Habari za muda sitaki matusi,wala kejeli na vijembe wakuu.
Nimekusudia kumsalimia mpendwa wangu wa siku nyingi sana ambae sijamsahau mpaka hivi leo ni
Miss Natafuta.
Popote alipo naomba mumpatie salamu zangu
Sent using
Jamii Forums mobile app
Unamtafuta spice wa jf? Katika wanawake wenye thread ama comments zao zizochosha ama kuboa, yeye ni mmoja wao.
Amebeba haiba yenye thamani sana kwa wanawake wa ki leo, saazingine hata yeye mwenyewe bila kujijua!
Nadhani huyu atakuwa ni msomi.
Lakini hata kama ni msomi, kuna wanawake wasomi wangapi wenye sifa mbofumbofu, ambao majibu yao kwa hoja ama maongezi tu ya mitaani, hauwezi kuwalinganisha na huyu hata kwa sifa za ufagizi wa ofisi kutokana na majibu ya kishenzi?
Huyu ana uwezo wa kupiga soga na vijana hadi vimbabu anavyotaka yeye bila kuboa. Kila sekta yupo vizuri anafiti.
Kwenye mambo ya mizaha yupo vizuri, kwenye mambo ya malavidavi yupo vizuri, kwenye mambo ya kielimu yupo vizuri pia.
Nitamshangaa akiwa hadi leo anatafuta, wakati yeye amekwisha jizolea sifa za kutafutwa!
Kwa haiba yake hiyo, kama ataendelea kuwa anatafuta, basi hicho kigezo atakuwa kakiweka mahususi kwa ajili ya kugaragazia wanaume makantongoze, lakini akawa hana shida kama jina lake linavyojinasibu!
Maana wanaume kama si wote, lakini wengi wanapenda mwanamke mwenye sifa kama zakwake, ambapo uchaguzi wa kuangalia sura huwa haupo na hauna maana tena.
Sent using
Jamii Forums mobile app