TANZIA Salum Shamte wa Katani Ltd afariki dunia

Informer

JF-Expert Member
Joined
Jul 29, 2006
Posts
1,606
Reaction score
6,672


Mkurugenzi wa zamani wa Katani Limited Salum Shamte amefariki dunia katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, alikokuwa akipatiwa matibabu.

Oktoba 31, 2019, Salum Shamte pamoja na wenzake akiwemo Juma Shamte ambaye ndiye Mkurugenzi wa sasa wa Katani Limited na mjumbe wa bodi, Fatma Diwani walipandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Tanga wakikabiliwa na mashtaka matatu.

Walikuwa wanakabiliwa na mashtaka ya uhujumu uchumi, utakatishaji fedha na kusababisha hasara ya Sh1.14 bilioni kwa vyama vya msingi vya ushirika (Amcos).

Mapema mwezi Machi 2020, Waziri Mkuu alipokea ripoti iliyozidi kumweka pabaya Shamte (kimsingi ripoti pia inamweka pabaya zaidi Dr. Dau aliyekuwa NSSF); isome hapa chini:

 
Tutaiba, tutadhulumu, tutafanya yooote, mwisho wa siku tunaondoka tukiwa watupu tunarudi Mbinguni kwa Mungu aliyetuumba.

Twendeni kwa tahadhari.

Pumzika Shamte!

Sent using Jamii Forums mobile app
Lile kundi la Wafanyabiashara wazawa linazidi kuyoyoma.......Mengi, Mafuruki, Idd Simba na sasa Shamte.
 
Nenda mwanakwenda Shamte. Ulimdhulumu sana Uncle wangu, akawa demoted, wewe na akina Marehemu Ibrahim Kaduna, mkamfanya aishi maisha magumu na ya stress sana. Mkadhulumu haki miliki za tafiti zake, aligundua jinsi ya kutengeneza pombe kwa kutumia maji ya mkonge, chakula cha kuku kwa kutumia mabaki ya mkonge na umeme kwa kutumia maji maji ya mkonge.

aliandika vitabu kuhusu mkonge lakini hakufaidika navyo. Alinieleza haya 2007 na mwaka huo huo akapata stroke, nilimuuguza Tanga, mkashindwa kumlipia hata Ambulance kutoka Tanga to Muhimbili.

nilipowatafuta kwa ajili ya matibabu yake mkaishia kunipa Tzs 50,000. Mzee Shamte unakumbuka siku ile uliniita pale fire? Ukampa dereva bahasha yenye hio pesa?
Baadae ali-recover bado mkagoma kumlipia bill, na MKUMBUKE alistahili sio kwamba ilikua fadhila.

Siku moja jioni ya 12 tukiwa tumerudi kutoka kwenye mazoezi ya viungo pale Morocco Physiotherapy clinic, STARTV wakawa wanaonyesha kipindi cha mkonge na walionyesha hizo products ambazo huyu mzee wangu ndio alikua amwzifanya yeye ila zilitangazwa kama vile ni kazi iliyofanywa na mtoto wa Shamte. Kwakuwa nilikua nine Shaun vanish a dots, nikachukua remote nikataka kubadili Chanel, ananiambia nisiondoe.

Next day akiwa kwenye mazoezi napata second stroke na ndio ikawa mwisho wake. Akina Shamte bado walishindwa hata kumsafirisha.

sina nia mbaya, kifo ni kifo but kwa kusema haya naamini nimemtendea haki Marehemu Mentor wangu. He was a true friend of Mine.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…