Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,468
- 911,184
Katika mahujiano ya jana kwenye Radio One kipindi cha michezo usiku khoja za Wambura zilirejewa na kuungwa mkono na baadhi ya watangazaji na wasikilizaji wakati ni hoja zinazokinzana na sheria za FIFA
!
Mgogoro wa uongozi ndani ya TFF unahusu sifa za baadhi ya wagombea akiwemo Wambura ambaye amekuwa akienguliwa kila mara kwa sababu zilezile na hivyo kimsingi kuwa ameonewa. Huwezi kumwadhibu mtu mara mbili kwa kosa lilelile kwa kufanya hivyo ni kuwa hujamsamehe na adhabu yenyewe inaonekana haina mipaka na hivyo kutokubalika. TFF inabidi watafute sababu nyingine mbali ya zile ambazo wamekuwa wakizitumia kumzuia Wambura kushiriki kwenye uchaguzi huo.
Kuhusu Malinzi kuzuia ni kichekesho kabisa kwa sababu uongozi ndani ya mpira ni madraka tu au hata ushiriki pia? Hivi mchezaji wa mpira hawezi kugombea wadhifa ndani ya TFF mpaka kwanza aliwahi kuwa na wadhifa kwenye kilabu kama siyo uendawazimu hivi ni nini?
Zipo sababu za kimsingi za kuhoji maamuzi ya TFF na hata taratibu zao za kukata rufani kama kweli zimezingatia haki za ubinadamu na hayo ni maeneo ambayo kamati ya FIFA itakapokuja inafaa kuyanyoosha.
Wambura na wenzie wanakosea kudai ya kuwa serikali ina ubavu ndani ya TFFhiyo mitazamo inampunguzia sifa ya kulisimamia kabumbu letu. Sheria za FIFA ziko wazi kwenye hilo na hata hivi sasa FIFA imewaandikia DRC kuwa waache kuingilia utawala wa chama cha mpia cha kwao au hata maombi yao ya kuchezesha soka mwaka 2014 huenda yasifikiriwe kama hawatajirekebisha. Barua hiyo kaandikiwa waziri mkuu wao kujibu maombi tajwa.
Kwenye suala la uhuru wa vyama vya mpira kujiendesha FIFA haina cha ubabaishaji hapo ila kusimamia kabisa sasa huyu Wambura anafikiri sisi hatujui hilo?
Wambura pia anatupotosha sana pale anaposema Tenga muda wake umekwisha na kwa hiyo hana mamlaka ya kisheria ya kusimamia uchaguzi ujao. Hivi haya ameyatoa wapi? Na hili anafikia mahali anajichanganya kwa Wambura kudai Tenga atakeleze maamuzi ya serikali sasa atayatekelezaje kama yeye hana nguvu ya kisheria kuusimamia uchaguzi husika?
Nionavyo Wambura khoja zake ni zenye kukithiri na ubinafsi sana na lolote lile litakafanikisha azma yake ya kutwaa uongozi ndani ya TFF atalikumbatia na anonekana anaichukulia TFF kama sehemu ya ajira hivi wakati ni kujitolea tu.
Tenga yuko sahihi kupinga serikali kujiingiza katika uendeshaji wa TFF na huo ndiyo msimamo wa FIFA na Wambura aache kuwapotosha wadau wa soka.
Jingine ni kuwa baadhi ya waathirika wa maamuzi ya TFF wamekimbilia mahakamani kwa kutumia vikaragosi wao ili kushinikiza kupata ugali wao. Hawa wachunguzwe na ushahidi ukipatikana wazuiwe kugombea nafasi zozote zile ndani ya TFF kwa sababu nilizozitaja awali.
Vilevile, mahakama zetu ni pofu yawaje zikaribishe migogoro ya TFF wakati kanuni zake za uendeshaji zinakataza migogoro yake kutatuliwa na mahakama kulingana na maelekezo ya FIFA?
Kuhusu marekebisho ya katiba ya TFF ya mwaka 2006 ni dhahiri serikali inajikaanga kwneye mafuta yake yenyewe kwa sababu markebisho tajwa yawe mazuri au la serikali iliyasajali na kuwa sheria sasa yawaje leo iyafute kama siyo kuingilia utendaji ndani ya TFF. Mamlaka ya serikali kufuta sheria halali za TFF inayatoa wapi kama siyo kujaribu kuwatungia sheria zake yenyewe?
!
Mgogoro wa uongozi ndani ya TFF unahusu sifa za baadhi ya wagombea akiwemo Wambura ambaye amekuwa akienguliwa kila mara kwa sababu zilezile na hivyo kimsingi kuwa ameonewa. Huwezi kumwadhibu mtu mara mbili kwa kosa lilelile kwa kufanya hivyo ni kuwa hujamsamehe na adhabu yenyewe inaonekana haina mipaka na hivyo kutokubalika. TFF inabidi watafute sababu nyingine mbali ya zile ambazo wamekuwa wakizitumia kumzuia Wambura kushiriki kwenye uchaguzi huo.
Kuhusu Malinzi kuzuia ni kichekesho kabisa kwa sababu uongozi ndani ya mpira ni madraka tu au hata ushiriki pia? Hivi mchezaji wa mpira hawezi kugombea wadhifa ndani ya TFF mpaka kwanza aliwahi kuwa na wadhifa kwenye kilabu kama siyo uendawazimu hivi ni nini?
Zipo sababu za kimsingi za kuhoji maamuzi ya TFF na hata taratibu zao za kukata rufani kama kweli zimezingatia haki za ubinadamu na hayo ni maeneo ambayo kamati ya FIFA itakapokuja inafaa kuyanyoosha.
Wambura na wenzie wanakosea kudai ya kuwa serikali ina ubavu ndani ya TFFhiyo mitazamo inampunguzia sifa ya kulisimamia kabumbu letu. Sheria za FIFA ziko wazi kwenye hilo na hata hivi sasa FIFA imewaandikia DRC kuwa waache kuingilia utawala wa chama cha mpia cha kwao au hata maombi yao ya kuchezesha soka mwaka 2014 huenda yasifikiriwe kama hawatajirekebisha. Barua hiyo kaandikiwa waziri mkuu wao kujibu maombi tajwa.
Kwenye suala la uhuru wa vyama vya mpira kujiendesha FIFA haina cha ubabaishaji hapo ila kusimamia kabisa sasa huyu Wambura anafikiri sisi hatujui hilo?
Wambura pia anatupotosha sana pale anaposema Tenga muda wake umekwisha na kwa hiyo hana mamlaka ya kisheria ya kusimamia uchaguzi ujao. Hivi haya ameyatoa wapi? Na hili anafikia mahali anajichanganya kwa Wambura kudai Tenga atakeleze maamuzi ya serikali sasa atayatekelezaje kama yeye hana nguvu ya kisheria kuusimamia uchaguzi husika?
Nionavyo Wambura khoja zake ni zenye kukithiri na ubinafsi sana na lolote lile litakafanikisha azma yake ya kutwaa uongozi ndani ya TFF atalikumbatia na anonekana anaichukulia TFF kama sehemu ya ajira hivi wakati ni kujitolea tu.
Tenga yuko sahihi kupinga serikali kujiingiza katika uendeshaji wa TFF na huo ndiyo msimamo wa FIFA na Wambura aache kuwapotosha wadau wa soka.
Jingine ni kuwa baadhi ya waathirika wa maamuzi ya TFF wamekimbilia mahakamani kwa kutumia vikaragosi wao ili kushinikiza kupata ugali wao. Hawa wachunguzwe na ushahidi ukipatikana wazuiwe kugombea nafasi zozote zile ndani ya TFF kwa sababu nilizozitaja awali.
Vilevile, mahakama zetu ni pofu yawaje zikaribishe migogoro ya TFF wakati kanuni zake za uendeshaji zinakataza migogoro yake kutatuliwa na mahakama kulingana na maelekezo ya FIFA?
Kuhusu marekebisho ya katiba ya TFF ya mwaka 2006 ni dhahiri serikali inajikaanga kwneye mafuta yake yenyewe kwa sababu markebisho tajwa yawe mazuri au la serikali iliyasajali na kuwa sheria sasa yawaje leo iyafute kama siyo kuingilia utendaji ndani ya TFF. Mamlaka ya serikali kufuta sheria halali za TFF inayatoa wapi kama siyo kujaribu kuwatungia sheria zake yenyewe?