poposindege
JF-Expert Member
- Nov 22, 2010
- 453
- 175
Chama cha mpira wa miguu Tanzania TFF kimemfungia Mchezaji Pius Buswita kwa kosa la kusajili timu mbili za Yanga na Simba.
Ambako kwa sheria za TFF mchezaji atakayekutwa na kosa hilo atafungiwa mwaka mmoja.
Kuna maswali yanahitaji majibu.
1- Je mchezaji huyo alisaini fomu za usajili za Klabu ya Yanga na Simba ambazo zimetoka TFF?
2- Katika orodha ya wachezaji wa Yanga iliyopelekwa TFF jina la Pius Buswita lipo, Mbona orodha ya wachezaji wa Simba iliyopelekwa TFF halipo(Kama kweli amesajili simba)?
3- Kwanini Simba hawakuweka jina lake kama mmoja wa wachezaji waliomsajili?
5- Kwa nini TFF wamfungie mchezaji aliyesajili timu moja, kwa kosa la kusajili timu mbili?
6- Je TFF wana ushahidi gani au wametumia upi, kwamba mchezaji huyo amesajili timu mbili ili hali timu ya Simba hayupo kwenye orodha yao iliyopelekwa TFF?
Ukweli kinachoonekana Pius Buswita amechukua pesa za Simba kwa ajili ya makubaliano ya kusajili timu hiyo. Ila ukweli hakusajili. Kinachotakiwa Mchezaji huyo alipe alichochukua kwa timu ya simba na si kufungiwa kucheza mpira.
Ni sawa na mchezaji kufanya kosa nje ya uwanja (Mfano kupigana Disco au kumtukana mkewe) basi iwe sababu ya kufungiwa kucheza mpira kwa muda wa mwaka mmoja.
Kwa mwanzo huu wa TFF mpya ya kuanza kutoa adhabu kiuonevu na baada ya raundi ya kwanza ya ligi tayari ratiba ishaanza kusogezwa mbele, muda si mrefu tutaona uongozi wa Malinzi (ambao ni mbovu) ulikuwa na afadhali.
Ambako kwa sheria za TFF mchezaji atakayekutwa na kosa hilo atafungiwa mwaka mmoja.
Kuna maswali yanahitaji majibu.
1- Je mchezaji huyo alisaini fomu za usajili za Klabu ya Yanga na Simba ambazo zimetoka TFF?
2- Katika orodha ya wachezaji wa Yanga iliyopelekwa TFF jina la Pius Buswita lipo, Mbona orodha ya wachezaji wa Simba iliyopelekwa TFF halipo(Kama kweli amesajili simba)?
3- Kwanini Simba hawakuweka jina lake kama mmoja wa wachezaji waliomsajili?
5- Kwa nini TFF wamfungie mchezaji aliyesajili timu moja, kwa kosa la kusajili timu mbili?
6- Je TFF wana ushahidi gani au wametumia upi, kwamba mchezaji huyo amesajili timu mbili ili hali timu ya Simba hayupo kwenye orodha yao iliyopelekwa TFF?
Ukweli kinachoonekana Pius Buswita amechukua pesa za Simba kwa ajili ya makubaliano ya kusajili timu hiyo. Ila ukweli hakusajili. Kinachotakiwa Mchezaji huyo alipe alichochukua kwa timu ya simba na si kufungiwa kucheza mpira.
Ni sawa na mchezaji kufanya kosa nje ya uwanja (Mfano kupigana Disco au kumtukana mkewe) basi iwe sababu ya kufungiwa kucheza mpira kwa muda wa mwaka mmoja.
Kwa mwanzo huu wa TFF mpya ya kuanza kutoa adhabu kiuonevu na baada ya raundi ya kwanza ya ligi tayari ratiba ishaanza kusogezwa mbele, muda si mrefu tutaona uongozi wa Malinzi (ambao ni mbovu) ulikuwa na afadhali.