Saruji kutoka nje inadaiwa kusababisha Serikali kupoteza mapato ya Sh25 bilioni kwa mwezi

mpigakura mlipakodi

Senior Member
Joined
Apr 24, 2013
Posts
143
Reaction score
33
Saruji kutoka nje inadaiwa kusababisha Serikali kupoteza mapato ya Sh25 bilioni kwa mwezi.


Dar es Salaam.

Kampuni ya Uzalishaji Saruji Tanzania Portland Cement Company (TPCC), imeomba Serikali kuanzisha juhudi za makusudi zitakazosaidia kukabiliana na uingizaji bidhaa nchini zisizo na viwango ikiwamo saruji.


Akizungumza na Kamati ya Bunge ya Uchumi, Viwanda na Biashara iliyotembelea kiwanda hicho mwishoni mwa wiki iliyopita, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya TPCC, Pascal Lesoinne, alisema suala hilo kama halijapatiwa ufumbuzi litaathiri uhai wa kampuni nyingi nchini, hatimaye uchumi wa nchi.



“Kampuni nyingi za Kitanzania za saruji hivi sasa zinakumbana na ushindani mkubwa kutoka kwa saruji itokayo nje hasa Pakistan,” alisema Lesoinne na kuongeza:

“Waingizaji saruji kutoka nje wanatumia ipasavyo mianya iliyopo kwenye mfumo wa forodha na uingiaji bidhaa kwa kulipa kati ya asilimia tano mpaka 10, hali ambayo inasababishia nchi hasara ya zaidi ya Sh25 bilioni.”

Aliongeza kuwa Tanzania haihitaji saruji kutoka nje, kutokana na uwapo wa viwanda vingi vinavyoweza fikia mahitaji ya nchi kikamilifu.



Pia, Lesoinne alisema kutokuwa na umeme wa uhakika, kumeongeza gharama za uendeshaji kwa kampuni yake na kwamba, inatumia zaidi ya Dola 2 milioni za Marekani kwa mwezi kwa ajili ya umeme mbadala.

Naye Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila, alionyesha wasiwasi wake kuhusu jitihada zinazochukuliwa na mamlaka husika na kuzitaka kufanya uchunguzi sahihi kujua ukweli wa suala hilo.

“Hili ni suala nyeti. Kamati hatuwezi kulifumbia macho kwa sababu lina athari kwenye maendeleo ya uchumi wa nchini yetu,” alisema Kafulila.



Naye Mkurugenzi wa Viwanda Wizara ya Viwanda na Biashara, Eliness Sikazwe, alisema Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk Abdallah Kigoda, tayari ameteua kamati ya wanachama saba kuchunguza suala hilo.


Source Mwananchi

My TAKE:

Saruji ya Twiga karibu yote iliyopo sokoni imechakachuliwa. Kuna tetesi kwamba agents wao wanahusika na TBS pamoja na kiwanda wanafahamu mchezo huo huu.

Napendekeza TBS wachukue hatua za haraka dhidi ya mchezo huu unaoitwa kupiga nyoka ili kunusuru hadhi ya nembo yao. Vile vile kiwanda kibadili vifungashio wanunuzi tuache kuuziwa cement kilo 45 kwa bei ya kilo 50.

Otherwise tutaendelea kushuhudia cement ya nje ikiliteka soko.
 
Kwani huyo meneja wa kiwanda hajui kua gharama za uzalishaji ndio zinazofanya makadirio ya bei kupanda, na hapo ndipo mwanya wa soko la saruji za nje unapopatikana? Kwanini asiiambie serikali wazi kua wao ndio wanaoua soko la ndani, na aombe uwiano wa ushindani katika soko uwe wa haki.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…