Sasa unaweza kuunganisha simu yako na kompyuta bila waya

Teknolojia ni Yetu sote

JF-Expert Member
Joined
Apr 28, 2020
Posts
620
Reaction score
1,240


Teknolojia inazidi kushika kasi watumiaji wa window 11 na window 10 wamewekewa mfumo Rahisi wa kuweza kuingiliana kati ya simu na kompyuta na kuweza kutumika bila shida yoyote.

Tunajua wengi mmeshawahi kutumia app ya phone link ambayo inakupa Uwezo wa kufanya mambo mbalimbali kwa kukuonyesha notification na taarifa mbalimbali za simu yako kwenye kompyuta achana na hiyo.



Sasa Microsoft wanakuletea feature mpya ambayo inafanya kazi kwa watumiaji wa window 11 na window 10 kuweza kuona vitu mbalimbali vilivyopo kwenye simu na kuvipeleka kwenye kompyuta bila kuunganisha na waya.

Utaweza kufungua file explorer utaweza kuona simu yako yote kwenye kompyuta hivyo utakua na Uwezo wa kuhamisha kitu chochote kwa urahisi bila kutumia USB waya au Phone link.

hakikisha simu yako ina support android version 11 na kuendelea Kisha ingia setting kwenye simu yako >> Bluetooth & device >>mobile device unganisha na kompyuta yako Anza kutumia.
 
Zilipendwa mbona wajanja kitambo sana

Labda tumuite na Chief-Mkwawa afafanue kama kuna jipya la 2024 kuhusu hio ishu
Kipya ni kwamba File Explorer ya windows inruhusu ku access files za Android remotely, ila hio feature sio mpya toka kipindi cha Symbian tuliweza hamisha mafile bila waya.
 
Kwa kutumia wifi ama internet, kama unatumia wifi unaweza ukawa na app moja kwenye pc na simu, kipindi cha Symbian tulitumia Dukto, sasa hivi app zimejaa kibao Air drop, xender na wengineo.

Pia waweza tumia internet (ama hata wifi) na protocol kama Ftp, tumia file manager yoyote nzuri itakua na option ya ku act kama server halafu Tengeneza ftp connection utapewa ip adress na port kwenye pc viweke my computer ama tumia browser weka details amba program kama filezilla utaweza access mafile ya simu mahala popote ulipo.
 
hakikisha simu yako ina support android version 11 na kuendelea Kisha ingia setting kwenye simu yako >> Bluetooth & device >>mobile device unganisha na kompyuta yako Anza kutumia.
Tuwekane sawa kdg, hapo ktk mobile device ndio nini kitadisplay?

Aina ya uhamishaji ni wa BT? maan navyojua Bluetooth ni outdated ktk kusafirisha taarifa kwa haraka.. watu wapo ktk WI-FI era ambayo nayo inategemea na aina yake zingine zipo slow zingine faster.

Sasa napata ukakasi kama Microsoft wameboresha huduma ya wireless transfer/ (phone cloning) then watumie BT ktk mchakato wakati ipo very slow and not reliable ukiwa umbali flan compared to WiFi ambayo inarange kubwa zaidi na ni strong.

Ikumbukwe kabla ya WiFi ilitumika BT as wireless network.. kuunganisha between simu na Pc instead of kutumia Moderms, ethernet and Usb cables...
 
Technology kama Quick transfer zinatumia vyote bt na wireless, kwa BT ni rahisi ku pair na kuvifanya vifaa vionane.
 
Weka procedures zote
 
Technology kama Quick transfer zinatumia vyote bt na wireless, kwa BT ni rahisi ku pair na kuvifanya vifaa vionane.
The ishu ni reliability... 1GB file unawez tumia less than 30 seconds ila kwa BT more than 2 minutes..

Pia Device iwe karibu as if unatumia NFC ila kwa WI-FI unawez kuw mbali hata 200+ meters na mambo yakawa mswano..
 

Attachments

  • Screenshot_20241101_001342.jpg
    270.4 KB · Views: 10
The ishu ni reliability... 1GB file unawez tumia less than 30 seconds ila kwa BT more than 2 minutes..

Pia Device iwe karibu as if unatumia NFC ila kwa WI-FI unawez kuw mbali hata 200+ meters na mambo yakawa mswano..
Soma vizuri comment yangu.

Kuelewa zaidi una pair vipi baina ya wifi na wifi? It's long process sometime mpaka umatch ip adress, Bluetooth ama Nfc ni rahisi ku pair baina ya vifaa viwili. So kazi ya kupair inafanyika na BT na kuhamisha file na wifi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…