Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
Makala yangu ya Mfungo wa Ramadhani inaelekea imependwa na wengi.
Jamaa wamenifata pembeni kutaka kunijua zaidi.
Jambo hili limenifanya nifikirie makala nyingine yenye mwelekeo huo huo.
Nitarejea In Shaa Allah lakini nakuacha na picha ya Msikiti wa Geneva na Msikiti wa Humburg ambako nilisali sala ya Ijumaa mwaka wa 2011.
Huu msikiti wa Humburg unaitwa Masjid Al Nour sawa na jina la msikiti wa mtaani kwangu Magomeni Mapipa.
Nimeupenda msikiti huu kwa hili jina.
Sala yangu ya kwanza ya Ijumaa kusali nje ya Tanzania nilisali msikiti wa Montaza Palace, Alexandria, Misri mwaka wa 1988.
Huu ni msikiti ni mzuri wa sifa.
Montaza Palace wakati wa Mfalme Farouk ilikuwa kasri ya mfalme akija kupumzika wakati wa kiangazi.
Msikiti huu ukajengwa katika makazi ya Mfalme Farouk.
Baada ya mapinduzi ya mwaka 1952 Montaza Palace ikiwa nyumba ya wananchi wa Misri.
Niliijua nyumba hii miaka mingi nyuma nilipoisoma kwenye kitabu cha Mohamed Heykal, "The Road to Ramadan," kitabu alichoandika kuhusu Vita Vya Yom Kippur vya 1973 kati ya Misri na Israel.
Katika kitabu hicho kuna sehemu Heykal anaeleza vituko vya Anwar Sadat alipomfuata kutoka Cairo kuja Montaza Palace Alexandria kupata kauli yake jinsi vita vilivyokuwa vinaendelea.
Nilipokwenda Cairo nikasali Ijumaa msikiti mmoja uko katikati ya mji jirani ni ilipo Egyptian Museum.
Ninachokumbuka msikiti huu ni kuwa sikuweza kuingia ndani msikitini kwa kuwa msikiti umejaa hadi nje watu wengi wako wengi nje barabarani.
Sifa kubwa ya mji wa Cairo ni wingi wa watu na wingi wa magari barabarani Waingereza wanaita, "bumper to bumper," na madereva wanashindana kupiga honi.
Mwaka uliofuatia nikaenda Sudan nikasali Sala ya Ijumaa msikiti wa Chuo Kikuu Cha Khartoum mwaka wa 1989.
Nilifika Sudan miezi michache baada ya Omar Bashir kupindua serikali na kutwaa madaraka.
Picha iko hapo chini utaitambua kwa kanzu na vilemba vya Kisudani.
Mwaka wa 1991 nimesali msikiti mkuu wa Glasgow, Scotland.
Katika misikiti niliyopata kusali sijapata kusali msikiti nikawa mimi ndiyo mtu mweusi peke yangu ndani ya msikiti kiasi watu wote ndani ya msikiti wananishangaa.
Naingia msikiti macho yote yako kwangu.
Nasali, ''tahiyatu masjid,'' yaani sala ya kuuamkia msikiti, macho yote ndani ya msikiti yako kwangu.
Jambo hili lilinifanya nijisikie vibaya.
Baada ya sala nimeingia kwenye duka la vitabu la msikiti.
Ndugu zangu Waislam wakanifuata kunisalimia na wakawa wananiuliza maswali.
Walitaka kujua wapi natoka na lini nimeingia Uislam?
Hawajui kuwa mimi ni mjukuu wa Sheikh Muhammad Mvamila.
Hawa ndugu zangu hawaijui Tanzania wala hawajapata kuisikia.
Nilipowaeleza kuwa nimezaliwa Muislam wakataka kujua Uislam umeingia lini Tanzania.
Walishangaa sana nilipowaeleza kuwa Uislam upo kwetu miaka 1000.
Nimesali Ijumaa Edinburgh.
Nilikwenda Edinburgh kwanza kuona Edinburgh Castle na kukitembelea chuo alichosoma Mwalimu Nyerere.
Edinburgh Castle ni sehemu inatembelewa sana na watalii na ni majumba mengi kwenye mlima mkubwa.
Hii mijumba ya kale iko hapo karne kwa karne.
Sehemu hii ilinikumbusha Macbeth wa William Shakespeare.
Niliyoshuhudia msikiti wa Glasgow sikuyaona Edinburgh hapo niliwakuta watu weusi wengi wao wakiwa wanafunzi kutoka Afrika.
Nimesali Ijumaa Msikiti wa Makka na Madina mwaka wa 1997, 1998 na 2014.
Mwaka wa 1997 nilikwena Umra na 1998 na 2014 nilikwenda Hijja.
Hijja ya 2014 nilipata mwaliko kutoka kwa Mfalme wa Saudia.
Waalikwa tulikuwa wengi kutoka Tanzania na kwengine ulimwenguni.
Picha hiyo hapo chini nimeupiga Masjid Badawy, Msikiti wa Mtume SAW kutoka dirisha la chumba cha hoteli niliyofikia 2014.
Nilinunua camera si mbali na Msikiti wa Mtume na nikajiambia kuwa picha yangu ya kwanza kupiga uwe Msikiti wa Mtume.
Hili nikalifanya.
Nimesali Ijumaa Tehran pamoja na Rais wa Iran Ahmed Najad mwaka wa 2007.
Nimesali Ijumaa Grande Mosque, yaani Msikiti Mkuu, Paris 2011.
Huu nidyo msikiti mkubwa Paris na Imam Mkuu ni Mngazija.
Hiyo picha hapo chini nimepiga na jamaa wa Kingazija nje ya msikiti.
Kulia kwenye picha ni rafiki yangu marehemu Salim Himid.
Nimesali Ijumaa New York mwaka wa 2011 kwenye kijimsikiti kidogo Manhattan, New York.
Msikiti huu nilikuta jamaa ndogo katika Sala ya Ijumaa si kama jamii nilizopata kuona kwengineko duniani.
Nje ya msikiti kuna askari wanafanya doria kulinda msikiti na wanaosali hapo.
Nimesali Ijumaa Istanbul mwaka wa 2015.
Takriban msikiti mzima watu wamepiga suti.
Sijui kama ni kawaida kuvaa suti au kwa sababu ulikuwa wakati wa baridi.
Nimesali Ijumaa Dubai Rashidiyya mwaka wa 2016.
Hii ni sehemu ambayo Wazanzibar waliotafuta hifadhi Dubai baada ya mapinduzi walipewa makazi hapo na kujengewa nyumba na Sheikh Rashid kiongozi wa Dubai.
Sala ya Ijumaa Msikiti wa Rashidiyya utasema uko Masjid Jibril Zanzibar,
Jamaa wamenifata pembeni kutaka kunijua zaidi.
Jambo hili limenifanya nifikirie makala nyingine yenye mwelekeo huo huo.
Nitarejea In Shaa Allah lakini nakuacha na picha ya Msikiti wa Geneva na Msikiti wa Humburg ambako nilisali sala ya Ijumaa mwaka wa 2011.
Huu msikiti wa Humburg unaitwa Masjid Al Nour sawa na jina la msikiti wa mtaani kwangu Magomeni Mapipa.
Nimeupenda msikiti huu kwa hili jina.
Sala yangu ya kwanza ya Ijumaa kusali nje ya Tanzania nilisali msikiti wa Montaza Palace, Alexandria, Misri mwaka wa 1988.
Huu ni msikiti ni mzuri wa sifa.
Montaza Palace wakati wa Mfalme Farouk ilikuwa kasri ya mfalme akija kupumzika wakati wa kiangazi.
Msikiti huu ukajengwa katika makazi ya Mfalme Farouk.
Baada ya mapinduzi ya mwaka 1952 Montaza Palace ikiwa nyumba ya wananchi wa Misri.
Niliijua nyumba hii miaka mingi nyuma nilipoisoma kwenye kitabu cha Mohamed Heykal, "The Road to Ramadan," kitabu alichoandika kuhusu Vita Vya Yom Kippur vya 1973 kati ya Misri na Israel.
Katika kitabu hicho kuna sehemu Heykal anaeleza vituko vya Anwar Sadat alipomfuata kutoka Cairo kuja Montaza Palace Alexandria kupata kauli yake jinsi vita vilivyokuwa vinaendelea.
Nilipokwenda Cairo nikasali Ijumaa msikiti mmoja uko katikati ya mji jirani ni ilipo Egyptian Museum.
Ninachokumbuka msikiti huu ni kuwa sikuweza kuingia ndani msikitini kwa kuwa msikiti umejaa hadi nje watu wengi wako wengi nje barabarani.
Sifa kubwa ya mji wa Cairo ni wingi wa watu na wingi wa magari barabarani Waingereza wanaita, "bumper to bumper," na madereva wanashindana kupiga honi.
Mwaka uliofuatia nikaenda Sudan nikasali Sala ya Ijumaa msikiti wa Chuo Kikuu Cha Khartoum mwaka wa 1989.
Nilifika Sudan miezi michache baada ya Omar Bashir kupindua serikali na kutwaa madaraka.
Picha iko hapo chini utaitambua kwa kanzu na vilemba vya Kisudani.
Mwaka wa 1991 nimesali msikiti mkuu wa Glasgow, Scotland.
Katika misikiti niliyopata kusali sijapata kusali msikiti nikawa mimi ndiyo mtu mweusi peke yangu ndani ya msikiti kiasi watu wote ndani ya msikiti wananishangaa.
Naingia msikiti macho yote yako kwangu.
Nasali, ''tahiyatu masjid,'' yaani sala ya kuuamkia msikiti, macho yote ndani ya msikiti yako kwangu.
Jambo hili lilinifanya nijisikie vibaya.
Baada ya sala nimeingia kwenye duka la vitabu la msikiti.
Ndugu zangu Waislam wakanifuata kunisalimia na wakawa wananiuliza maswali.
Walitaka kujua wapi natoka na lini nimeingia Uislam?
Hawajui kuwa mimi ni mjukuu wa Sheikh Muhammad Mvamila.
Hawa ndugu zangu hawaijui Tanzania wala hawajapata kuisikia.
Nilipowaeleza kuwa nimezaliwa Muislam wakataka kujua Uislam umeingia lini Tanzania.
Walishangaa sana nilipowaeleza kuwa Uislam upo kwetu miaka 1000.
Nimesali Ijumaa Edinburgh.
Nilikwenda Edinburgh kwanza kuona Edinburgh Castle na kukitembelea chuo alichosoma Mwalimu Nyerere.
Edinburgh Castle ni sehemu inatembelewa sana na watalii na ni majumba mengi kwenye mlima mkubwa.
Hii mijumba ya kale iko hapo karne kwa karne.
Sehemu hii ilinikumbusha Macbeth wa William Shakespeare.
Niliyoshuhudia msikiti wa Glasgow sikuyaona Edinburgh hapo niliwakuta watu weusi wengi wao wakiwa wanafunzi kutoka Afrika.
Nimesali Ijumaa Msikiti wa Makka na Madina mwaka wa 1997, 1998 na 2014.
Mwaka wa 1997 nilikwena Umra na 1998 na 2014 nilikwenda Hijja.
Hijja ya 2014 nilipata mwaliko kutoka kwa Mfalme wa Saudia.
Waalikwa tulikuwa wengi kutoka Tanzania na kwengine ulimwenguni.
Picha hiyo hapo chini nimeupiga Masjid Badawy, Msikiti wa Mtume SAW kutoka dirisha la chumba cha hoteli niliyofikia 2014.
Nilinunua camera si mbali na Msikiti wa Mtume na nikajiambia kuwa picha yangu ya kwanza kupiga uwe Msikiti wa Mtume.
Hili nikalifanya.
Nimesali Ijumaa Tehran pamoja na Rais wa Iran Ahmed Najad mwaka wa 2007.
Nimesali Ijumaa Grande Mosque, yaani Msikiti Mkuu, Paris 2011.
Huu nidyo msikiti mkubwa Paris na Imam Mkuu ni Mngazija.
Hiyo picha hapo chini nimepiga na jamaa wa Kingazija nje ya msikiti.
Kulia kwenye picha ni rafiki yangu marehemu Salim Himid.
Nimesali Ijumaa New York mwaka wa 2011 kwenye kijimsikiti kidogo Manhattan, New York.
Msikiti huu nilikuta jamaa ndogo katika Sala ya Ijumaa si kama jamii nilizopata kuona kwengineko duniani.
Nje ya msikiti kuna askari wanafanya doria kulinda msikiti na wanaosali hapo.
Nimesali Ijumaa Istanbul mwaka wa 2015.
Takriban msikiti mzima watu wamepiga suti.
Sijui kama ni kawaida kuvaa suti au kwa sababu ulikuwa wakati wa baridi.
Nimesali Ijumaa Dubai Rashidiyya mwaka wa 2016.
Hii ni sehemu ambayo Wazanzibar waliotafuta hifadhi Dubai baada ya mapinduzi walipewa makazi hapo na kujengewa nyumba na Sheikh Rashid kiongozi wa Dubai.
Sala ya Ijumaa Msikiti wa Rashidiyya utasema uko Masjid Jibril Zanzibar,