Santiel Kirumba achangia Bajeti ya TAMISEMI Sekta ya Elimu

Santiel Kirumba achangia Bajeti ya TAMISEMI Sekta ya Elimu

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301

MHE. SANTIEL KIRUMBA ACHANGIA BAJETI YA TAMISEMI SEKTA YA ELIMU

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Shinyanga Mhe. Santiel Eric Kirumba ameunga mkono hoja ya kupitisha bajeti ya Wizara ya TAMISEMI ambapo amechangia hasa upande wa Elimu kwa watoto kupewa chakula mashuleni.

Mwaka 2021 Bunge lilipitisha mpango wa kitaifa kuhusu kutoa chakula mashuleni kupitia Wizara ya TAMISEMI.

Mkoa wa Shinyanga Mpango wa kutoa chakula umetekelezeka kwa Shule 205 na kati ya Shule 609 zilizopo Mkoa wa Shinyanga ni Shule 290 tu zinazotoa chakula cha mchana

Kukosa chakula mashuleni kunapelekea watoto kuwa watoro mashuleni, wadumavu kiafya na kurudi nyuma kielimu. Shule nyingi hazifanyi vizuri kutokana kwamba watoto hawapati chakula shuleni

Mtoto mdogo wa miaka saba mpaka kumi na nne anaenda shuleni anakaa saa moja asubuhi mpaka saa tisa mchana bila chakula, kwa namna yoyote Mtoto hawezi kufanya vizuri kwenye masomo

Mhe. Santiel Kirumba ameishauri Serikali kuwa vipindi vya masomo mashuleni vianze saa tatu asubuhi

Pia, Mhe. Santiel ameshauri Serikali itumie wadau wa elimu kama PCI waweze kusaidia kutoa chakula mashuleni ili kupunguza utoro, kuongeza ufaulu wa watoto na kupunguza Udumavu wa Afya.


WhatsApp Image 2023-04-19 at 15.43.23.jpeg
 
Back
Top Bottom