Sakata la mchezaji Hassan Kessy, Simba wako sahihi

Hukumu haijasema Kessy kavunja mkataba Simba, wala haikusema kwamba Yanga imemsajili wakati ana mkataba na Simba. Ilichosema ni kwamba Yanga imepeleka jina la Kessy CAF wakati bado ni mchezaji wa Simba. Ni kosa la utovu wa nidhamu, si la usajili haramu. Asingeweza kusajiliwa kwa ajili ya Ligi kwa kuwa Dirisha Dogo lilishafungwa kitambo. Na bila ya kusajiliwa Ligi ya Ndani asingeweza kusajiliwa Ligi ya CAF. Kilichofanywa ni kuwasilishwa jina lake CAF ili liwahi mfunda (deadline) wa kutumia majina huku usajili ukiendelea. Fundisho hapa siyo kwa wachezaji tu bali hata kwa viongozi wanaoendesha timu kwa hadaa, chuki, tamaa na mazowea.
 
Simba please msikubali hiyo pesa ni ndogo sana Yanga ili iwe fundisho kwao inabidi wapigwe faini ya hela ndefu isiyopungua milioni 200
 
Kikombe hiki hakiwezi kuwaepuka TFF ndo chanzo cha ubabaishaji
 
Fomu za usajili zinapotumwa CAF hapo ndipo leseni hutumwa na sharti ni kwamba mchezaji awe amesajiliwa kwa ligi ya ndani. Kutumwa jina la Kessy ni hadaa dhidi ya CAF kwa kushirikiana na kiongozi mojawapo wa TFF. Simba walipokomaa ndipo TFF wakajaribu kila njia kuzima soo. Jitihada ya mwisho katika kutapatapa ni kudai Simba hawajamlipa Kessy mishahara 3 ya mwisho wa mkataba.Simba walipopeleka risiti za mishahara ndipo ikabidi wajaribu ku minimize damage kwa kutoa hii hukumu. Simba wana ushahidi mzuri wa kukomaa na Kessy ili iwe fundisho kwa wachezaji na viongozi waliozoea kubebwa na maamuzi ya kibabaishaji.
 
Ni rahisi Ngamia kupita Tundu la sindano kuliko hilo unaloliota kutekelezwa.... [emoji23]
 
tutawapa 50 watoto wazuri kama haitoshi semeni tutawaongeza,mnataka hii 50 tuwape lini?
Unavyoreply kwa mbwembwe kamanuna hela, au wewe ndio utakezilipa. Kumbe mifukoni kwako vumbi tu!!
 
Tatizo lako unafikiri CAF na FIFA wapo wababaishaji kama hao wanaowabeba kila mwaka. Simba walikomaa na suala la Bokungu ikabidi TP Mazembe wafungiwe kushiriki mwaka 1 mashindano ya CAF na kutupwa nje ya mashindano licha ya kuitoa Simba. Kaa mkao wa kula .
 
Adhabu ndogo sana Simba watumie haya maamuzi kufungua kesi ya madai. Vipi kuhusu mechi alizocheza Kessy itakuwaje?
Kumruhusu Kessy kucheza ilikuwa kulinda kiwango chake kisipotee, mi sioni kama kuna tatizo hapo.
 
Cha mijinga huliwa na mjanja. Mlijitia wajuaji. Mngeandika barua tu ya kuomba kuidhinishiwa. Siku 5 za mkataba zimezaa milioni 50.Mhindi sidhani kama atakubali kulipa kirahisi.Lazima vichwa vita roll kwa ujinga huu.
[emoji12] [emoji12] [emoji12] [emoji12] [emoji12] [emoji12] [emoji12] [emoji12] [emoji12]
 
Ngoma bado. Simba sio wajinga tusubiri tuone, kibaya zaidi naye Kessy alipohamia Yanga ni kama alizidisha mbwembwe na tambo km ndo kafiiiika. Mmmh
 
Kama ni FIFA nadhani wanasheria wa Simba wako vizuri...tusubiri
 

Kessy kama angecheza zile mechi za Kombe la Shirikisho Africa ndio wangeweza kuporwa point kipindi hicho Kessy hakuwa na leseni ya Yanga alikuwa na ya Simba na kipindi cha usajili wa ndani kilikuwa kimepita hizi za kucheza ligi ya VPL msimu huu mkataba wa kesi uliishaisha but madai ya msingi Simba walipaswa kulipwa na Yanga gharama za kufunja mkataba wa Kessy ndio maana Simba wakadai walipwe bilioni 1
 
Akili zimekurudia. Post zako za nyuma ulidai Simba haina madai ya msingi. Mchezo ndio umeanza Simba wanadai bilioni 1.2 za Yanga kutuma jina la mchezaji waliyekuwa na mkataba naye .Milioni 50 ni uamuzi wa TFF. Hii ngoma bado mbichi sana. Itabidi CAF na FIFA wahusike.
 

Wachezaji wote wa Simba hawafiki thamani ya 1.2 bilioni,mlidai fidia kuanzia Yondani,Twite,Okwi,Singano zote ziliota mbawa endelea kuota
 
Hapo ngoma ndio kwanza imeisha kutengenezwa bado kuchezwa, mbichiiiii....bado madai ya Simba FIFA au CAF ...labda Kessy awafuate Simba kuomba msamaha kimya kimya. Hizo bilioni moja wanazodai Simba watapata tu wakikomaa njia iko wazi sasa.
 
Wachezaji wote wa Simba hawafiki thamani ya 1.2 bilioni,mlidai fidia kuanzia Yondani,Twite,Okwi,Singano zote ziliota mbawa endelea kuota
Nadhani wewe ni mtupu kwenye masuala ya mkataba. Unapokwenda sign mkataba kuna vipengele mbalimbali. Sasa katika kipengele cha mkataba wa Kessy kuna sehemu inasema atayevunja mkataba atalipa dola za kimarekani laki 6.Haijalishi thamani ya mchezaji.
 
Nadhani wewe ni mtupu kwenye masuala ya mkataba. Unapokwenda sign mkataba kuna vipengele mbalimbali. Sasa katika kipengele cha mkataba wa Kessy kuna sehemu inasema atayevunja mkataba atalipa dola za kimarekani laki 6.Haijalishi thamani ya mchezaji.

Unaishi nchi gani ndugu yangu hivyo vipengele vipo na kila mwaka wachezaji wanavunja hiyo mikataba nani aliwahi kulipa hiyo bilioni?

Nakupa mfano wa Singano,Yondani,Ngasa hii yote mikataba ilivunjwa
 
Singano ni kosa la Simba kutotimiza masharti ya mkataba ya kumlipia pango. Yondani na Ngassa hawakuwa na vipengele vya aina hiyo. Wacha kutoa mifano mfu. Ukivunja mkataba upande uliovunja mkataba upo liable kulipa fidia kutokana na masharti ya mkataba.
 
Kessy alilipiwa pango,au hakukuwa na hicho kipengele?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…