Sasso vs Kroiler

Sasso vs Kroiler

mr Future

Member
Joined
Jan 26, 2019
Posts
69
Reaction score
84
Habari wakuu,!
Nimeamua kuanza ufugaji wa kuku chotara,
Napenda kujuzwa zaidi ni mbegu ipi nzuri kati ya hizi
1:sasso
2: Kroiler
3:kuku wa Malawi
Katika vipengele hv
1:utagaji 2:ustahimilivu wa magonjwa 3: Kasi ya ukuaji
Pia anayefahamu mtiririko wa ulishaji karibu
Karibuni wote Kwa kunipa msaada
 
Naomba nikujibu kama ifwatavyo lakini nitajibu kutokana na ulivyo uliza Mkuu

Angalizo sipo apa kebeza aina ya kuku bali najibu kutokana na uzoefu nilio kuwa nao


✓ Utagaji
Kwanza kabisa hao kuku wote ulio wataja apo juu ni chotara Yani asilimia 50 ni kwaajili ya nyama ( bloire) pia asilimia 50 ni kwaajili ya mayai ( layers) ivo chakula ndicho kitakacho amua kuku wako awe katika kundi lipi
Utagaji wa hao kuku Ina kadiliwa ni week ya 21 kwanzia kutotolewa na wastani huwa wanataga mayai mawili ndani ya siku tatu. Vitu vya kuzingatia ili kuku hao watage kwa asilimia kubwa ni
1 chakula
Ili kuku wako awe kwa ajili ya kutaga inabid apewe chakula kutokana na umli pamoja na uzito alio nao kwaiyo kwanzia
∆ 1-8 week inabidi apewe chakula chenye asilimia 18-20 ya protein
∆ 9-16 week inabidi apewe chakula chenye asilimia 16-18 ya protein
∆ 17 na kuendelea inabid apewe chakula chenye asilimia 18-20 ya protein

Siku nikipata muda nitatoa ufafanuzi jinsi ya kutengeneza chakula ili kuweza kupata izo asilimia za protein

2 kiasi Cha chakula
Kuku inabid ale kutokana na uzito wake
∆ 1-4 week inabidi apewe chakula muda wote bila kipimo masaa 24
∆ 5-8 week inabid apewe 50-90 gram kwa kuku masaa 16
∆ 9-16 week inabid apewe 95-115 gram kwa kuku masaa 16
∆ 17 na kuendelea inabidi apewe 120-125 gram kwa kuku masaa 16

3 mwanga
Kuku anavyo Anza kutaga Yani week ya 20 na kuendelea inabid apate masaa 16 ya mwanga na masaa 8 ya Giza ili Kuongeza uzalishaji wa homorne itakayo pelekea utagaji utakuwa juu

4 usafi
Banda inabid liwe safi pia vyombo vya maji na chakula inabid visafishwe

6 uokotaji wa mayai
Kuku aina ya chotara huwa wanachukua muda mrefu kwenye Maandalizi ya utagaji ivyo kama kukuwa na mayai kwenye kiota itamfanya asiwe huru kutokana na kuzuiwa na mayai ivyo inabid mayai yaokotwe mara kwa mara

✓ Magonjwa
Apo kuku wote huwa wanasumbuliawa na mangojwa ivyo chanjo na dawa ni muhimu kwa kuku wote. Mtililiko wa chanjo ni kama ufuatavyo

∆ siku ya Saba inabid uwape Newcastle kwaajili ya kideli

∆ siku ya Kumi na nne inabidi uwape Gumboro kwaajili ya Mdondo

∆ siku ya ishirini na moja inabid uwape Newcastle kwaajili ya kideli

∆ siku ya ishirini na nane inabidi uwape Gumboro kwaajili ya Mdondo

∆ siku ya thelasini na Tano inabid uwape chanjo ya Ndui Yan Flow pox

Ukizingatia izo chanjo apo juu na usafi kwenye mabanda yako Magonjwa kwako yatakuwa ni historia.
Kwa upande wa Sasso wenywe huwa awapewi iyo chanjo ya Gumboro kutokana na maelezo Yao so sitayaweka apa maana ni mambo ya biashara


∆ Kasi ya ukuaji
Hao kuku wote ukuaji wao ni sawa maana swala la ukuwaji Lina tegemeana na vitu vingi kama vile chukula, Magonjwa, Huduma kuku anazo pata pamoja na usafi wa mazingira
Lkn kwenye upande wa uzito Sasso yupo juu kuzidi wote maana yeye ni mfupi kidogo kwa kroiler

Endapo ukitaka kuku wako wakuwe haraka inabidi uwape chakula chenye asilimia 20-25 ya protein Yani ndani ya miiezi miwili wanaeweza kuwa na kilo 2.5-3.5 lkn nyama yao itakuwa sio tamu maana umelazimisha wakuwe haraka ivyo ukuaji wa tissue umelazimishwa itapelekea bahadhi ya pigment azitakuwepo ivyo nyama itakuwa ya kawaida tuu
 
Naomba nikujibu kama ifwatavyo lakini nitajibu kutokana na ulivyo uliza Mkuu

Angalizo sipo apa kebeza aina ya kuku bali najibu kutokana na uzoefu nilio kuwa nao


✓ Utagaji
Kwanza kabisa hao kuku wote ulio wataja apo juu ni chotara Yani asilimia 50 ni kwaajili ya nyama ( bloire) pia asilimia 50 ni kwaajili ya mayai ( layers) ivo chakula ndicho kitakacho amua kuku wako awe katika kundi lipi
Utagaji wa hao kuku Ina kadiliwa ni week ya 21 kwanzia kutotolewa na wastani huwa wanataga mayai mawili ndani ya siku tatu. Vitu vya kuzingatia ili kuku hao watage kwa asilimia kubwa ni
1 chakula
Ili kuku wako awe kwa ajili ya kutaga inabid apewe chakula kutokana na umli pamoja na uzito alio nao kwaiyo kwanzia
∆ 1-8 week inabidi apewe chakula chenye asilimia 18-20 ya protein
∆ 9-16 week inabidi apewe chakula chenye asilimia 16-18 ya protein
∆ 17 na kuendelea inabid apewe chakula chenye asilimia 18-20 ya protein

Siku nikipata muda nitatoa ufafanuzi jinsi ya kutengeneza chakula ili kuweza kupata izo asilimia za protein

2 kiasi Cha chakula
Kuku inabid ale kutokana na uzito wake
∆ 1-4 week inabidi apewe chakula muda wote bila kipimo masaa 24
∆ 5-8 week inabid apewe 50-90 gram kwa kuku masaa 16
∆ 9-16 week inabid apewe 95-115 gram kwa kuku masaa 16
∆ 17 na kuendelea inabidi apewe 120-125 gram kwa kuku masaa 16

3 mwanga
Kuku anavyo Anza kutaga Yani week ya 20 na kuendelea inabid apate masaa 16 ya mwanga na masaa 8 ya Giza ili Kuongeza uzalishaji wa homorne itakayo pelekea utagaji utakuwa juu

4 usafi
Banda inabid liwe safi pia vyombo vya maji na chakula inabid visafishwe

6 uokotaji wa mayai
Kuku aina ya chotara huwa wanachukua muda mrefu kwenye Maandalizi ya utagaji ivyo kama kukuwa na mayai kwenye kiota itamfanya asiwe huru kutokana na kuzuiwa na mayai ivyo inabid mayai yaokotwe mara kwa mara

✓ Magonjwa
Apo kuku wote huwa wanasumbuliawa na mangojwa ivyo chanjo na dawa ni muhimu kwa kuku wote. Mtililiko wa chanjo ni kama ufuatavyo

∆ siku ya Saba inabid uwape Newcastle kwaajili ya kideli

∆ siku ya Kumi na nne inabidi uwape Gumboro kwaajili ya Mdondo

∆ siku ya ishirini na moja inabid uwape Newcastle kwaajili ya kideli

∆ siku ya ishirini na nane inabidi uwape Gumboro kwaajili ya Mdondo

∆ siku ya thelasini na Tano inabid uwape chanjo ya Ndui Yan Flow pox

Ukizingatia izo chanjo apo juu na usafi kwenye mabanda yako Magonjwa kwako yatakuwa ni historia.
Kwa upande wa Sasso wenywe huwa awapewi iyo chanjo ya Gumboro kutokana na maelezo Yao so sitayaweka apa maana ni mambo ya biashara


∆ Kasi ya ukuaji
Hao kuku wote ukuaji wao ni sawa maana swala la ukuwaji Lina tegemeana na vitu vingi kama vile chukula, Magonjwa, Huduma kuku anazo pata pamoja na usafi wa mazingira
Lkn kwenye upande wa uzito Sasso yupo juu kuzidi wote maana yeye ni mfupi kidogo kwa kroiler

Endapo ukitaka kuku wako wakuwe haraka inabidi uwape chakula chenye asilimia 20-25 ya protein Yani ndani ya miiezi miwili wanaeweza kuwa na kilo 2.5-3.5 lkn nyama yao itakuwa sio tamu maana umelazimisha wakuwe haraka ivyo ukuaji wa tissue umelazimishwa itapelekea bahadhi ya pigment azitakuwepo ivyo nyama itakuwa ya kawaida tuu
Ahsante sana mkuu!!, Nimekuelewa,
Je nikifuga sasso ndani ya miezi mitatu naweza uza kwaajili ya nyama Kwa Bei walau ya TSH 10,000/= au zaidi,?
 
Ahsante sana mkuu!!, Nimekuelewa,
Je nikifuga sasso ndani ya miezi mitatu naweza uza kwaajili ya nyama Kwa Bei walau ya TSH 10,000/= au zaidi,?
Miezi mitatu unaweza kuuza Tete kwa gharama ya 10000-12000 na Jogoo 15000-18000
 
Habari wakuu,!
Nimeamua kuanza ufugaji wa kuku chotara,
Napenda kujuzwa zaidi ni mbegu ipi nzuri kati ya hizi
1:sasso
2: Kroiler
3:kuku wa Malawi
Katika vipengele hv
1:utagaji 2:ustahimilivu wa magonjwa 3: Kasi ya ukuaji
Pia anayefahamu mtiririko wa ulishaji karibu
Karibuni wote Kwa kunipa msaada
Hao sio kuku wa Biashara kama unataka kufuga kuku wa Biashara fuga kuku wa mayai wa kisasa na kuku wa nyama.

Chotara ni hasara kuwa fuga na huwezi pata bei nzuri, kwa mkupuoa, Ili upate bei nzuri labda uwauzie watu wa kwenda kuchinja wale na hawa ni mmoja mmoja, pia Chotara hao sio watagaji kabisa sasa usiwapigie mahesabu ya kuuza mayai yao.

Kama uko mjini miji mikubwa fuga kuku wa mayai au Broiler, achana na hawa Chotara, utakuja baadae humu na story za kupumzisha mabanda jwa muda baada ya kuwa wamekufanya ndivyo sivyo
 
Yeah lakini Kwa huku Dodoma soko lipo, kwasabu nimewah uza wa kienyeji pure mara kadhaa Kwa mkupuo wa kuku Zaid ya 20 Kwa Bei ya juu, na kuhusu chotara soko lipo kwenye bar ,hotels na restaurants, pia yupo ndugu yang aliwafuga wakaumwa akawauz Kwa Bei ya sh 5000 kilo mmoja Tena wakiwa wagonjwa
 
Yeah lakini Kwa huku Dodoma soko lipo, kwasabu nimewah uza wa kienyeji pure mara kadhaa Kwa mkupuo wa kuku Zaid ya 20 Kwa Bei ya juu, na kuhusu chotara soko lipo kwenye bar ,hotels na restaurants, pia yupo ndugu yang aliwafuga wakaumwa akawauz Kwa Bei ya sh 5000 kilo mmoja Tena wakiwa wagonjwa
Kwa hiyo tulikula kibudu?
 
hellow. ukiachana na sasso na kroiler. kuna TANBRO ni spec nzuri sana kwa ajili ya mayai, nyama au vyote kwa pamoja. pia tunauza broilers, layers.. nipigie au whatsapp 0716883266
Weka picha za hao tanbro tuwaone kwanza
 
Back
Top Bottom