sasa ni rasmi: babu wa samunge ni bilionea!!


haka kazee kana laana! yaani kameanzia utapeli uzeeni na umekachanganyia kweli, duh!!
ama kweli wajinga ndio waliwao, na hapo samunge wameliwa kwelikweli
 
Katika hao watu million tatu, mpaka leo sijakutana ana kwa ana na mmoja alienihakikishia kuwa kapona, niliokutana nao wote, kama kumi hivi, hakuna aliepona.
 
haka kazee kana laana! yaani kameanzia utapeli uzeeni na umekachanganyia kweli, duh!!
ama kweli wajinga ndio waliwao, na hapo samunge wameliwa kwelikweli
(red)Kauli pekee inayoonyesha wewe ni MTANZANIA HALISI-hujachanganya damu!

Wivu wa kike(ref Mkapa), majungu, Uswazi na Uchawi!
Mbona mnakuwa myopic namna hii brodas?....kwanini msiongelee juu ya wanaopona HIV?
Unafik wa nini enyi wana-Iblis?...Kawaida ukitaka kuheshimika na kauli zako, jaribu kubalance story!
Binafsi naona wanaopona wengi zaidi kuliko complications..kama ni ratio nitaweka 1:500...yes!
 
Miss Judith yuko manual zaidi kuliko kufikiria uhalisia wa data ANAZOOKOTEZA.
Anasoma na kusikia kwenye redio zinazoishia MAGOMENI, na kukimbilia kubandika conclusive informatio!

How pity!...sijui ni kukanganyikiwa!

hivi na wewe unaweza kujiita great thinker kweli?

mbona dada wa watu kanukuu habari ya gazetini na kaweka link pale ya kubonyeza, unawezaje kusema kuwa kuwa kaokoteza data? unataka kutuambia kuwa gazeti la tz daima nalo linasoma hadi magomeni tu?

wewe sasa nimegundua kama sio demu lenye ID na avatar ya kidume, basi una matatizo binafsi na huyu binti kigori! no wonder umeamua kujiita nyau jimi! very funy
 
Katika hao watu million tatu, mpaka leo sijakutana ana kwa ana na mmoja alienihakikishia kuwa kapona, niliokutana nao wote, kama kumi hivi, hakuna aliepona.
Ok..kama umekutana na kumi ambao hawajapona , basi hesabu ni kama ifuatavyo:

Wasiopona ni 10/3,000,000=0.000003333333333~=0.000003%
Sasa hapo CHANGANYA na zako ili ujue wanapona ama la!

Tusifupishe maisha watu kwa kuwaza Dark-Side tu ya matters!...Life is too good to worry to that extent!
andio maana tunakufa kwa mashinikizo!
 
Katika hao watu million tatu, mpaka leo sijakutana ana kwa ana na mmoja alienihakikishia kuwa kapona, niliokutana nao wote, kama kumi hivi, hakuna aliepona.
walau kwa hilo niko tofauti. Nina rafiki yangu, akiruhusu nitaweka namba yake, alikuwa na sukari inafiki 18 hadi 20, baada ya kikombe amepima mara kadhaa anapata 4.5 hadi 5.5. Mwingine simfahamu, lakini nilikutana naye Mahakama Kuu, niliambiwa ni mtumishi pale, alikuwa anataniwa na wenzake kuwa hajapona sukari baada ya kikombe, aliwajibu kwa vitendo. ''Leta pepsi'', akanywa ya kwanza. ''leta nyingine'', akanywa na pili, ''leta ya tatu'', akanywa nyingine, nilisikia waliokuwa wakimtania awali wakisema kama hivyo amepona.
 

mhitimu wa shule ya kata kaona mwezi katika numbers!
 

too low!

kwa hiyo kunywa pepsi ndiyo kipimo cha kupona sukari?

hata kama umesoma shule za kata, this is too low!
 
Bora sisto hOYCE WAAMBIE!
Mimi binafsi nilipokea ndugu yangu toka mikoani mbali sana(mwanamke) ambaye alikuwa ana mwezi wa 3 anableed continously, na alipowasili nilishangaa kumwona na mzigo wa matambara kwenye begi kwaajiri ya kumsitiri na hilo tatizo!

Alipokwenda Samunge na kupata kikombe tu, ile kufika Arusha alikuwa keshakata damu hizo, na hadi leo naongea ni mwezi na nusu umekatika hana habari na damu tena, na alishaanza shughuli zake za kipato, wakati alishaachaga, na alikuwa anashinda amelala!
So siambiwi kitu juu ya Babu Mwasapile!
Acha wabishi ambao hawajui kuugua waendelee kuhoji, kwanza wanapunguza JAM!
 

hakuwahi kupata upungufu wa damu ?
 
hakuwahi kupata upungufu wa damu ?

Mkuu,
Alikuwa keshaattend hospital mno, na ana vidonge vya kila..
By the time anakuja kwangu alikuwa very pale, na mikono myeupe kama karatasi.
Kwa hbr anazonambia saa yuko fit vbaya mno.
 

Figo haimo katika orodha ya magonjwa anayotibu babu....Mwambie ankal wako alikurupuka! Hebu soma hii nukuu hapa chini:

Magonjwa sugu yanayodaiwa kutibiwa na kikombe hicho kinachokwenda na imani zaidi ni kisukari, shinikizo la damu, pumu, saratani na ukimwi.
 
M,kuu wangu X-Paster,
Naweza kukuunganisha toka Zanzibar hadi Samunge na Ukarudi Zenji same day!
Ni matter ya mafao mfukoni mwako tu!...ha ha haaaa!
Hayo mambo ya kusubiri utasubiri sana hadi dahari, usione kitu!
Nao watapoteza wengi...!

Mkuu wewe ndio propaganda ofisa wa iki kibabu nini?
 
.
Eeh kweli watapukutika wengi mwaka huu. Si unaona Osama alivyowatangulia?
.
Yaani kakutangulia kivipi, kuna uhusiano gani sasa hapo... Are you okay upstairs...!? Nadhani you are bit weak upstairs...! Si bure.
 
Wagonjwa 3 milioni! Kwa analytical review ya haraka haraka, hizi hesabu naona kama zina walakini!

Kama tukiassume huyu mzee hapumziki kabisa, then katika kila dakika moja anahudumia wagonjwa 6, kwa saa moja atahudumia wagonjwa 360 na kwa siku (masaa 24) atahudumia wagonjwa 8,640, na hivyo anahitaji siku 347 (karibu mwaka mmoja!) kuhudumia wagonjwa milioni tatu.
 
Nao watapoteza wengi...!

Mkuu wewe ndio propaganda ofisa wa iki kibabu nini?
Kiongozi,
Hapotezwi mtu hapa.
Kwann hamuongelei wanaopona, mnatafuta tu discrepancies zisizo na kichwa wala kiwiliwili?
Bosi wangu,
Mimi sio P/O wa Mwasapile, bali nimeona kwa macho yangu watu waliokuwa taabuni kwa miongo kadha, na sasa wamekuwa wazima.

Ukipata muafaka wa kwenda mkuu wangu niconsult, utafurahi, na utakuwa balozi wa babu visiwani.
 
Yaani kakutangulia kivipi, kuna uhusiano gani sasa hapo... Are you okay upstairs...!? Nadhani you are bit weak upstairs...! Si bure.

Bora umwambie maana watu wengine don't even think they just type and post.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…