Uchaguzi 2020 SAU wazindua Kampeni na Ilani kwa vitendo. Watumia Trekta Kulima kuonesha dhamira ya Kumtoa Mtanzania kwenye Jembe la Mkono

Uchaguzi 2020 SAU wazindua Kampeni na Ilani kwa vitendo. Watumia Trekta Kulima kuonesha dhamira ya Kumtoa Mtanzania kwenye Jembe la Mkono

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Salaam Wakuu,

Chama cha sauti ya umma (SAU) Kimezindua Kampeni na Ilani kwa Vitendo, Baada ya Kutumia Trekta kama mfano wa Jinsi Watanzania Watakavyokuwa Wanalima Pindi Wakipewa Nafasi ya Kuongoza Nchi. Wamezindua kwa kuvuna Miwa na Viazi Shambani.

Uzinduzi wa ilani umefanyika kivitendo katika eneo la KWAZOO kata ya buyuni na baadae mkutano wa uzinduzi eneo la MOMBASA karibu na stand ya mabus katika Jimbo la Ukonga jijini Dar es Salaam.

Vipaumbele vya SAU ni;

1. Huduma ya maji Safi na salama bure
2. Eliimu mpka chuo bure
3. Matibabu bure
4. Kilimo cha kisasa nana kuwezesha kilimo hai(organic farming)

5. Kuwawezesha wakulima mikopo na kulimiwa kwa trekta bure na kuja kulipa baada ya kuuza kwasababu serikali ya SAU ita watafutia masoko ya uhakikika wakulima

6. Kutokana na migogoro mingi ya ardhi, Wizara ya ardhi itakuwa kuwa chini ya rais na Wizara zote zitakuwa 12

7. Serikali ya SAU itakuwa ya kilimo na viwanda
8. Atamteua Ummy Mwalimu na Kassim Majaliwa kuwa Mawaziri

Zaidi soma: Sauti ya Umma (SAU): Ilani ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani

Uchaguzi 2020 - Mgombea Urais kupitia SAU, Muttamwega Mgaywa na mgombea mwenza wamewasili Ofisi za NEC peku kuchukua fomu

Chama cha Sauti ya Umma (SAU) kimezindua Ilani na kampeni zake kwa ajili uchaguzi unaotarajia kufanyika Oktoba 28, mwaka huu, huku kikiahidi kuwa endapo kikishika dola huo utakuwa mwisho ma matumizi ya jembe la mkono nchini na kila mkoa utakuwa na ndege yake kwa ajili ya kubeba abiria.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa ilani na kampeni za chama hicho jana, jijini Dar es Salaa, mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania, Muttamwega Mgaywa alisema ilani ya chama hicho imelenga kuikomboa nchi kupitia kilimo na viwanda.

Alisema chini ya uongozi wa Serikali ya SAU, hakuna mkulima atakayelima Kwa kutumia jembe la mkono, badala yake trekta ndizo zitakazotumika ili kumpunguzia mzigo kwa mkulima.

Pia aliahidi kuwa chini ya Serikali ya chama hicho, wanawake watakuwa wakijifungua bure.

Aidha, ameongeza kuwa iwapo atachaguliwa ataendeleza kazi nzuri iliyofanywa na marais waliopita hususani awamu ya tano

Kuhusu suala la ardhi na Maywa amesema kila Mtanzania atamiliki ardhi bila gharama yoyote.
Kwa upande wake mgombea mwenza wa chama hicho, Satia Musa Bebwa amewahakikishia vijana wanaomaliza elimu ya juu kupata mitaji itakayowawezesha kuingiza kipato.
1600020440749.png

Kutoka Kushoto: Mgombea urais wa Zanzibar, Issa Mohamed Zonga, Katikati mgombea urais wa Tanzania Muttamwega Bhatt Mgaywa, na Kulia mgombea mwenza Bi. Satia Mussa Bebwa
1600020620472.png

1600020269632.png

Mgombea Urais wa Tanzania kuptia SAU, Muttamwega Bhatt Mgaywa Kulia na Mgombea mwenza bi. Satia Mussa Bebwa
Wakizindua ilani Kilimo na Viwanda kwa vitendo
1600020660138.png
1600020679799.png

1600020726591.png

 

Attachments

Angalau ilani Yao inaeleweka japo wamejikita Sana eneo moja kubwa la kilimo sekta nyingine muhinu illani haijagusa mfano Sekta ya biashara madini nk lakini wamejitahidi kueleweka japo fix nyingi hawajaeleza hayo masoko watatafutaje nk
 
Kwanza waseme walienda kuiba miwa kwenye shamba la nani? Na wamelipa hizo miwa? Mwitamwega na yeye anataka kuwa na akili kama za ndugu yake Musiba.
 
Angalau ilani Yao inaeleweka japo wamejikita Sana eneo moja kubwa la kilimo sekta nyingine muhinu illani haijagusa mfano Sekta ya biashara madini nk lakini wamejitahidi kueleweka japo fix nyingi hawajaeleza hayo masoko watatafutaje nk
Kura yako ni muhimu kwao hao ndio wazalendo wa kweli
 
Angalau SAU wamejikita kwenye kilimo.Sio yule mwengine kakomaa na Magufuli mwanzo mpaka mwisho.
 
Angalau SAU wamejikita kwenye kilimo.Sio yule mwengine kakomaa na Magufuli mwanzo mpaka mwisho.
Shetani hakemewi mara moja...... Si unaona kila magufuli akikemewa na Lissu anaweweseka kinyama...... 😂😂

Hapa ni spana tu kutoka kwa Tundu Lissu 👍👍
 
Ilani iko vizuri sana asilmia kubwa ya watanzania ni wakulima na wafugaji hivyo kujikita Sana eneo hili itatoa ajira nyingi sana kwao watanzania

Hii ya kiko hai ndio yenyewe hasaaa

Sent from my TECNO LC6 using JamiiForums mobile app
 
Shetani hakemewi mara moja...... Si unaona kila magufuli akikemewa na Lissu anaweweseka kinyama...... [emoji23][emoji23]

Hapa ni spana tu kutoka kwa Tundu Lissu [emoji106][emoji106]
Mpaka sasa Lissu aeleweki sera yake ni ipi.anabwabwaja tu wala hana hoja wala sera.
 
Kila mkoa uwe na 🛩🛫🛩 yake. Nafikiria uko angani itakuwaje
 
Katika vyote hayo mambo ya kuhubiri bure itafanya nisiwachague... hakuna nchi inaendelea bila wananchi wake kujishughulisha na gharama za uendeshaji maisha ambapo huchochea ukuwaji wa uchumi...

Bure for what? hata CCM mambo ya bure ni kuwaongezea wengine mzigo usio na sababu... wote tufanye kazi tujenge nchi na tutumie vipato vyetu kujipatia huduma muhim.
 
Angalau ilani Yao inaeleweka japo wamejikita Sana eneo moja kubwa la kilimo sekta nyingine muhinu illani haijagusa mfano Sekta ya biashara madini nk lakini wamejitahidi kueleweka japo fix nyingi hawajaeleza hayo masoko watatafutaje nk


lakini angalau kidogo wamejitahidi kuliko mbuzi flan za ufipa
 
Back
Top Bottom