Sakata la Green City Morogoro: Shule nyingine zimulikwe pia

Sakata la Green City Morogoro: Shule nyingine zimulikwe pia

ibanezafrica

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2014
Posts
7,261
Reaction score
6,553
Kitendo cha kinyama kilichofanywa na mwalimu/meneja wa shule ya Green City la kumpiga mwanafunzi hadi kupoteza fahamu kwa masaa karibu 20 eti kisa kachelewa masaa machache kuripoti shule Jumapili ni kitendo kinachopaswa kulaaniwa na serikali inabidi ifanye uchunguzi wa shule nyingine zenye tabia za namna hiyo.

Wazazi tujitokeze na kuzianika shule za namna hii zenye adhabu zinazopitiliza ili wajirekebishe au serikali izimulike.

Korogwe girls inasemekana adhabu zilizopitiliza pale napo zimekithiri, wanafunzi wanalimishwa, wanachimbishwa mashimo makubwa kama adhabu, hali inayopelekea hata ufanisi wa watoto kushuka shule sasa inathamini hizo kazi/adhabu, shule ina maekari ya mashamba yanayotegemewa kulimwa na wanafunzi wenyewe kwa kigezo cha adhabu.

Nimeridhishwa na hatua zilizochukuliwa na serikali ya mkoa wa morogoro kumsimamisha kazi meneja wa shule na kumkabidhi kwa jeshi la polisi.

Jamani shule zenye tabia hizi tuziseme hapa serikali ifuatilie, watoto wetu wanateseka.
 
Waalimu kama hawa dawa Yao unampeleka SUMBAWANGA Huko akafundishe atakutana na wachawi wanasoma na NYUNGO zao kwenye mabegi
 
Kitendo cha kinyama kilichofanywa na mwalimu/ meneja wa shule ya green city la kumpiga mwanafunzi hadi kupoteza fahamu kwa masaa karibu...
Pia Bwiru girls watoto wa kike wanapewa adhabu kali sana ikiwemo kuchumba na kuhamisha mawe makubwa sana. Hali inayopelekea rushwa ya ngono kwa wahusika kutafuta unafuu
 
Hivi walimu hawajaacha ukatili tu?!!dahh
Waalimu waache ukatili, tulikuwa na mwalimu anaitwa Joseph, snatembea na fimbo ameiandika nitakuchana mboko,na akichana mboko kweli wanafunzi,na adhabu za kutembea kwa kifua kwenye kokoto.

Huyo mwalimu, alikuwa na afya na mrefu.

Waalimu acheni ukatili, wanafunzi wanachangamoto nyingi za kimaisha, hasa wanafunzi wa kike.
 
Paduca hills pia, mtoto anachelewa kufika shule siku ya kuripoti huenda amepata adha barabarani au anatokea mbali mfano kagera huko lakini akifika shule siku hiyo anapewa adhabu ya kubeba vifusi ndoo 200.

Walimu hawaangalii mtoto amechelewa kuripoti kwa sababu gani kama ni amepata changamoto au ni uzembe wote wanawekwa kwenye kundi moja, inasikitisha.
 
Pia Bwiru girls watoto wa kike wanapewa adhabu kali sana ikiwemo kuchumba na kuhamisha mawe makubwa sana. Hali inayopelekea rushwa ya ngono kwa wahusika kutafuta unafuu
Jambo hili lifuatiliwe ma wakuu wa elimu mwanza inuma sana...jamani tuzitaje shule hizi
 
Paduca hills pia, mtoto anachelewa kufika shule siku ya kuripoti huenda amepata adha barabarani au anatokea mbali mfano kagera huko lakini akifika shule siku hiyo anapewa adhabu ya kubeba vifusi ndoo 200.

Walimu hawaangalii mtoto amechelewa kuripoti kwa sababu gani kama ni amepata changamoto au ni uzembe wote wanawekwa kwenye kundi moja, inasikitisha.
Hii ipo wapi?kwakweli serikali za mikoa ziunde tume kuzifuatilia shule zote lalamikiwa
 
Korogwe girls inasemekana adhabu zilizopitiliza pale napo zimekithiri, wanafunzi wanalimishwa, wanachimbishwa mashimo makubwa kama adhabu, hali inayopelekea hata ufanisi wa watoto kushuka shule sasa inathamini hizo kazi/adhabu, shule ina maekari ya mashamba yanayotegemewa kulimwa na wanafunzi wenyewe kwa kigezo cha adhabu.
Ukiuliza walimu wanakuambia na wao walishurutishwa hivyohivyo
 
Tofauti kati ya Gereza na Shule kwa nchi yetu ni ndogo sana. Sijui nani aliwaambia Walimu kuchapa fimbo ndio kufundisha. Utumwa tu aliyeanzisha hii adhabu sijui nani.
 
Tofauti kati ya Gereza na Shule kwa nchi yetu ni ndogo sana. Sijui nani aliwaambia Walimu kuchapa fimbo ndio kufundisha. Utumwa tu aliyeanzisha hii adhabu sijui nani.
Tulishatoa ushauri fimbo zipigwe marufuku coz zinadhalilisha utu wa mwanafunzi na kumfanya aloose confidence maisha yake yote lkn wadau wanadai bila fimbo watoto watakuwa mashoga.
 
serikali inabidi ifanye uchunguzi wa shule nyingine zenye tabia za namna hiyo.
Hapa usitafute mchawi, mchawi ni Serikali yenyewe: wanakubali vipi shule kuongozwa na asiye na haiba au malezi ya kimalezi ya elimu?. Uliona wapi hospitali inasimamiwa na asiye na akisi ya tiba/afya, angalia hata makanisa yanayoongozwa na wasio na haiba ya theologia wanaishia kuomba waumini wawapelekee kucha, nywele na mavuzi: hujashtuka tu?
 
Huyo mwalimu kama mimi ndio mzazi na kikundi cha kutatua matatizo ya mtaro na maji machafu.nazani asinge simulia kwa nini manaspaa ya uchafu imemfanyia hivo
 
Back
Top Bottom