Salamu toka kwa Rev.Masanilo

Pole Uncle kwa kifungo, jitahidi kulamba ndimu kwa wingi, malimao na hata ukwaju ili ukirudi uje utupe story adimu...we miss u!

This is very funny! Kula ndimu kwa wingi ndo kunaleta story adimu?'
 
Mwambie tumemmiss pia ,Naomba nimpe box yangu ya kijiji anitupie hiyo kitu maalum kwa supu DL tafadhari
Firstlady1
Private Bag
Migombani Area
Misigiri
Singida
 
Hapo umena Jumatatu jioni kwa saa za Afrika Mashariki Mchungaji atakuwa huru! Hizi taarifa amenifikishia kwa njia ya sms

Shem tafadhali kua msiri kidogo...huoni mashushushu hapo juu??Au unataka vibaka wamsubirie baba mchungaji wangu mlangoni?
 
Shem tafadhali kua msiri kidogo...huoni mashushushu hapo juu??Au unataka vibaka wamsubirie baba mchungaji wangu mlangoni?

Pouwa shem langu la nguvu! Nadhani Uwiano hatosoma huku.
 
Huyu Pweza wa Mchungaji, RAY C bado hajamuona?

Maana Ray C analalamika kuwa "Pweza amefichwa alifikiri hatamuona, ila kumbe bibie kashamuona zamani...."

Ajihadhari sana huko maana Pweza anatafutwa kwelikweli.......

 
Last edited by a moderator:
Uzuri wa Jela ya JF si kama jela za uraiani maana huko inabidi UWE NA YA CHUMA.


Ukumbi ukikosa Mchungaji si itakuwa Kasheshe maana huyu REV. Kishoka yeye ni Kiingereza tu na wengine sisi Kiingereza izi noti richabo.
 
Last edited by a moderator:
Asante kwa ripoti toka jela ukienda kumjulia khali mpelekee kijibarua hiki. Nenda na mkate huu,mpe bwn jela ampe ale,ila mwambie ndani kuna kikaratasi cha ujumbe katikati mwa mkate. Ujumbe huu uko ivi: "mchungaji Rev. Masanilo,ile rufaa uliyoniagiza nikate,mahakama ilikataa ilisema acha mchungaji amalizie recöncilliation. Hata ivo mi nimefunga kwa kumwombea novena. Rev.Masa,wale kondoo wako wamekaukiwa neno na wameanza kutawanyika kwa kiu ya kiroho,pia ile mikate uliyoicha imekaribia kuisha,mchungaji wahi kurudi kwani kondoo wanakufa njaa. Juzi nimepita jangwa la MMU nkakuta kondoo wako wanakula majani makavu/thread ngumu. Rev.,ivi ule ubani uliuacha chumba gani?maana nimepita jamvin nkakuta kuna roho wachafu wanalinyemelea jamvi,pia mwambie Pilato aliyekupeleka huko utumikie dhambi ile pia awapeleke hawa wanaotutenga kwa makundi mawili kwa kigezo kimoja ili uwaachile uongozi wa jela. Rev. usiponkuta jamvini utembelee kaburi langu pale jf uweke ua na mshumaa. Nasema ivi kwa sababu jamvini kuna mbu wengi wanatoboa chombo chetu,pia chandarua imetoboka,alafu yule adui yako kasema viela vyote atawapa Dowans,sie tukae gizani. Tangu uondoke cm yako haipatikani,je hauichaji?au na jela kuna mgao wa umeme?siku moja ilipopatikana akapokea mdada kasema eti ndo bwn jela,je kama mnalindwa na bwn jela mdada una maana utabahatika kutuletea wanakondoo wadogo uliowapata ukiwa kifungoni? Pia ukija usirudi mbio huku hamna sadaka,melkisedeki amekula sadaka yote,pia wanakondoo wamegoma kutoa sadaka mpaka urudi. Kumbuka kurudi na nauli ya kutosha maana Sumatra wamesema lazma uje na nauli mpya,pia Dowans umeme wamepandisha 18% na Gas mtungi umepanda,ule wako tumejaza sh.47500/=sio msaada,ukija utanilipa maana ninajenga pale Rombo. Pia mzee Tambe kasema katiba mpya na tume ni changa la macho,sijui ana maana gani? Pia yule mwenyekiti wa kambi ya upinzan na katibu wake hawatakuja huko na kesi yao imepigwa kalenda, pia kamwambia H.R yule wa kambi ya upinzan ya bunge la9 kuwa aendelee kusubiri. Rev.mshumaa wangu unazimika hamna umeme,nadhan unaona mwandiko ulivoacha kusomeka. Kaa salama,ukija pitia mtoni ukaoge usilete vipele vya jela uraiani kumbuka huku maji ya mgao. Nakuomba ukija pitia pale Mahakamani uwaeleze kuwa umetubu dhambi iliyokupeleka siku40 jangwani kwa majaribio. Nakubariki mchungaji.Akukumbukaye,Nabii,@§¤:-"¤. GSANA."
 
mwambie twashukuru, asijali ndo dunia ha ha ha. hata si twamkosa pia
 
dah... para ndefu hadi macho yanauma
 
Mchungaji kapigwa selo kondoo wanatawanyika!!
 
huyo Rev Masanilo ndio nani,embu tuwekeni sawa na yuko jela kwa sababu gani mhh;;tujuzeni na sisi tumpe pole au mnajuana kwa vilemba wakongwe wa JF??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…