APA CHICAGO
JF-Expert Member
- Oct 20, 2019
- 259
- 292
Salaam kwenu wanabodi wa jukwaa hili kubwa na lenye heshima ndani na nje ya nchi yetu.Sio tu linaheshima lkn pia lina taarifa za kuaminika.
Nimeanza na neno samahani kwa wabunge wetu kwa sababu kelele zimekuwa nyingi sana huko bungeni wengi wa wabunge wanaopata nafasi ya kuchangia wamekuwa wakizungumzia masrahi ya wafanyakazio ikiwemo kupanda madaraja, mishahara na pension za wastaafu.
Kinachonishangaza kutoka kwa waheshimiwa hawa ni kuwa walikuwepo tangu awamu ya tano ilipoingia madarakani rasimi tangu 2016 hadi leo lakini walikuwa wanaimba mapambio ya Uhakiki wa wafanya kazi hewa na ujenzi wa miundo mbinu leo hao hao wamegeuza gia angani utazani hawakuwepo kabisa kipindi hiki chote ambacho watumishi wa umma walinyimwa stahiki zao na hadi leo wanaishi kwa mshahara alioupandisha Mara ya mwisho mhe,Jakaya Kikwete mwaka 2015.
Wana bodi kwa maoni yangu wabunge wetu hawana uwezo wa kuisimamia serikali badala yake wanatenda kazi zao kwa kuangalia Rais wa nchi aliyepo wakati huo anataka nini?
Ushauri wangu kwa wabunge ninawaomba wadai katiba mpya kwa niaba ya watanzania wote itakayo tupa nafasi ya kujenga Taasisi imara badala ya kutegemea utashi wa kiongozi aliyeshika madaraka wakati huo. Hii itasaidia pia kuwapa uwezo wabunge wetu kuisimamia serikali pia bunge letu tukufu liamue kufuta sheria na nyaraka kandamizi kwa mfano waraka wa Katibu Mkuu kiongozi unaowataka watumishi wa umma kuomba likizo ya bila malipo miezi miwili wakati wa kugombea nyazifa za kisiasa ni waraka wa hovyo katika nchi huru kama Tanzania.
Wote tumejionea chini ya uongozi wa hayati Dr.John Pombe Joseph Magufuli watu wazima wamechapwa viboko hadharani na wateule wa rais, Watumishi wa umma wa umma wamenyanyaswa vya kutosha kwa sababu tumekosa taasisi imara zinazopewa nguvu kwa mujibu wa katiba ya nchi.
Wabunge wetu ambao ni wawakilishi wetu tusaidieni kudai Katiba mpya kama mna nia ya dhati.
Nimeanza na neno samahani kwa wabunge wetu kwa sababu kelele zimekuwa nyingi sana huko bungeni wengi wa wabunge wanaopata nafasi ya kuchangia wamekuwa wakizungumzia masrahi ya wafanyakazio ikiwemo kupanda madaraja, mishahara na pension za wastaafu.
Kinachonishangaza kutoka kwa waheshimiwa hawa ni kuwa walikuwepo tangu awamu ya tano ilipoingia madarakani rasimi tangu 2016 hadi leo lakini walikuwa wanaimba mapambio ya Uhakiki wa wafanya kazi hewa na ujenzi wa miundo mbinu leo hao hao wamegeuza gia angani utazani hawakuwepo kabisa kipindi hiki chote ambacho watumishi wa umma walinyimwa stahiki zao na hadi leo wanaishi kwa mshahara alioupandisha Mara ya mwisho mhe,Jakaya Kikwete mwaka 2015.
Wana bodi kwa maoni yangu wabunge wetu hawana uwezo wa kuisimamia serikali badala yake wanatenda kazi zao kwa kuangalia Rais wa nchi aliyepo wakati huo anataka nini?
Ushauri wangu kwa wabunge ninawaomba wadai katiba mpya kwa niaba ya watanzania wote itakayo tupa nafasi ya kujenga Taasisi imara badala ya kutegemea utashi wa kiongozi aliyeshika madaraka wakati huo. Hii itasaidia pia kuwapa uwezo wabunge wetu kuisimamia serikali pia bunge letu tukufu liamue kufuta sheria na nyaraka kandamizi kwa mfano waraka wa Katibu Mkuu kiongozi unaowataka watumishi wa umma kuomba likizo ya bila malipo miezi miwili wakati wa kugombea nyazifa za kisiasa ni waraka wa hovyo katika nchi huru kama Tanzania.
Wote tumejionea chini ya uongozi wa hayati Dr.John Pombe Joseph Magufuli watu wazima wamechapwa viboko hadharani na wateule wa rais, Watumishi wa umma wa umma wamenyanyaswa vya kutosha kwa sababu tumekosa taasisi imara zinazopewa nguvu kwa mujibu wa katiba ya nchi.
Wabunge wetu ambao ni wawakilishi wetu tusaidieni kudai Katiba mpya kama mna nia ya dhati.