Salim Himidi na Mgahawa wa Kihindi Paris

Salim Himidi na Mgahawa wa Kihindi Paris

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
Salim alikuwa hapendi tule kwenye migahawa yenye vyakula vya Kizungu na siku zote akinipeleka migahawa ya Kihindi na kuna mgahawa mmoja akiupenda sana.

Mwenye mgahawa huu alikuwa Mzanzibari ambae baba yake alikimbilia Ufaransa baada ya mapinduzi ya mwaka wa 1964 na baada ya baba yake kufariki mwanae akawa anauendesha.

Hapo tutaagiza chai, chapati, sambusa na kababu pamoja na chatney yake. Ukitukuta hapo tunakunywa chai na ukatupia jicho sahani zetu wala huwezi kujua kama tuko katikati ya jiji la Paris, utadhani labda tuko ‘’Passing Show,’’ Malindi, au mgahawa wowote Stone Town, Zanzibar.

Tutakunywa chai huku tukisikiliza muziki wa Kihindi wa Lata Mangeshkar, Asha Bhosle, Mohamed Rafi na Mukesh uliokuwa ukipigwa kwa sauti ya chini sana.

Nilijua Salim akiwa hapa alikuwa anarejea udogoni Zanzibar akiiwaza Zanzibar ambayo haitaweza kurudi tena.

Salim akinihadithia utoto wake nyumbani Zanzibar na vipi filamu za Kihindi na nyimbo zake zilivyokuwa zikisikilizwa kila nyumba na vipi wacheza senama wa Kihindi kama Raj Kapoor, Dev Anand, Dilip Kumar, Nargis, Madhubala walivyokuwa maarufu visiwani.

PICHA: Picha hii nimempiga Bwanatosha akiwa kwenye mgahawa wake aupendao wa Kihindi Paris.


Himidi.jpeg

Himidi 1.jpeg
 
Ukiitizama historia ya Zanzibar na hali yake iliyonayo sasa kwa kweli inasikitisha sana
 
Maadamu tungewakubali wa kuja na kuwafanya waishi kwa amani Kweli nchi za Africa zingegika mbali sana
Kila nchi duniani matajiri wakubwa ni wa kuja na sio wazawa



Sent from my iPhone using Tapatalk
 
Sasa huyu alikimbia Zanzibar sababu ni mapinduzi ama utashi wake binafsi?
 
Hii inatupa Watanzania tusiojua maisha ya wenzetu walotangulia kabla yetu. Tukajua historia ya maisha na madhila waloyaapitia.
 
Umetaja Passing Show nikakumbuka Luukman na Mercury.

Ahsante kwa uandishi mujarab.
 
Dah!! Uandishi wako umepevuka, ulijua kuweka kumbukumbu zako sawia, habari+picha! Hata habari ikiwa fupi kama hii bado inatupa wasomaji extra miles, tunavisoma ambavyo hujaviandika, tunaviona ambavyo hujatuonyesha!!

Hakika Mungu aliubariki ujio wako hata kabla hujazaliwa, uendelee kutubariki kwa baraka zako mzee wetu, INSHAALLAH

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Luukman na Mercury ni nani hawa?

Migahawa/restaurants maarufu sana Unguja.

Lukmaan ipo mtaa wa Mkunazini na Mercury restaurant ipo maeneo ya Bandarini karibu na wanapoingilia abiria wakielekea kupanda boat.
 
Back
Top Bottom