Sasa serikali 1 ndiyo iwe msimamo kama wote Tanzania bara na Zanzibar hatutaki serikali 3.Serikali 2

Sasa serikali 1 ndiyo iwe msimamo kama wote Tanzania bara na Zanzibar hatutaki serikali 3.Serikali 2

kibaravumba

JF-Expert Member
Joined
Dec 21, 2012
Posts
6,634
Reaction score
7,015
Wote wenye hoja ya serikali tatu naamini walizingatia kutokuzitonesha hisia za, na utashi wa wazanzibari ambao wamekuwa wakionyesha kupitia viongozi wao kutoridhishwa na aina hii ya muungano wa serikali 2.Hakuna mtu wa bara anayelakamikia muungano uliopo zaidi ya kujibu kejeli na matusi yanayotolewa kwa watu wa bara kutoka kwa baadhi ya wazanzibari wakiamini eti watu wa bara(Tanganyika)wanawabana katika muungano huu kiasi kwamba zimekuwepo kauli mbiu kama "mtuache tupumue" "tunataka turuhusiwe kujiunga na OIC kwani 99% ya wakazi wa Zanzibar ni waislamu"Watu wa bara makafir na mna roho mbaya!kwa nini hamdai Tanganyika yenu?!Sisi wengine tunashangaa tu kwa vile tunajua matatizo tuliyonayo si kwa sababu ya muungano ila kutowajibika kwa watawala ambao huchangia kudidimiza maendeleo yao wakishirikiana na wanyang'anyi wa nje ya nchi wenye majina matamu kv.wawekezaji!Sasa kwa vile inaonekana serikali 3 ni nongwa na wengi kwa unafiki wanataka tubaki na serikali 2 ili, kwanza kuepuka gharama(sababu nyepesi) na, pili kuepusha kuvunja muungano(Hoja isiyo na mashiko)Basi pamoja na hoja zao dhaifu tukubali lakini,Ili kuepuka kabisa hofu ya hayo wanayosema kwenye hoja zao,waunge mkono kuundwa kwa serikali moja na serikali ya umoja wa kitaifa Zanzibar ivunjwe.Zanzibar kama bara kuwa na mawaziri wakuu ama magavana wawili chini ya rais mmoja wa JMT

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Mkuu zanzibar ni ngumu kuimeza,kama muungano ni raha basi kaunganeni na msumbiji kisha muwaambie waifute msumbuji yao uone kitakachotokezea,kwa vile watanganyika mmeukataa utanganyika wenu basi tulieni wajanja tule rasilimali zenu kiulainii,zanzibar kwanza.
 
mkuu hivi kwa nini watanganyika hatutaki kuuzungumzia wala kuudai utanganyika wetu,tunabaki kuwangangania tu wazanzbari ambao wao wanataka wajitegemee.matokeo yake wanaishia kututukana tu kwenye mitandao.huwa najisikia aibu kama mtanganyika!
 
mkuu hivi kwa nini watanganyika hatutaki kuuzungumzia wala kuudai utanganyika wetu,tunabaki kuwangangania tu wazanzbari ambao wao wanataka wajitegemee.matokeo yake wanaishia kututukana tu kwenye mitandao.huwa najisikia aibu kama mtanganyika!

Mkuu hata mimi najiuliza sana hawa watanganyika hawa,ukiwaona katika vipindi mbalimbali jinsi wanavyomtuhumu Warioba kwa kuweka maoni ya watanzania waliotaka serikali 3,inaleta mshangao kiasi kwamba naona kama huenda kuna kitu ambacho sisi baadhi yetu hatukijui kuhusu kung'ang'ania hizi serikali 2!Nilisoma mahali fulani akinukuliwa Polycarp Pengo akidai pia Tanzania hatuhitaji serikali 3 badala yake hizi 2 zinatosha.Ajabu hawaongei kabisa kuhusu katiba ya Zanzibar ilivyouvunja katiba ya Muungano bila hofu na hatma ya jambo hili ambalo mimi naona kama vile ilikuwa hatua muhimu sana kuelekea kuuvunja muungano.Na akitokea rais mbabe huko Zanzibar anaweza kwenda mbele zaidi na kuifanya Zanzibar iwe Sovereign State hata katika serikali hizi 2.

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Hakuna kukuru wala kakara ,kiherehere ni kwa waCCM wanajua fika kiama chao ni kuwepo kwa serikali tatu ,pindipo serikali tatu zikikubalika utakuwa ndio mwisho wao hao MaCCM ,Napenda ufahamu tu ,Serikali ya Tanganyika haipo ,iliopo ambayo inamaliza muda wake kipindi kifupi kiliobaki.

Uchaguzi utakaokuja ,hili mlijue wazi ,utakuwa Uchaguzi mkuu wa kwanza Tanganyika tokea ipate uhuru,:shock: zaidi wa vyama vingi ,Serikali iliyopo ya Tanzania ndio inamaliza muda wake na siku katiba ya Serikali tatu ikipita ,serikali hii inapoteza uhalali wake na kwa maana hio wale wote waliomo ndani ya serikali hii watakuwa hawana ajira ,ambao asilimia 99.99 ni CCM ya wafanyakazi serikalini ,,ndio maana mkawasikia hao akina Nape wakijitia ushujaa wa kisabuni na kujikaza wakati mvua ni kubwa na mwangaza wa Tanganyika umeshaanza kupasua kwenye Horizon.
 
CCM mkitaka msitake serikali tatu ni lazima ,kutaka kuzilinda hizo mbili mnazozitumia kutuibia maliasili na mambo kibao ni kiingiza Nchi kwenye vurugu ,hapatakalika na patakuwa hapatoshi ,hakuna asiechoka na ukiritimba wenu ,polisi,wahoi,majeshi wahoi wafanyakazi serikalini wamaji ,mnaoneemeka ni nyie wa dizaini zenu ,nyumba za mapolisi na amajeshi tunazijua huko makwao na zinatia huruma ,ndugu na jamaa zao tunawajua ,wengine huwa tunawasaidia wazee wao kwani shida nao pia inawakuta japo wanawao wamo kwenye vyombo vya dola. Ila akina vingunge wao shida kwa familia zao haziwafikii ,

CCM mtambue tu wananchi walio wengi hawapo peke yao wapo na waliomo humohumo ndani na wao hawataki hicho cha serikali mbili zibaki ,wanasubiri kitu kimoja tu wawatenge ,umoja wa ukweli wa upingaji wa serikali zilizowekwa na CCM.
 
mkuu hivi kwa nini watanganyika hatutaki kuuzungumzia wala kuudai utanganyika wetu,tunabaki kuwangangania tu wazanzbari ambao wao wanataka wajitegemee.matokeo yake wanaishia kututukana tu kwenye mitandao.huwa najisikia aibu kama mtanganyika!

Watanganyika wengi wanahisi kurudi kwa tanganyika kanisa halitopata nafasi zanzbr.
 
Serikali moja ndiyo nzuri, lakini itabidi kwanza uondoe wanasiasa wote na kuanza na generation mpya ambayo haijawahi kuonja utamu wa madaraka. Kutokana na hilo kutowezekana, jawabu linalobaki ni hilo la serikali tatu tu. Kila upande uchunge raslimali zake, halafu kwenye mambo yanayohusu Muungano kila upande ama uchangie sawasawa au uchangie proportional na idadi ya watu wake.
 
Back
Top Bottom