martial jb
JF-Expert Member
- Oct 21, 2021
- 863
- 1,462
Habari wakuu,
Ni dhahiri kwa hali ilipofikia inaonyesha fika kuwa Yanga wameamua kutia aibu brand ya klabu na mashabiki wao kuijumla.
Hii ni kuhusiana na sakata la Feitoto
Kila dalili zinaonyesha kuwa Fei haitaki Yanga lakini Yanga wanaonyesha ung'ang'anizi wa hali ya juu kwa mchezaji huyo, jambo linalotafsiriwa kama ni aibu kwa klabu upande wa wadau mbalimbali wa soka.
Tayari taswira inaonyesha kuwa Fei ni mkubwa kuliko Yanga kwa vitendo vinavyoonyeshwa na Yanga. Kutokana na hili hata Mama Fei mwenyewe anashangaa kwa nini Yanga wamekuwa Sikio la kufa kwa mteja wake!.
THIS IS INSANE FOR THE CLUB!
Tukumbuke nyuma kidogo Simba SC ilivyoonyesha hadhi yake mbele ya wachezaji wake mahiri kama Singano Messi na Emmanuel Okwi kudhihilisha ukubwa wa klabu mbele yao.
THIS IS HOW MUST BE!
Okay tuachane na hayo tuje kwenye ukweli sasa, Kama Yanga wanatambua mchango wa Fei kwenye klabu yao, kwa nini wasitimize au kumpatia stahiki zake ikiwemo na vigezo vyake anavyohitaji!?
Karibu Tanzania nzima inafahamu ni jinsi gani Feisal Maestro alivyoipenda sana Yanga, kiasi cha dhahiri kudhihilisha kuwa Yanga ndio waliomkosea kijana wao kwani si rahisi Feisal kuibadilika Yanga kufikia hatua hiyo.
Ikumbukwe mchezo huu mchafu haujaanza leo kwa klabu ya Yanga kutaka kudhulumu stahiki za wachezaji wake, na mara kadhaa kesi hizi zimepelekwa TFF na ngazi zingine za juu, endapo ukiangazia sakata la Kakolanya na Morrison.
Itoshe kusema dharau kwa wachezaji wa ndani zikome kwani kinachoangaliwa ni kiwango na si utaifa. Pili, Yanga ijitathmini maana kuhonga kwenye ngazi za Uongozi haiwezi tosha mbele ya haki ya mtu!.
Naomba wachezaji mjifunze kwa hili ambalo YANGA wanafanya kwa wachezaji wa ndani. Kwa kweli inasikitisha sana.
Ni dhahiri kwa hali ilipofikia inaonyesha fika kuwa Yanga wameamua kutia aibu brand ya klabu na mashabiki wao kuijumla.
Hii ni kuhusiana na sakata la Feitoto
Kila dalili zinaonyesha kuwa Fei haitaki Yanga lakini Yanga wanaonyesha ung'ang'anizi wa hali ya juu kwa mchezaji huyo, jambo linalotafsiriwa kama ni aibu kwa klabu upande wa wadau mbalimbali wa soka.
Tayari taswira inaonyesha kuwa Fei ni mkubwa kuliko Yanga kwa vitendo vinavyoonyeshwa na Yanga. Kutokana na hili hata Mama Fei mwenyewe anashangaa kwa nini Yanga wamekuwa Sikio la kufa kwa mteja wake!.
THIS IS INSANE FOR THE CLUB!
Tukumbuke nyuma kidogo Simba SC ilivyoonyesha hadhi yake mbele ya wachezaji wake mahiri kama Singano Messi na Emmanuel Okwi kudhihilisha ukubwa wa klabu mbele yao.
THIS IS HOW MUST BE!
Okay tuachane na hayo tuje kwenye ukweli sasa, Kama Yanga wanatambua mchango wa Fei kwenye klabu yao, kwa nini wasitimize au kumpatia stahiki zake ikiwemo na vigezo vyake anavyohitaji!?
Karibu Tanzania nzima inafahamu ni jinsi gani Feisal Maestro alivyoipenda sana Yanga, kiasi cha dhahiri kudhihilisha kuwa Yanga ndio waliomkosea kijana wao kwani si rahisi Feisal kuibadilika Yanga kufikia hatua hiyo.
Ikumbukwe mchezo huu mchafu haujaanza leo kwa klabu ya Yanga kutaka kudhulumu stahiki za wachezaji wake, na mara kadhaa kesi hizi zimepelekwa TFF na ngazi zingine za juu, endapo ukiangazia sakata la Kakolanya na Morrison.
Itoshe kusema dharau kwa wachezaji wa ndani zikome kwani kinachoangaliwa ni kiwango na si utaifa. Pili, Yanga ijitathmini maana kuhonga kwenye ngazi za Uongozi haiwezi tosha mbele ya haki ya mtu!.
Naomba wachezaji mjifunze kwa hili ambalo YANGA wanafanya kwa wachezaji wa ndani. Kwa kweli inasikitisha sana.