Pre GE2025 Salim ASAS: Uongozi CCM umekuwa kama Mnada. Watu wanapandishiana Dau kwa Wajumbe Ili kuununua!

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Tatizo mihuni na mijambazi ndiyo imepata kadi za CCM.
 
msigwa pesa zake akatumie na familia yake, zitaisha atakimbilia NCCR mageuzi kumalizia trace zake, kanisani hawezi tena maana waumini washashtuka
 
Huyu Asasi ni mhuni tu. Kwani ununuzi wa uongozi huko ccm umeanza leo? Mbona upo miaka mingi sana.
 
Hizi ndiyo hadaa zilizo baki huko CCM. Huyu anazungumza utadhani anaumizwa sana na hali hiyo aliyo ielezea; ambayo kwa kawaida ningeungana naye sana kumhimiza apige kelele zaidi huko ndani ya chama.

Lakini ukweli ni kwamba ni watu kama huyu ndio wanaozidisha maovu ndani ya chama hicho. Kwa hivyo vimaneno vyake vichache, atatupiwa mifupa na yeye alambe na kusahau maneno aliyokwisha zungumza.
Akisha kusanya vya kutosha, na yeye anaingia mnadani na dau lake!

Kama chama kimefikia huko anakokusema, yeye bado anafanya nini ndani ya chama kama hicho?

Kutamka tu maneno haya mazuri, tena mara moja moja ndiko kutakako badilisha hali ya huko CCM?
 

Mmmmhhh yeye aliishia ngapi au alizidiwa kwa ngapi??[emoji15][emoji15][emoji15][emoji15]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…