Samatta hana kiwango Cha kucheza EPL

Samatta yupo vizuri Sana. Sasa hawezi kukaba yeye, atoe pasi yeye afunge yeye. Tumefunga magoli mawili tu na yote yana juhudi za Samatta. Alipiga shuti likamshinda kipa ndio Msuva akafunga, lingine ni yeye katikati ya mabeki watatu na kipa wao juu akafunga. Tusifananishe kiwango hicho na watu wanaofunga kwa kuwa timu zao ni nzuri zaidi ya yetu.
ili awe bora lazima awe na wachezeshaji wazuri kwenye eneo la kiungo... Mbwana yupo vizuri ni mchezaji mzuri mwenye kipaji cha mpira
 
Kama Samata angekuwa Msenegali sahivi tungesikia tu Mbongo anavyompambana, "Kuna Msenegali yuko Genk anatupia hatari naskia Chelsea na Everton zinamtaka...." Ila kwa kuwa ni Mtanzania mwenzetu basi imebidi tu ili litimie lile neno... "Mbongo anapenda maendeleo ila anachukia wenye maendeleo".
 
Biashara ni branding. Hao unaona wazuri matangazo mengi yanasaidia. Sammata angekuwa mkenya angeonekana mfalme, lakini wabongo tunavutana mashati. Yaani Belgium wanaimba Samagoal halafu kuna mbongo anasema hakuna kitu.
 
Kweli kabisa, yaani Genk wanaimba Samagoal halafu wasikie kuna mbongo anasema hamna kitu hapo, si aibu.
 
Shukrani sana...
 
Ingia Utube uangalie Mbwana Samatta Skills ndio utajua uwezo wake...
 
Ujue kuna comment nyengine mpaka naishia kucheka,mtu anakomaa kabisa anasema samata ndo mfungaji bora ubelgiji kwa kufuatilia vitu vya April wakati ligi imeisha mwezi may.Kama hufuatilii soka acha kuzungumzia soka.
 
Hii misimu miwili consecutive, sasa kama unajua hilo unawezaje kumhukumu Samatta kwa mechi tatu na timu yenyewe bado haijaandaliwa ikawa Bora? Lakini kama unaangalia mpira kwa usahihi tusingebishana, either huangalii au unaangalia ukiwa na biasenes. Samatta anajiamini, ana nguvu na anajiposition vizuri. Zaidi ya hapo ni kiongozi mzuri uwanjani. Ana speed. Sio rahisi watu kuimba jina lako Belgium. Tutangaze vya kwetu tuache kuoneana wivu. Angekuwa mkenya kila mtu angekuwa anataja Samatta.
Pole mkuu huyo lukaku ni mfungaji bora wa national team... huko uingereza ni hii misimu 2 mambo yake hayajaenda sawa but samata n mchezaji wa kawaida tu mwenye bahati hana maajabu yyte uwanjan
 
Pole nafikiri hujanielewa sijasema samata ni mchezaji mbovu nimekuambia ni mchezaji wa kawaida tu... Labda nikuulize tu samata tangu aanze kucheza nation team yupo na goli ngapi? Bongo hatuna wachezaji bora, tunawachezaji wa kawaida tu
 
Sasa timu yenyewe bado. Ndio maana kawashauri watoke nje wapate exposure. Hawezi kucheza peke yake timu nzima. Hivi unadhani tukimleta Christano Ronaldo, Messi au Mbape ata perform bongo kama anavyo perform huko kwao? Dah, naona wewe una beef naye tu. Huwezi kumhukumu kwenye timu hii. Ame prove akiwa TP Mazembe alikuwa top scorer based in Africa. Akaenda Genk unamuona, Wabelgiji hawawezi kuleta mtu wa kawaida kutoka Africa tena nchi iliyo chini kwenye rank za FIFA, lazima ufanye vitu extra ordinary.
Pole nafikiri hujanielewa sijasema samata ni mchezaji mbovu nimekuambia ni mchezaji wa kawaida tu... Labda nikuulize tu samata tangu aanze kucheza nation team yupo na goli ngapi? Bongo hatuna wachezaji bora, tunawachezaji wa kawaida tu
 
Sasa niwe na beef na mtu asiye nifahamu? Mimi naamini hata ww ukiambiwa Leo utaje top20 ya mastreka Africa huwez mtaja japo unaamin n mchezaji mzuri kwangu n wakawaida tu mwenye bahati
 
Nikiwahi kusema ikaonekana wivu, jamaa kwanza umri umesonga, kila mwisho wa msimu wanatuletea tetesi kibao lakini baadae utasikia karudi Belgium.
 
Hiki kitu nishawahi kukiona yaani ukiwaangalia wachezaji wanaocheza nje na hawa wa ndani wakiwa timu ya taifa huoni tofauti.
Wote wanaruka ruka tu uwanjani
 
kuna watu wa ajabu sana aisee dah wanaleta ma chart ya april bila kujua format ya league ya belgium jupiler league,hadi kufikia april kabla ya kwenda play off samatta ndo alikuwa anaongoza ,sijui nabishana na wafu?
Kabla ya Playoffs Samatta alikuwa anaongoza..enheeee baada ya play offs kuisha ikawaje... utakuwa msukule
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…