The Palm Tree
JF-Expert Member
- Apr 13, 2013
- 7,951
- 12,541
Watazame na wasikilize wanaoongoza serikali hii yaani CCM, Magufuli na wenzake wanavyojitetea kwa kila aina ya mashambulizi ya mwili na maneno mabaya dhidi ya wanaowaona kama vikwazo kwao yaani kina Tundu Lissu na CHADEMA yake, kina Zitto Z. Kabwe, Maalim Seif Shariff Hamad na ACT Wazalendo yao.
Yaani utadhani ni raia wa nchi zilizo katika sayari tofauti zenye uadui mkubwa. Na hawa kwa kuwa wana machineries za kutesea na kuulia yaani bunduki na risasi, polisi na jeshi, basi huzitumia ipasavyo ili kulinda positions zao na chakula cha MATUMBO YAO.
Tuseme nini sasa?
Ni hivi, asikudanganye mtu, hakuna cha uzalendo wala nini bali ni hadaa za uzalendo uchwara tu ili kuhakikisha maslahi ya matumbo yao hayapotei!
Hebu wasikilize na watazame kina Freeman Mbowe, Tundu Lissu, Halima James Mdee na wenzao wengi huko CHADEMA wanavyowashambulia wenzao huko CCM kwa kejeli na kila aina ya maneno unayoweza kuita matusi.
Watazame na kuwasikiliza na kina Zito Kabwe, Maalim Seif Sharif Hamad na wenzao huko ACT WAZALENDO wanavyowashambulia wenzao walio ktk chungu cha chakula yaani CCM kwa kila aina ya kejeli na neno lolote lile unaloweza kuliita tusi.
Yaani utadhani ni watu wanaoishi nchi zilizo katika sayari tofauti. Wengine Sayari ya Mars wengine sayari ya Dunia.
Tuseme nini sasa?
Ni hivi, asikudanganye mtu hakuna cha uzalendo wala nini. Hakuna anayepigania maslahi ya mtu mwingine awaye yeyote bali yao na matumbo yao mwenyewe.
Wengine ili kuteka nyara mawazo ya sisi wanaotuhadaa kuwa wanatupigania, wametupa majina ya kuutweza utu wetu kama "wanyonge", " walalahoi" nk.
Yote haya ni zana tu ili waaminike na kuficha uhalisia "missions" zao ovu.
Ni bahati mbaya kuwa, na sisi raia wa kawaida tumekubali na kuingia kwenye hadaa hizi na kujikuta tunaunga mkono moja ya pande maslahi hizi yaani WATAWALA na au WANAOTAKA KUZICHUKUA NAFASI ZA UTAWALA a.k.a wapinzani.
Kwa kufanya hivi, tumeifanya mission yao iwe rahisi sana. Na sisi wananchi wa kawaida katika mazingira haya, kamwe hatutakuja kupata tunayoyatamani katika nchi yetu.
Haya ninayoandika yamethibitishwa na Maalim Seif Sharif Hamad wa ACT WAZALENDO kwa kuamua kujiunga wa aliokuwa anawaona maadui zake na sisi wananchi tukaamini hivyo.
Sasa kawatelekeza na kuwaacha wananchi aliowaaminisha kuwa wakati wa kukomesha dhuluma umefika iwe jua ama mvua kwa yeye kujiunga na CCM tulioaminishwa kuwa ndiyo maadui wa ustawi wetu!
Natamani kuanzia leo nisimwamini mwanasiasa yeyote. Na ofcoz ndivyo itakavyokuwa. Na nitatumia njia zingine kabisa kupambania hali na ustawi wangu kijamii na kiuchumi.
Wamebaki kina Freeman Mbowe, Tundu Lissu na CHADEMA yao kwa ujumla. Tusishangae wakajiunga na waliotuaminisha kuwa ni maadui wa ustawi wetu.
Kweli kabisa, binadamu ni kiumbe kisicho na perfect definition. Ulivyo wewe ndugu ndivyo hivyo ulivyo. Asije mtu kukudanganya kuwa umuamini yeye na kwamba anaweza kukufanya na kukugeuza uwe mtu tofauti na alivyokuumba Mungu.
Yaani utadhani ni raia wa nchi zilizo katika sayari tofauti zenye uadui mkubwa. Na hawa kwa kuwa wana machineries za kutesea na kuulia yaani bunduki na risasi, polisi na jeshi, basi huzitumia ipasavyo ili kulinda positions zao na chakula cha MATUMBO YAO.
Tuseme nini sasa?
Ni hivi, asikudanganye mtu, hakuna cha uzalendo wala nini bali ni hadaa za uzalendo uchwara tu ili kuhakikisha maslahi ya matumbo yao hayapotei!
Hebu wasikilize na watazame kina Freeman Mbowe, Tundu Lissu, Halima James Mdee na wenzao wengi huko CHADEMA wanavyowashambulia wenzao huko CCM kwa kejeli na kila aina ya maneno unayoweza kuita matusi.
Watazame na kuwasikiliza na kina Zito Kabwe, Maalim Seif Sharif Hamad na wenzao huko ACT WAZALENDO wanavyowashambulia wenzao walio ktk chungu cha chakula yaani CCM kwa kila aina ya kejeli na neno lolote lile unaloweza kuliita tusi.
Yaani utadhani ni watu wanaoishi nchi zilizo katika sayari tofauti. Wengine Sayari ya Mars wengine sayari ya Dunia.
Tuseme nini sasa?
Ni hivi, asikudanganye mtu hakuna cha uzalendo wala nini. Hakuna anayepigania maslahi ya mtu mwingine awaye yeyote bali yao na matumbo yao mwenyewe.
Wengine ili kuteka nyara mawazo ya sisi wanaotuhadaa kuwa wanatupigania, wametupa majina ya kuutweza utu wetu kama "wanyonge", " walalahoi" nk.
Yote haya ni zana tu ili waaminike na kuficha uhalisia "missions" zao ovu.
Ni bahati mbaya kuwa, na sisi raia wa kawaida tumekubali na kuingia kwenye hadaa hizi na kujikuta tunaunga mkono moja ya pande maslahi hizi yaani WATAWALA na au WANAOTAKA KUZICHUKUA NAFASI ZA UTAWALA a.k.a wapinzani.
Kwa kufanya hivi, tumeifanya mission yao iwe rahisi sana. Na sisi wananchi wa kawaida katika mazingira haya, kamwe hatutakuja kupata tunayoyatamani katika nchi yetu.
Haya ninayoandika yamethibitishwa na Maalim Seif Sharif Hamad wa ACT WAZALENDO kwa kuamua kujiunga wa aliokuwa anawaona maadui zake na sisi wananchi tukaamini hivyo.
Sasa kawatelekeza na kuwaacha wananchi aliowaaminisha kuwa wakati wa kukomesha dhuluma umefika iwe jua ama mvua kwa yeye kujiunga na CCM tulioaminishwa kuwa ndiyo maadui wa ustawi wetu!
Natamani kuanzia leo nisimwamini mwanasiasa yeyote. Na ofcoz ndivyo itakavyokuwa. Na nitatumia njia zingine kabisa kupambania hali na ustawi wangu kijamii na kiuchumi.
Wamebaki kina Freeman Mbowe, Tundu Lissu na CHADEMA yao kwa ujumla. Tusishangae wakajiunga na waliotuaminisha kuwa ni maadui wa ustawi wetu.
Kweli kabisa, binadamu ni kiumbe kisicho na perfect definition. Ulivyo wewe ndugu ndivyo hivyo ulivyo. Asije mtu kukudanganya kuwa umuamini yeye na kwamba anaweza kukufanya na kukugeuza uwe mtu tofauti na alivyokuumba Mungu.