Sare za Shule, Kwa nini?

Kutokuwako madawati sio kigezo cha kuwafanya wasivae yunifomu hujapitia darasa nini? Komaa watoto waende shule na sare sio unalewa tuuu halafu ukishindwa unalalama
 


Hilo Hapo juu ni Darasa la Mzungu wakati wa Ukoloni Nchini mwetu, mbona Watoto wamekaa Darasani hawana hata Mashati? Unafikiri kwa nini?

Ni Kwa sababu kwa Mzungu Elimu ni muhimu kuliko kitu kingine chochote kile. Kwa sababu Mzungu anajua Mtoto akielimika atajikomboa na matokeo yake Utapunguza Umaskini kwani atajifunza mambo ambayo yatamnufaisha yeye pamoja na Jamii yake, lkn wewe unaona ni Bora Mtoto akae Nyumbani kwa kukosa Sare kuliko kupata Elimu, sasa naanza kuelewa kwa nini sisi ni Masikini na tutabaki kuwa Masikini Daima, Mpaka tutakapoweza kutambua ni Mambio gani yanafaa kupewa KIPAUMBELE wa kwanza ktk Maisha!
 
Muwasilisha mada, wazazi wanakosa fedha za kununulia nguo ama sare?, iweje wapate za kununulia nguo za nyumbani wakose za kununulia sare? jaribu kutengeza hoja kamilifu idiyo kuwa na ombwe ndani yake. umesema
 

Wewe acha unafiki, aidha utakuwa hauishi TZ au kama unaishi TZ basi utakuwa hauna Akili timamu, kwa maana kama unataka kusaidia Watoto yatima si uanze na watoto wa Miaka 10 wanaosha Vioo vya Magari kwenye Mataa Dar?

Hivi ktk Nchi kama TZ unaweza kutafuta Maskini wa kusaidia Kweli? Hao Watoto walipaswa kuwa Darasani lkn wameondoka vijijini wamekuja Dar kwa ajili ya Umaskini wapo kila mahali, kama wewe ni Mtu wa kusaidia ungeanzia hapo!
 
Muwasilisha mada, wazazi wanakosa fedha za kununulia nguo ama sare?, iweje wapate za kununulia nguo za nyumbani wakose za kununulia sare? jaribu kutengeza hoja kamilifu idiyo kuwa na ombwe ndani yake. umesema

Kwani sare ni Magome ya MIti? Hilo ni swali Gani unauliza? Wewe ukitembea TZ ndio utajua, hizo nguo wanazovaa wengi wao ni mitumba ambayo wanapewa na Wazungu au makanisani huko Misheni, sasa Wazungu hawagawi Sare za Shule hizo ni lazima wanunue!

Ukifika Umasaini au Dodoma huko kwa Wasandawe au hata Iringa Vijijini na Shinyanga ndani ndani, Watu hata Pesa hawatumii, mimi nimefika vijiji TZ hihi yetu Watu wanabadilishana Mazao na siyo kwamba anauza kitu ili apate Pesa, kwani hakuna mwenye Pesa ya kununua chochote! Kuna Vijiji nimefika nilikuwa naPesa lkn hakuna cha kununua mpaka uende Wilayani!

 
Sare za shule ni muhimu katika kujenga taifa moja na imara. Ikiruhusiwa kila mtoto aende shule na atakacho, basi kutakuwepo na watakaokwenda uchi kwani kuna wazazi ambao kwa ujumla hawataki kuwajibika kwa watoto wao na wale watakaokuwa wanabadilisha viwalo kila siku. Wanafunzi wengine, hata wale ambao wasingejengewa inferiority complex, huanza kukua nayo pole pole. Mwishoe ni psychological tourture na mtengano wa kitaifa kuanzia ngazi ya chini kabisa. Walioweka sare walikuwa na maana yake na mimi mwenyewe kwa kusoma shule ya sekondari ya aina hiyo miaka ya 80 najua madhara yake fika.
 

Kwa hiyo kwa maoni yako ni kwamba ni Bora Mtoto akae nyumbani mpake apate Sare ndiyo aende Shule?
 
Kwa hiyo kwa maoni yako ni kwamba ni Bora Mtoto akae nyumbani mpake apate Sare ndiyo aende Shule?

Watanzania wengi wanapenda kufanyiwa kila kitu, hawataki kufanya kazi kujiletea maendeleo, in short wengi ni wavivu wakitegemea serikali iwafanyie ila kitu.Mzazi huwezi zaa mtoto halafu hata shati na kaptula ya shule ushindwe kumnunulia, ukisubiri serikali ipitishwe sharia ya kuondoa uniform. Ni kiongozi mwenye maono mafupi ndio anaweza kuja na sheria ya kipuuzi kama hivyo. Maeneo mengine nchi hii, kwa kuwa ni lazima mzazi amnunuie mtoto nguo ndizo hizo hizo zinakuwa nguo za kutokea. Sare ni lazima kwani ina implication zaidi ya unachofikiria. Nguo za shule n msaada pia w malezi ya mtoto kwani akifanyavisivyo anaweza pata msaada au malezi muafaka. Kwa kifupi hoja yako haina mashiko.
 

Haujajibu swali unaleta tu maelezo marefu. Nimekuuliza Je, kwa maoni yako unaona Ni bora mtoto abakie Nyumbani mpaka mzazi apate Fedha ya Kumnunulia Sare?
 
huo ni uzembe wa wazazi na walezi na sio vizuri kupenda sana vya bure wakati nguvu na uwezo wa kutafuta unao. ningeshauri hao walezi wakishindwa kumpa nwanafunzi mahitaji madogo kama hayo wakamatwe na kupewa vifungo vya nje hata kutengeneza barabara..mitaro na usafi wa mazingira. tusijushushe kiasu cha kupenda kusaidiwa kila kitu. nina uhakika kuna mambo flani ukimba kuwasaidia watakua wakali kweli
 

Wakuu inawezekana mleta mada akawa na hoja.

Ila swali la kujiuliza vile vile: 'Ni kwanini sare nyingi zinazotumika mashuleni zinareflect dini ya wanafunzi?'
Kwani sheria/sera ya uvaaji sare shuleni inaelekeza kila mwanafunzi avae kwa mujibu wa matakwa ya dini yake?
Mbona wanafunzi wengi wanaovaa hijabu na misalaba wanaenenda tofauti na imani zao?

Tunapanda na kupalilia udini bila sababu za msingi kabisa!?!
 
Nadhani elimu ni bora kuliko unifomu. Hii Tanzania ni kubwa sana, kuna watu Tanzania hii hawana uhakika wa hata mlo mmoja sembuse unifomu. Mshukuruni Mungu mmezaliwa katika familia ambazo japo zina uhakika wa mlo. Hakuna anaependa kuwa na maisha duni, mazingira hayaruhusu watu kujikwamua kutoka ktk lindi la umasikini.
 


Kinachotusumbua watu wengi TZ ni ubinafsi uliopitiliza, kila mtu anajifikiria yeye tu, kwa kuwa yeye ana uhakika wa kula na mahali pa kulala basi anafikiri yoyote ambaye hana huo uhakika ni kosa lake na ni Mvivu, na hivyo ndivyo wengi wetu tunavyofikiri na inakwenda mpaka kwa Viongozi wetu na ndio maana hakuna mabadiliko yoyote, kila kitu kilichopo nchini kwetu kilifanywa na Wazungu, Wazungu ndio wanatunza yatima wetu, Wazungu ndio wanatoa fedha kwa ajili ya kuvisha watoto na Wazee wetu maskini Vijijini!
Viongozi wanasema Wazazi lazima wachangie Fedha kwamba Serikali haiwezi kuwafanyia kila kitu wakati yeye Serikali inamfanyia kila kitu mpaka chakula inamletea nyumbani, sasa huyu Mwanakijiji pesa atapata wapi kama hana kazi?

Mimi nimeyashuhudia haya, Mzungu anasafiri ktk Marekani au Ulaya kuja kuwaletea Watoto nguo, lkn Mtz anakaa Dar anakwenda kijijini kuwakebehi na smart phone na kurudi mjini kisha anakuja kusema kama Mzazi hawezi kununua Sare basi Mzembe, sasa yeye pesa atapata wapi kama hana kazi na wala Elimu hana? Atalima nini na amuuzie nani?

Sasa mtoto wake pia unamwambia asiende Shule mpaka anunue Sare, matokeo yake Mtoto anabaki Nyumbani na akifika Miaka 14 Mimba naye anapata Mtoto mzunguko wa ufukara unaendelea...
 

Unajua wewe ni sawa sawa na yule anayesema watu wote wasiokuwa na kazi ni Wazembe, ni kwa nini hawatafuti kazi, mimi mbona mimi nina kazi? Ndio Tafsiri ya maneno yako... wewe haujatembea Hii nchi ndio maana unaongea hivyo!

 
Mleta hoja aweza kuwa na hoja hapa, ila ni lazima kuangalia pande zote.....wazazi na wajibu wao...na serikali na wajibu wake.

Mimi binafsi naunga mkono uvaaji wa uniforms...kwani hata kuvaa uniform kila anapoenda shule mwanafunzi ni sehemu ya elimu....si sawa na kumkuza mtoto anayekurupuka tu asubuhi na "masurupwete" kubeba madaftari na kukimbilia shuleni....lazima tujenge jamii itakayotofautisha shuleni na machungani (kuchunga ng'ombe, kondoo au mbuzi).

Na kama kweli shule zetu zinatimiza wajibu inavyotakiwa, huwa ni rahisi zaidi kusimamia usafi wa mwanafunzi akiwa na uniforms kuliko akija amevaa blangeti.....

Pia inajenga nidhamu kwa wazazi na watoto wao kwani huwapelekea kufanya juu chini kuhakikisha uniform ni safi kwa njia yoyote ili kufuata matakwa ya shule....bila hivyo hakutakuwa na ufuaji wa nguo aise.

Nasi wanainchi pia lazima tuangalie na upande wetu...nadhani tuepukane na kuongeza tuuu familia....kama mzazi unajiona huna uwezo epuka familia kubwa....watoto watano, sita au saba wa nini wote hao...
 

Unachoongelea wewe ni Matokeo ya mambo ambayo yameshatokea, watoto wameshazaliwa kama wazazi wao walifwata au hawakufwata Uzazi wa mpango hilo ni swala lingine, lkn hoja wapo tena wengi na wanazuiwa kwenda Shule kwa sababu hawana Sare, sasa Je ni sawa kumkosesha mtoto Elimu kwa sababu baba au mama au sijui Mlezi hana fedha ya kununua Sare ya Shule? Ndio Hoja yangu hapa! Haijalishi kama Baba au Mama ni mlevi ukweli unabaki kwamba Mtoto au Watoto hawasomi, sasa Je ni haki kwa huyu Mtoto? Yeye ana kosa Gani?

 

Hii siyo mada mbona nguo zisizo za shule wanakuwa nazo,muhimu ungesema uhamasishaji wa wazazi kuwapeleka watoto wao shule uongezeke,serikali ihakikishe walau mlo mmoja unapatikana kwa wanafunzi kwa siku kwa ajili ya kuwafanya watoto ambao familia zao hazina uhakika wa chakula kwa kila siku nao waweze kusoma wakiwa wameshiba,sare ni kitu cha mara moja kwa mwaka gharama yake haizidi 15000 hili linawezekana kwa kila mzazi anayejishughulisha
 
Haujajibu swali unaleta tu maelezo marefu. Nimekuuliza Je, kwa maoni yako unaona Ni bora mtoto abakie Nyumbani mpaka mzazi apate Fedha ya Kumnunulia Sare?

Na ndicho nilichokujibu. Mzazi hana budi kuhakikisha anamtunza motto wake kwa kumpatia mahitaji muhimu ikiwemo sare za shule. Short of that mtoto abakie nyumbani. Ikiwa sheria itambana mtoto lazima aende shule mzazi atafanya kazi kutafuta hiyo uniform. Lazima uwe na puhing factor ya watuufanya kazi na si vinginevyo.
 

Nimesema nidhamu ya kuvaa uniform nayo ni elimu....na sioni haja ya mzazi kulegezewa hapa, mzazi awajibike....na kama anashindwa kumudu hata unifomu basi eneo husika wamuadhibu, na watoto wajifunze kupitia adhabu anayopata baba yao,ili nao wakikua waepuka kufanya kama mzazi wao ikiwa ni pamoja na kupanga uzazi.

Mkiwadekeza wanainchi kupita kiasi mnazalisha taifa la wasiothamini mali/vitu......kama tuonavyo sasa mali za ni uma zinageuzwa shamba la bibi...

Mashabiki wa simba na Yanga kila siku wanahujumu ule uwanja kwa kuwa tu vichwani mwao wanaona ni mali ya umma...lakini mngewachangisha na kuwatumikisha kwa nguvukazi mashabiki haohao kamwe hawatofanya ufedhuli tunaoshuhudia sasa..

..so wazazi wawajibike kwa uzao wao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…