Pre GE2025 Salma Kikwete: Sitosahau nilipogombea Ubunge na kura zangu zikahesabiwa hadharani

Pre GE2025 Salma Kikwete: Sitosahau nilipogombea Ubunge na kura zangu zikahesabiwa hadharani

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
1,869
Reaction score
4,877
Wakuu,

Mbunge wa Jimbo la Mchinga na mke wa Rais mstaafu wa Awamu ya Nne, Mama Salma Kikwete, amesema kuwa moja ya kumbukumbu asizoweza kusahau maishani mwake ni wakati wa kuhesabiwa kura hadharani alipogombea ubunge.

salma.jpg

Akizungumza leo Machi 5, 2025, katika kongamano la Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani lililoandaliwa na Halmashauri ya Chalinze, Mama Salma amesema kuwa hatua hiyo ilikuwa sahihi ili kuondoa shaka kuhusu ushindi wake.

"Kitu ambacho sitasahau maishani mwangu wakati nagombea nafasi ya ubunge ni kuhesabiwa kura hadharani. Niliona ni jambo sahihi kwa sababu kama tungehisabu ndani, wangesema nimeshinda kwa kura za itifaki," amesema Mama Salma.

Source: Nipashe
 
Kitu ambacho alipaswa asisahau ni kuongezea wananchi maskini mzigo wa Penseni ya wenzi wa Marais
Umempiga za uso, Hana hata aibu huyu mwanamke! Yeye na familia yake ni matrionea akataka waendelee kulipwa Tena! Hizi hela watalia kaburini? Hana utu kwa watz mafukara! Atajibu siku ya kiama!!! Atubu!!!
 
Akizungumza leo Machi 5, 2025, katika kongamano la Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani lililoandaliwa na Halmashauri ya Chalinze, Mama Salma amesema kuwa hatua hiyo ilikuwa sahihi ili kuondoa shaka kuhusu ushindi wake
Na mumewe alipokwenda west africa alisema kura zimehesabiwa peupe ila mbona za mwanaye hazikuhesabiwa peupe
 
Umempiga za uso, Hana hata aibu huyu mwanamke! Yeye na familia yake ni matrionea akataka waendelee kulipwa Tena! Hizi hela watalia kaburini? Hana utu kwa watz mafukara! Atajibu siku ya kiama!!! Atubu!!!
tatizo hata hizo za uso hazimpati au wanasema dua la kuku halimpati mwewe...
 
Wakuu,

Mbunge wa Jimbo la Mchinga na mke wa Rais mstaafu wa Awamu ya Nne, Mama Salma Kikwete, amesema kuwa moja ya kumbukumbu asizoweza kusahau maishani mwake ni wakati wa kuhesabiwa kura hadharani alipogombea ubunge.


Akizungumza leo Machi 5, 2025, katika kongamano la Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani lililoandaliwa na Halmashauri ya Chalinze, Mama Salma amesema kuwa hatua hiyo ilikuwa sahihi ili kuondoa shaka kuhusu ushindi wake.

"Kitu ambacho sitasahau maishani mwangu wakati nagombea nafasi ya ubunge ni kuhesabiwa kura hadharani. Niliona ni jambo sahihi kwa sababu kama tungehisabu ndani, wangesema nimeshinda kwa kura za itifaki," amesema Mama Salma.

Source: Nipashe
Wahaya na waganda wanasema: watubeyahaa
 
Yooote tisa, kwa hiiiyo "Kura ya Itifaki" si ajabu atapewa muongozo ss hv.

ndio kusema ilikuwa kura ya democrasia kweli kweli, achana na bao la mkono.
 
Wakuu,

Mbunge wa Jimbo la Mchinga na mke wa Rais mstaafu wa Awamu ya Nne, Mama Salma Kikwete, amesema kuwa moja ya kumbukumbu asizoweza kusahau maishani mwake ni wakati wa kuhesabiwa kura hadharani alipogombea ubunge.


Akizungumza leo Machi 5, 2025, katika kongamano la Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani lililoandaliwa na Halmashauri ya Chalinze, Mama Salma amesema kuwa hatua hiyo ilikuwa sahihi ili kuondoa shaka kuhusu ushindi wake.

"Kitu ambacho sitasahau maishani mwangu wakati nagombea nafasi ya ubunge ni kuhesabiwa kura hadharani. Niliona ni jambo sahihi kwa sababu kama tungehisabu ndani, wangesema nimeshinda kwa kura za itifaki," amesema Mama Salma.

Source: Nipashe

Kwenye kampeni za uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2005 kilikuwa na msemo uliokuwa ukifahamika kwa kifupi kwa jina la:
BMW (Baba, Mama na Watoto)
 
Back
Top Bottom