load of money kwahio na haya machungu bado profits ni lukuki....

Na Tigo anashusha bei (sio sababu anatupenda sana) HAPANA; sababu Voda ameshusha na yeye asipofanya hivyo watu wataingia mitini na katika hio faida kuna pesa anaingiza katika research and promotion ili aendelee kukaa na wateja wake au kuvuta wengine;

Kwahio Serikali wakipandisha matozo yao wenyewe wanayaleta kwa mteja na sabanu serikali tuseme impandisha mpaka tshs 500 regardless muda au wakati basi wao hawawezi wakaleta offer za tshs 400/= sababu wanajua hata Tigo au yoyote yule hawezi kushusha beyond hiyo 400/= Ofcourse ingekuwa overheads ni kubwa sana na hawapati faida kubwa wangeweza kukaa pamoja na kupanga bei ya kumkomoa mlaji...

Ndio hapo nikasema kweli hawa watu (serikali) wangekuwa na Mwarobaini kwanini huo mwarobaini wasimwenyeshe TTCL ili bei ziwe chini wote tuhamie nyumbani na hao so called matapeli watashusha bei ili tusiende TTCL...

Sisi ndio walaji tunaowaweka kina Voda Mjini hivyo wakiachiwa kweli ushindani na washindane na mmoja wapo wa washindani ni kampuni yetu (TTCL) ambaye hawawezi wakapanga nae matokeo (bei za bundle) watashusha to the minimum.... (sababu huo sio mkate wakipandisha watakula bundle zao wenyewe)
Mkuu kama makampuni hayako tayari kufanya kazi ya kanisa thats why unaona ni sahihi kwa wao kushirikiana na serikali kufanya unyonyaji ambao wangeweza kupinga, kwanini na serikali usiiangalie kwa jicho hilo hilo kuwa nayo haiwezi kufanya kazi ya kanisa kuhudumia wananchi wake bila kuweka mikakati ya kodi kandamizi?

Kwasababu mwisho wa siku hapo kila mtu anaangalia tumbo lake

Ssa kama tunaweza kuiona serikali ina matatizo kwenye hili basi tusitafute justification kwa hizi kampuni za mawasiliano kuziona kama hazihusiki, ikiwa pale tunapoona nao wanayo nafasi ya kuweza kugomea huu unyonyaji lakini wameamua kula buyu kwasababu nao ni wanufaiki wa ubadhilifu huu.

Kumbuka hoja yangu sio kuitetea serikali katika hili, hoja yangu ni ku-point kila eneo ambalo linahusika kuhalalisha huu utapeli ilihali walikuwa wapo kwenye nafasi ya kupinga uhuni huu na ikawezekana
 
Mkuu kama makampuni hayako tayari kufanya kazi ya kanisa thats why unaona ni sahihi kwa wao kushirikiana na serikali kufanya unyonyaji ambao wangeweza kupinga, kwanini na serikali usiiangalie kwa jicho hilo hilo kuwa nayo haiwezi kufanya kazi ya kanisa kuhudumia wananchi wake bila kuweka mikakati ya kodi kandamizi?
Haya makampuni yana Mungu wawili tu..., Profits na Shareholders ambao nao wanaangalia Profits (Profits at all Costs Kwahio wewe kama CEO unaweza ukadouble the profits aliyepo anakwenda na Maji) kwahio hio ndio kazi ya hizi kampuni...

Kushirikiana na Serikali (AKA kufanya Lobbying) ni moja ya kazi yao; Kwahio hapo mmoja anafanya kazi yake kulainisha njia ili aweze (kutengeneza pesa as much as possible) na mwingine hafanyi kazi yake (kutetea mwananchi kusimama kwa jili ya mwananchi ambaye anamlipa through kodi) ;

Pili hata sera / sheria za Serikali zinawaumiza pia refer TOZO ilivyopelekea wao mapato yao kupungua..., Na unaongelea kupinga ? Ukipinga unaweza kuanzishiwa zengwe (Refer Selcom alivyonyanganywa Tender ya Tanesco) na Maxmalipo kupewa motor vehicle ambayo Selcom halikuwa hana (kwa mgongo wa kampuni ya wazawa).. Kwahio ukijifanya mjanja unaweza kujikuta mwenzako anapewa a dish kwenye silver platter wakati wewe hata makombo haupati (kwahio wanatumia weaknesses za walafi ili waendelee kutafuna (Ingawa siwezi kulaumu hizi kampuni kama vile ambavyo siwezi kumlaumu mbwa kwa kubweka) that's his nature
Kwasababu mwisho wa siku hapo kila mtu anaangalia tumbo lake
Serikali inabidi isiangalie Tumbo lake bali matumbo ya maboss wake ambao ni sisi.., Hawa watendaji tunawalipe ili watufanyie sisi kazi wala sio hisani tofauti na wale wawekezaji walioweka pesa yao ili waweze kupata maradufu..., If they can make 100/= why settle with 50/= (As much profit as possible)
Ssa kama tunaweza kuiona serikali ina matatizo kwenye hili basi tusitafute justification kwa hizi kampuni za mawasiliano kuziona kama hazihusiki, ikiwa pale tunapoona nao wanayo nafasi ya kuweza kugomea huu unyonyaji lakini wameamua kula buyu kwasababu nao ni wanufaiki wa ubadhilifu huu.
Hata wangeweza kupinga baadhi ya haya mambo ambayo wamekuwa wakipinga mfano TOZO ni sababu yanaingilia kwenye faida zao bila haya matozo wala kupangiana na sheria za ajabu ajabu huenda wangetengeneza pesa zaidi..., Ila kumbuka hata watakapopinga ni sababu faida yao imepungua sio sababu sisi tumenyonywa (hawa sio watetezi wetu) ni kwamba sisi ni wateja tu na kama kuna uwezekano wa kutunyonya watafanya hivyo (that's how the beast was built) kwahio kuliko kumwambia mbwa aache kubweka na aanze kuwika ni bora tutafute kuku wetu anayeweza kuwika (TTCL) na kumlaumu pale anapokaa kimya..., sio kuwapangia wengine ambao wapo pale kukusanya pesa na si vinginevyo...,

Pia hawa jamaa unakuta nchi za watu wanaajiri kabisa lobbyists ambao kazi zao ni kutoa mlungula kwa watunga sera ili mirija yao iendelee kufanya yake (Na bora hii kuna Competition ya kuwashika Mashati) kule ambapo watu wanataka TANESCO ibinafsishwe ndio tutapigwa mpaka tushangae...
Kumbuka hoja yangu sio kuitetea serikali katika hili, hoja yangu ni ku-point kila eneo ambalo linahusika kuhalalisha huu utapeli ilihali walikuwa wapo kwenye nafasi ya kupinga uhuni huu na ikawezekana
Alafu tukubaliane Utapeli ni Upi, kama unasema Utapeli ni Bei za Bundle huo sio Utapeli bali ni bei ambayo wamepanga na wewe unaamua kununua au kuacha kabla ya transaction..., unless unanunua ya Tshs 100/= unapewa ya Tshs 50/= ..., Mfano wewe kuliko kulalamika Vitumbua vya Jirani vimechacha na wewe nyumbani una Jiko na mke kwanini usipike vyako vizuri... (Ukizingatia una Jiko zuri kuliko yote Mtaani) na hapa Jiko namaanisha Miundombinu ya TTCL
 
Mchawi hapa ni TCRA yeye ndo amewapangia bei elekezi hizo kampuni ndo maana wote sasa hivi ni MB 490 Kwa tshs 1,000. Na kama pesa serikali inavuna kweli kweli pia sidhani kama watakaa waje washushe gharama wameshaonja asali, tumeona maneno ya kejeli anayo zungumza nape kwenye sakata hili
 
Mchawi hapa ni TCRA yeye ndo amewapangia bei elekezi hizo kampuni ndo maana wote sasa hivi ni MB 490 Kwa tshs 1,000. Na kama pesa serikali inavuna kweli kweli pia sidhani kama watakaa waje washushe gharama wameshaonja asali, tumeona maneno ya kejeli anayo zungumza nape kwenye sakata hili
The greatest trick the Devil ever pulled was convincing the world he didn’t exist. - The Usual Suspects

Na hii Serikali ingawa ndio causative wa haya yote imewa-convice wadau kwamba mbaya wao ni Mitandao na wao ni Watetezi
 
Mchawi hapa ni TCRA yeye ndo amewapangia bei elekezi hizo kampuni ndo maana wote sasa hivi ni MB 490 Kwa tshs 1,000. Na kama pesa serikali inavuna kweli kweli pia sidhani kama watakaa waje washushe gharama wameshaonja asali, tumeona maneno ya kejeli anayo zungumza nape kwenye sakata hili
Mbona alafu hizo mb 490 Za buku sasa hivi zinaisha faster kuliko zilivyokuwa mwaka jana. Uliweza kuingia insta siku nzima Mara mbili tatu na ukaamka Tena ukafanya mambo yako yote mtandaoni mpaka kinaisha mda wake. Sasa hivi ukiweka cha buku unaingia insta dk 2 unaambiwa umetumia 75% hapo umebrowz story mbili tatu……. Huu ni wizi uliopitiliza…..
 
Mbona alafu hizo mb 490 Za buku sasa hivi zinaisha faster kuliko zilivyokuwa mwaka jana. Uliweza kuingia insta siku nzima Mara mbili tatu na ukaamka Tena ukafanya mambo yako yote mtandaoni mpaka kinaisha mda wake. Sasa hivi ukiweka cha buku unaingia insta dk 2 unaambiwa umetumia 75% hapo umebrowz story mbili tatu……. Huu ni wizi uliopitiliza…..
Labda Story unazo-browse zimebadilika ?

Kama ni kweli usemayo huu kweli utakuwa wizi unachouziwa ni tofauti na ulichoambiwa ila suala la watu kuuza vifurushi kwa bei fulani huwezi kuita wizi, bali ndio soko huria lenyewe lilivyo...
 
Wange mlamba chuma tu kpnd kile kanyoshewa bomba na jamaa
Jamaa n hasara ya karne kwa vijana ambao weng wetu kula yetu hutokana na mchango wa internet
 
Back
Top Bottom